Mkuu wa wilaya ya Iringa Mhe.Mohamed Moyo ametoa siku 14 kwa Halmashauri ya Manispaa ya Iringa kumkabidhi majengo 45 ya Madarasa yanayojengwa kupitia fedha za Ruzuku ya Serikali.
Mhe Moyo meyasema hayo leo tarehe 24/11/2022 wakati wa ziara yake ya kukagua miradi hiyo na kutoridhishwa na hatua zilizofikiwa kwenye baadhi ya madarasa ambayo yalianza kujengwa mwezi October mwaka huu.
Moyo amesema wataalamu wazingatie ubora wa majengo wanayojenga ukilinganisha na thamani ya fedha waliyopewa kutekeleza miradi hiyo.
Akikagua ujenzi huo amewataka wakuu wa Shule na watendaji wa kata kuwashirikisha Madiwani na wanachi katika hatua mbalimbali za ujenzi kwani miradi hiyo ni ya wananchi hivyo wanapaswa kufahamu kila hatua.
'Nasema hivi washirikisheni Madiwani wenu maendeleo ya ujenzi kila wiki wapate taarifa tunaelewana?alihoji Moyo'
Aidha Moyo amemtaka Mkurugenzi kujipanga vyema kuhakikisha vyumba vyote vinakamilika kwa wakati huku kila darasa likiwa na Viti na Meza tayari kwa ajili ya kutumiwa na wanafunzi wa kidato cha kwanza mwaka 2023.
Dr.Stephen Ngwale ni kaimu Mkurugenzi Manispaa ya Iringa amesema amepokea maagizo ya Mkuu wa Wilaya na kuwa atatekeleza maagizo hayo kwa wakati.
Halmashauri ya Manispaa ya Iringa ilipokea fedha kiasi cha sh.milioni mia tisa zilizotolewa na Rais wa Jamhuri wa Muungano wa Tanzania Mhe.Samia Suluhu kwa ajili ya ujenzi wa vyumba 45 vya madarasa yatakayomaliza tatizo la upungufu wa madarasa kwa wanafunzi wa kidato cha kwanza Manispaa ya Iringa kwa mwaka 2023.
Tupe Kayinga ni Afisa Elimu Sekondari Manispaa ya Iringa anamshukuru Rais wa awamu ya sita Mhe Samia Suluhu kwa kifungua pochi na kutupa fedha za madarasa.
Ziara hiyo ya siku moja ilihudhuriwa na Wakuu wa Sehemu na vitengo,viongozi wa CCM ngazi ya kata,waheshimiwa Madiwani ,watendaji wa Kata na maafisa Maendeleo ya jamii wa kata.
Imetolewa na Kitengo cha mawasiliano Serikalini-Manispaa ya Iringa.
Iringa Municipal Council
Sanduku la Posta: 162
Telephone: +255-2702647
Mobile: 255-2702647
Email: md@iringamc.go.tz
hakimiliki@2017Iringa Manispaa haki zote zimehifadhiwa