Mstahiki Meya wa Manispaa ya Songea Mhe Michael Mbano ameongoza timu ya Waheshimiwa Madiwani ,Mwenyekiti wa CCM Wilaya ndugu Said Rubeya pamoja na timu ya wataalamu kutoka Manispaa ya Iringa kutembelea Machinjio ya kisasa iliyopo Katta ya Tanga Manispaa ya Songea mapema wiki hii kwa lengo la kujifunza namna inavyoendeshwa na kusimamiwa tozo , masuala ya kiutawala na kubadilishana mawazo katika masuala mbalimbali ya maendeleo.
Mstahiki Meya wa Manispa ya Iringa Mhe Ibrahim Ngwada amesema ziara hiyo itasaidia kuboresha machinjio ya Ngelewala iliyopo Halmashauri ambayo imeanza kufanya kazi kwa mfumo usio wa kisasa..
"Tumekuja ili tujifunze na naamini tutaenda kuiboresha machinjio yetu ya Ngelewala kutokana na haya tuliyoyaona hapa Songea alisema Ngwada."
Naye Mstahiki Meya wa Manispaa ya Songea Mhe Michael Mbano amewakariibisha wageni na kuwaongoza kutembelea mradi huo ambapo alihakikisha wanaridhika na maelezo yaliyotolewa na wataalam kuhusiana na usimamizi na uendeshaji wa Machinjio hiyo ya kisasa huku akitoa ushirikiano mkubwa na ufafanuzi wa maswali yaliyoulizwa na wajumbe wa ziara hiyo walioonesha kiu kubwa ya kujifunza mambo mbali mbali yahusuyo machinjio hiyo.
Dr.Michael Segamiko ni Mkurugenzi wa Manispaa ya Songea amesema Machinjio ya kisasa ya Manispaa ya Songea imegharimu kiiasi cha shilingi bilioni 5.7 na imeanza kutoa huduma ingawa haijakamilika kwa asilimia 100.
Aidha amesema Manispaa ya Songea ni moja Kati ya Miji michache yenye Machinjio ya Kisasa inayotumia mitambo ya kisasa.nchini Tanzania.
Kwa upande wao Baadhi ya Madiwani Wa Manispaa ya Iringa wamesema wamenufaika na ziara hiyo na kuahidi kuyatendea kazi waliyojifunza kwa maendelei ya Manispaa ya Iringa.
Iringa Municipal Council
Sanduku la Posta: 162
Telephone: +255-2702647
Mobile: 255-2702647
Email: md@iringamc.go.tz
hakimiliki@2017Iringa Manispaa haki zote zimehifadhiwa