• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
HALMASHAURI YA MANISPAA YA IRINGA
HALMASHAURI YA MANISPAA YA IRINGA

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA OFISI YA RAIS TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA HALMASHAURI YA MANISPAA YA IRINGA

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Mipango Miji
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Afya
      • Maji
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Environment and Cleaning
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Kazi
    • Vitengo
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji nyuki
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Ufugaji
    • Kilimo
  • Huduma zetu
    • Huduma ya elimu
    • Huduma ya Afya
    • Huduma ya Maji
    • Huduma ya kilimo
    • Huduma ya Uvuvi
    • Huduma ya Ufugaji
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu
    • Ratiba ya Vikao
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati wa Halmashauri
    • Ripoti
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Maktaba ya picha
    • Video za shughuli za ofisi au Kitaifa
    • Hotuba

CHONGOLO ATAFUNA MFUPA MGUMU WA MACHINJIO YA NGELEWALA

Posted on: June 1st, 2023

AAHIDI KUTOA SH BILIONI 1.9 KWA AJILI YA VIFAA VYA KISASA

Katibu Mkuu wa  CCM Taifa ndugu.Daniel Chongolo ameahidi fedha kiasi cha sh.bilioni 1.9 kwa ajili ya ukamilishaji wa ujenzi wa Machinjio ya Ngelewala pamoja na ununuzi wa vifaa vya kisasa  vitakavyotumika katika Machinjio hiyo iliyopo Kata ya Mwangata  Manispaa  ya Iringa.

Chongolo ameyasema hayo  Juni 1 2023 alipokuwa  akihitimisha ziara yake  ya siku 7 Mkoani Iringa ambapo   katika Halmashauri ya Manispaa ya Iringa ametembelea mradi  wa mchepuo wa Barabara ya Tumaini- Igumbilo na upanuzi  wa uwanja wa ndege  Iringa ( Nduli)


'Nitawaita Dodoma Mkuu wa Mkoa, Mstahiki Meya, Mkurugenzi na.baadhi ya wataalam na viongozi wa chama na Serikali

Ili tuzungumze namna gani tunaweza kuinusuru machinjio hii kwa kupata  fedha kiasi hicho kwa ajili ya ukamilishaji wa Machinjio hii ili iwe ya kisasa na ilete tija kwa Halmashauri na wananchi wa Manispaa na maeneo mengine alisema Chongolo."

Naye Mkuu  wa Mkoa wa Iringa Mhe.Halima Dendego amesema walikaa na Halmashauri nakufanya tathimini ya mradi huo wa Machinjio na kupata gharama zinazohitajika kukamilisha ujenzi pamoja na vifaa vya kisasa  vya kuchinjia ambapo jumla ya sh.bilioni 1.9  zinahitajika kukamilisha mradi huo na  zitatimiza ndoto zetu za kuwa kiwanda cha nyama na Machinjio ya kisasa Manispaa na Mkoani Iringa kwa ujumla.

Dendego amesema miradi inayokaa muda mrefu huwa na gharama kubwa kuikamilisha lakini lengo ni zuri na kwa kuwa Baba leo umekuja najua utasema kitu alisema Dendego.

Awali akisoma tariifa ya utekelezaji wa mradi huo Afisa Mifugo na Uvuvi wa Manispaa ya Iringa Dr.Stephen Ngwale amesema  Mradi wa Machinjio ya Ngelewala ulianza rasmi kutoa huduma Julai 2022 kwa kutoa huduma ya uchinjaji Ng"ombe,Mbuzi na kondoo na inafanya kazi kwa mfumo wa kawaida.

Dr.Ngwale amesema mradi huo mpaka sasa umefikia wastani wa asilimia 95 na kuwa umegharimu zaidi ya shilingi bilioni 2  na kuwa mradi huo kwa sasa unachinja Ng'ombe 30 hadi 40 ,Mbuzi 15 hadi 25, Kondoo 10 hadi 15. Kwa siku huku akibainisha mafanikio ya mradi kuwa ni utoaji wa ajira 172 kwa wakazi wa Manispaa na kuongezeka kwa mapato ya ndani ya Halmashauri kwani katika kipindi cha Julai hadi Aprili 2023 Machinjio hiyo imeiingizia Halmashauri zaidi ya shilingi milioni 60 ambazo zimekusanywa kama ushuru wa nyama.

Katika ziara hiyo Mhe.Jeca Msambatavangu Mbunge wa Jimbo la Iringa Mjini amemkaribisha Katibu Mkuu Ccm Taifa na kumuomba kuangalia suala la miundombinu ya Barabara ya kutoka Machinjio hadi kitasengwa kutokea Kalenga iweze kuboreshwa ili kupunguza adha kwa wakazi wa maeneo hayo hasa wanafunzi wanaosoma Shule ya Sekondari Isakalilo.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUONGEZWA MUDA WA KUCHUKUA FOMU YA UJENZI WA JENGO LA BIASHARA TEMBO BAR February 15, 2024
  • MATOKEO YA KIDATO CHA SITA, 2023/2024 July 13, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI July 17, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI July 23, 2024
  • Soma zote

Habari za Hivi punde

  • PPP CENTRE YATOA MAFUNZO KWA WATAALAMU IRINGA MC

    April 04, 2025
  • ALUTE: "HAKIKISHENI MIRADI INAKAMILIKA KWA WAKATI NA KWA UBORA"

    December 21, 2024
  • UCHAGUZI HURU NA WA HAKI UNAHITAJI USHIRIKISHAJI - RC SERUKAMBA

    October 10, 2024
  • MSIGALA AWAONYA MAAFISA MAENDELEO KUJIHUSISHA NA MIKOPO HEWA

    October 05, 2024
  • Soma zote

Video

MEYA WA MANISPAA KUZIPIGANIA TIMU ZA MKOA KUPANDA DARAJA
More Videos

Viunganisho vya Haraka

  • National Examination Council of Tanzania
  • Watumishi Portal
  • MATOKEO YA KIDATO CHA SITA,2023/2024
  • Sheria ndogo za Manispaa
  • Vivutio vya Utalii na Taarifda zake
  • Taarifa kwa vyombo vya Habari

Tovuti Zinazofanana

  • Goverment Website
  • TAMISEMI
  • Iringa Region Website
  • IMtv Fahari ya Iringa

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

https://bachelorthesiswritingservice.com

Location Map

Wasiliana nasi

    Iringa Municipal Council

    Sanduku la Posta: 162

    Telephone: +255-2702647

    Mobile: 255-2702647

    Email: md@iringamc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya usiri
    • Ukanusho
    • MMM
    • Ramani ya eneo
    • Huduma zetu

hakimiliki@2017Iringa Manispaa haki zote zimehifadhiwa