Mstahiki Meya wa Manispaa ya Iringa Mhe. Ibrahimu Ngwada amewapongeza wanafunzi waliohitimu kidato cha nne ambao ni yatima wanaolelewa katika kituo cha Rahma Ophanage kilichopo Mkimbizi Manispaa ya Iringa huku akiwataka kusoma zaidi.
Mh. Ngwada ameyasema hayo kwenye hafla fupi iliyofanyika kituoni hapo kwa lengo la kuwapongeza wahitimu hao ambapo alimshukuru mjumbe wa baraza kuu la Taifa( MNEC) Salim Abri na familia yake ambao wameamua kuwalea watoto hao yatima kama watoto wa familia yao.
Aidha Ngwada amewataka wahitimu kujiendeleza zaidi kimasomo kwani fursa wanayo hivyo waitumie vizuri kuhakikisha wanafikia malengo yao.
Naye mlezi wa wahitimu hao Ndugu Salim Asas amesema pamoja na wahitimu kumaliza kidato cha nne anawapongeza kwa hatua hiyo lakini wataendelea kubaki na kuhudumiwa katika kituo hicho mpaka wafikie Elimu ya juu kwani hao ni familia ya Salim Abri.
Kituo cha Rahma Ophanage kilianzishwa mnamo mwaka 2017 katika eneo la makao mapya Igeleke kwa lengo la kuwasaidia watoto yatima na kimesajiliwa mwaka 2019 chini ya usimamizi wa Familia ya Salim Abri.
Iringa Municipal Council
Sanduku la Posta: 162
Telephone: +255-2702647
Mobile: 255-2702647
Email: md@iringamc.go.tz
hakimiliki@2017Iringa Manispaa haki zote zimehifadhiwa