• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
HALMASHAURI YA MANISPAA YA IRINGA
HALMASHAURI YA MANISPAA YA IRINGA

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA OFISI YA RAIS TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA HALMASHAURI YA MANISPAA YA IRINGA

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Mipango Miji
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Afya
      • Maji
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Environment and Cleaning
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Kazi
    • Vitengo
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji nyuki
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Ufugaji
    • Kilimo
  • Huduma zetu
    • Huduma ya elimu
    • Huduma ya Afya
    • Huduma ya Maji
    • Huduma ya kilimo
    • Huduma ya Uvuvi
    • Huduma ya Ufugaji
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu
    • Ratiba ya Vikao
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati wa Halmashauri
    • Ripoti
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Maktaba ya picha
    • Video za shughuli za ofisi au Kitaifa
    • Hotuba

MSIGALA AWAONYA MAAFISA MAENDELEO KUJIHUSISHA NA MIKOPO HEWA

Posted on: October 5th, 2024

Mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa ya Iringa Ndg. Kastori Msigala amewaonya Maafisa Maendeleo ya jamii wa Manispaa ya Iringa kutojihusisha na utoaji wa mikopo hewa kwa vikundi vya wanawake, vijana na makundi maalumu kwani wakifanya hivyo watachukuliwa hatua kali za kisheria.

Msigala ameyasema hayo katika Ukumbi wa Manispaa ya Iringa wakati akifungua Mafunzo ya Muongozo Mpya wa Usimamizi na Utoaji Mikopo ya Vikundi vya Wanawake, Vijana na watu wenye ulemavu ambayo yametolewa kwa Wataalamu wa Maendeleo ya Jamii kwa lengo la kuwajengea uwezo ili wakatoe elimu kwa wanufaika wa mikopo kwenye Kata zao kwani zaidi ya Fedha kiasi cha Shilingi Milioni 800 za Kitanzania zimetolewa na Halmashauri ya Iringa kwa mwaka wa fedha 2024/25 kwa ajili ya mikopo ya vikundi vya wanawake, vijana na watu wenye ulemavu.

"Lengo la Serikali ni kuendelea kutoa tija na ufanisi katika zoezi zima la kutoa mikopo ya wanawake, vijana na makundi maalumu, nataraji mafunzo haya yatatoa muongozo mpya kwenu juu ya usimamizi wa utoaji wa mikopo kwa wataalamu wetu pindi tutakapoanza kutoa fedha upya ili  changamoto zile za nyuma zisijitokeze tena, Nawaomba mkafanye kazi ya utoaji wa mikopo kwa uadilifu mkubwa sitegemei kusikia habari za vikundi na mikopo hewa. Watakaojihusisha na hili sitawavumilia, watachukuliwa hatua." Amesema Msigala.

Afisa Maendeleo Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Iringa Ndg. Saida Mgeni amesema kuwa mafunzo hayo yamelenga kuwajengea uwezo Maafisa Maendeleo ya Jamii kama wasimamizi wa mikopo hiyo kwenye Kata ili kupata maelekezo kutoka Serikalini kuhusiana na Muongozo, Kanuni pamoja na Sheria za Utoaji wa mikopo na hatimaye kutatua changamoto za mikopo ambayo haikurejeshwa kwa wakati, hivyo matarajio ya Serikali ni kuwa mikopo inayoenda kutolewa mwaka huu itafuta changamoto au mapungufu mbalimbali yaliyojitokeza katika urejeshaji wa mikopo.

Mkuu wa Divisheni ya Maendeleo ya Jamii Manispaa ya Iringa, Ndg. Mwatumu Dossi amesema kuwa mafunzo hayo yatasaidia kuboresha utoaji na ufuatiliaji wa mikopo hiyo kwani awali vikundi vimekuwa vikifanya udanganyifu, vingine vimekuwa vikisambaratika na kushindwa kurejesha mikopo ambayo walichukua, hivyo sheria na kanuni za sasa zitawabana.

Aidha Mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa ya Iringa Ndg. Kastori Msigala amewakumbusha maafisa hao kushiriki  katika Zoezi la Uandikishaji litakaloanza Tarehe 11 mpaka 20 Novemba, 2024 na hatimaye kujitokeza kwa wingi kwenye Uchaguzi wa Serikali za Mitaa unaohusisha Wajumbe wa Mtaa na Mwenyekiti wa Mtaa ambao utafanyika Siku ya Tarehe 27 Novemba, 2024.

Tayari umma umeshataarifiwa  kuhusiana na taratibu za maombi na sifa za wanufaika wa mikopo hiyo mara tu mafunzo hayo yatakapokamilika taratibu nyingine zitafuata.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUONGEZWA MUDA WA KUCHUKUA FOMU YA UJENZI WA JENGO LA BIASHARA TEMBO BAR February 15, 2024
  • MATOKEO YA KIDATO CHA SITA, 2023/2024 July 13, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI July 17, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI July 23, 2024
  • Soma zote

Habari za Hivi punde

  • PPP CENTRE YATOA MAFUNZO KWA WATAALAMU IRINGA MC

    April 04, 2025
  • ALUTE: "HAKIKISHENI MIRADI INAKAMILIKA KWA WAKATI NA KWA UBORA"

    December 21, 2024
  • UCHAGUZI HURU NA WA HAKI UNAHITAJI USHIRIKISHAJI - RC SERUKAMBA

    October 10, 2024
  • MSIGALA AWAONYA MAAFISA MAENDELEO KUJIHUSISHA NA MIKOPO HEWA

    October 05, 2024
  • Soma zote

Video

MEYA WA MANISPAA KUZIPIGANIA TIMU ZA MKOA KUPANDA DARAJA
More Videos

Viunganisho vya Haraka

  • National Examination Council of Tanzania
  • Watumishi Portal
  • MATOKEO YA KIDATO CHA SITA,2023/2024
  • Sheria ndogo za Manispaa
  • Vivutio vya Utalii na Taarifda zake
  • Taarifa kwa vyombo vya Habari

Tovuti Zinazofanana

  • Goverment Website
  • TAMISEMI
  • Iringa Region Website
  • IMtv Fahari ya Iringa

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

https://bachelorthesiswritingservice.com

Location Map

Wasiliana nasi

    Iringa Municipal Council

    Sanduku la Posta: 162

    Telephone: +255-2702647

    Mobile: 255-2702647

    Email: md@iringamc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya usiri
    • Ukanusho
    • MMM
    • Ramani ya eneo
    • Huduma zetu

hakimiliki@2017Iringa Manispaa haki zote zimehifadhiwa