Manispaa ya Iringa kwa mwaka wa fedha 2017/ 2018 imechangia kiasi cha Shilingi Milioni 123,173,750/= kwa ajili ya kuendeleza Miradi ya Maendeleo kwa ngazi ya Kata ambapo jumla ya Kata 15 zimepokea fedha hizo kati ya Kata 18 zilizo katika Manispaa ya Iringa.
Mgawanyo wa fedha kwenye Kata umetengwa kulingana na utekelezaji wa Miradi ya Maendeleo kwenye Kata ambapo Kata zilizopokea fedha ni Kata ya Kitanzini, Mshindo, Mivinjeni Mlandege, Ilala, Mkwawa, Kihesa, Mwangata, Kitwiru, Mtwivila, Ruaha, Isakalilo, Nduli, Igumbilo na Mkimbizi.
Aidha, Miradi iliyotengewa fedha ni pamoja na mradi wa ukarabatiwa Ofisi Kata ya Mshindo utakaotumia kiasi cha shilingi 5,000,000/=, ukarabati wa Ofisi Kata ya Kitanzini utakaotumia kiasi cha shilingi 5,000,000/= na kusaidia Ukarabati wa Ofisi ya Kata ya Mtwivila kwa gharama ya shilingi 8,000,000/=
Miradi mingine ni ukamilisha wa nyumba ya Mwalimu Shule ya Msingi Mlangali Kata ya Mlandege utakaogharimu shilingi 10,000,000/=, ukamilishaji wa Matundu ya vyoo Shule ya Msingi Nyumbatatu Kata ya Ilala utakao ghalimu shilingi 5,000,000/=, kusaidia ujenzi wa Madarasa Shule ya Msingi Njiapanda Kata ya Isakalilo shilingi 12,000,000/=, kusaidia Ujenzi wa Madarasa Shule ya msingi Ndiuka Kata ya Igumbilo utakaoghalimu shilingi 5,000,000/=, kusaidia ujenzi wa darasa Shule ya Msingi Igumbilo Kata ya Igumbilo utakaoghalimu shilingi 5,000,000/=, kusaidia ukamilishaji wa vyumba viwili vya madarasa Shule ya Msingi Mawelewele Kata ya Mwangata utakaoghalimu kiasi cha shilingi 8,000,000/= pamoja na kusaidia ukamilishaji wa nyumba ya mwalimu Shule ya Msingi Ukombozi Kata ya Mkimbizi ambao utagharimu kiasi cha shilingi 10,000,000/=
Katika kuendelea kuchangia Miradi ya Maendeleo Manispaa ya Iringa imechangia ununuzi wa viti na meza 100 kwa gharama ya shilingi 5,000,000/= katika ya Shule ya Msingi Nduli iliyopo Kata ya Nduli, ukamilishaji wa vyoo katika Shule ya Sekondari Mivinjeni iliyopo Kata ya Mivinjeni kwa gharama ya shilingi 8,000,000/=, kusaidia ukamilishaji wa vyumba vya Madarasa katika Shule ya Sekondari Ipogolo iliyopo Kata ya Kitwiru kwa gharama ya shilingi 8,000,000/= na kusaidia ujenzi wa madarasa katika Shule ya Sekondari Tagamenda iliyopo Kata ya Ruaha kwa gharama ya shilingi 8,000,000/=.
Aidha Manispaa imetoa kiasi cha shilingi milioni 15,000,000/= ili kusaidia ujenzi wa wodi ya Zahanati ya Itamba iliyopo Kata ya Mkwawa na kiasi cha shilingi 6,173,750/= kwaajili ya ukamilishaji wa Soko la Ngome katika Kata ya Kihesa.
Iringa Municipal Council
Sanduku la Posta: 162
Telephone: +255-2702647
Mobile: 255-2702647
Email: md@iringamc.go.tz
hakimiliki@2017Iringa Manispaa haki zote zimehifadhiwa