• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
HALMASHAURI YA MANISPAA YA IRINGA
HALMASHAURI YA MANISPAA YA IRINGA

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA OFISI YA RAIS TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA HALMASHAURI YA MANISPAA YA IRINGA

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Mipango Miji
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Afya
      • Maji
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Environment and Cleaning
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Kazi
    • Vitengo
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji nyuki
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Ufugaji
    • Kilimo
  • Huduma zetu
    • Huduma ya elimu
    • Huduma ya Afya
    • Huduma ya Maji
    • Huduma ya kilimo
    • Huduma ya Uvuvi
    • Huduma ya Ufugaji
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu
    • Ratiba ya Vikao
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati wa Halmashauri
    • Ripoti
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Maktaba ya picha
    • Video za shughuli za ofisi au Kitaifa
    • Hotuba

BENKI YA CRDB YATOA MADAWATI 50 SHULE YA MSINGI UYOLE IRINGA MC

Posted on: May 28th, 2024

Shule ya Msingi Uyole iliyopo katika Halmashauri ya Manispaa ya Iringa imepokea jumla ya madawati 50 kutoka benki ya CRDB kama sehemu ya kurudisha fadhila kwa jamii.

Akizungumza katika halfa fupi ya makabidhiano ya Madawati hayo, iliyofanyika Shuleni hapo, Mstahiki Meya wa Halmashauri ya Manispaa ya Iringa Mhe. Ibrahim Ngwada amesema kuwa anawashukuru wadau hao kwa mchango wa madawati kwani utasaidia kwa kiasi kikubwa kutatua tatizo la upungufu wa madawati lililopo shuleni hapo.

" Lengo la benki sio kufanya biashara zake tu, bali pia kusaidia jamii iliyopo. Kwa niaba ya Wanairinga na Halmashauri nawashukuru sana kwa msaada wa madawati mlioutoa kwetu. Shule hii ni mpya na ya kisasa imegharimu zaidi ya Tsh. Milioni 300. Tumechonga madawati 105 na meza 30. Tulitarajia kusajili wanafunzi 315, lakini mpaka sasa walioandikishwa ni 460. Hivyo kutokana na ongezeko la wanafunzi, tumekuwa na upungufu wa madawati". Amesema Ngwada.

Aidha, Meneja wa CRDB Kanda ya kati, Ndg. Chabu Mishwamo amesema kuwa wao kama wadau wakubwa wa serikali wana wajibu wa kuchangia katika shughuli mbalimbali za kijamii na kuungana na kuisaidia Serikali ambayo imefanya kazi kubwa sana ya kujenga madarasa mengi nchini Tanzania.

" Tumekuja mahali hapa Uyole kwa ajili ya kuleta madawati,  Sisi kama wadau tuna wajibu wa kuangalia ni kwa namna gani tunasaidia Serikali kwa ajili ya kujenga Taifa bora hapo baadae, kwa mahali hapa tumeleta madawati 50 ambayo yataleta tija na chachu kwa wanafunzi wetu kuhudhuria darasani na kuketi, kujifunza na kuwa wazalendo". Amesema Mishwamo.

Mwenyekiti wa Serikali ya Mtaa Ndg. Justine Sanga ameishukuru Serikali kwa ujenzi wa Shule hiyo ya Uyole kwani imesogeza huduma na imesaidia kupunguza ajali kwa wanafunzi waliokuwa wakisafiri umbali mrefu.


Aidha  Sanga ameishukuru Benki ya CRDB kwa msaada wa madawati hayo, kwani bado shule ilikuwa na uhitaji.

Awali akisoma taarifa fupi ya shule hiyo Mwalimu Mkuu Ndg.J oseph Millinga amesema, Shule ya Uyole ilijengwa kwa ajili ya kupunguza msongamano wa wanafunzi uliokuwa katika Shule ya Msingi Kitwiru, pia ilijengwa ili kupunguza ajali za wanafunzi waliokuwa wanasafiri umbali mrefu. Shule ilifunguliwa rasmi mwezi Januari, 2024 kwa usajili wa wanafunzi  waliohamia 306. Mpaka sasa imesajili zaidi ya wanafunzi 400.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUONGEZWA MUDA WA KUCHUKUA FOMU YA UJENZI WA JENGO LA BIASHARA TEMBO BAR February 15, 2024
  • MATOKEO YA KIDATO CHA SITA, 2023/2024 July 13, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI July 17, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI July 23, 2024
  • Soma zote

Habari za Hivi punde

  • PPP CENTRE YATOA MAFUNZO KWA WATAALAMU IRINGA MC

    April 04, 2025
  • ALUTE: "HAKIKISHENI MIRADI INAKAMILIKA KWA WAKATI NA KWA UBORA"

    December 21, 2024
  • UCHAGUZI HURU NA WA HAKI UNAHITAJI USHIRIKISHAJI - RC SERUKAMBA

    October 10, 2024
  • MSIGALA AWAONYA MAAFISA MAENDELEO KUJIHUSISHA NA MIKOPO HEWA

    October 05, 2024
  • Soma zote

Video

MEYA WA MANISPAA KUZIPIGANIA TIMU ZA MKOA KUPANDA DARAJA
More Videos

Viunganisho vya Haraka

  • National Examination Council of Tanzania
  • Watumishi Portal
  • MATOKEO YA KIDATO CHA SITA,2023/2024
  • Sheria ndogo za Manispaa
  • Vivutio vya Utalii na Taarifda zake
  • Taarifa kwa vyombo vya Habari

Tovuti Zinazofanana

  • Goverment Website
  • TAMISEMI
  • Iringa Region Website
  • IMtv Fahari ya Iringa

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

https://bachelorthesiswritingservice.com

Location Map

Wasiliana nasi

    Iringa Municipal Council

    Sanduku la Posta: 162

    Telephone: +255-2702647

    Mobile: 255-2702647

    Email: md@iringamc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya usiri
    • Ukanusho
    • MMM
    • Ramani ya eneo
    • Huduma zetu

hakimiliki@2017Iringa Manispaa haki zote zimehifadhiwa