• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
HALMASHAURI YA MANISPAA YA IRINGA
HALMASHAURI YA MANISPAA YA IRINGA

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA OFISI YA RAIS TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA HALMASHAURI YA MANISPAA YA IRINGA

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Mipango Miji
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Afya
      • Maji
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Environment and Cleaning
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Kazi
    • Vitengo
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji nyuki
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Ufugaji
    • Kilimo
  • Huduma zetu
    • Huduma ya elimu
    • Huduma ya Afya
    • Huduma ya Maji
    • Huduma ya kilimo
    • Huduma ya Uvuvi
    • Huduma ya Ufugaji
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu
    • Ratiba ya Vikao
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati wa Halmashauri
    • Ripoti
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Maktaba ya picha
    • Video za shughuli za ofisi au Kitaifa
    • Hotuba

DC IRINGA AONGOZA VIONGOZI, WATAALAMU WA HALMASHAURI YA MANISPAA YA IRINGA KWENDA KUJIFUNZA MOROGORO JINSI YA KUWAPANGA MACHINGA

Posted on: October 12th, 2021

MKUU wa wilaya ya Iringa Mohamed Moyo amewaongoza watalaamu na viongozi wa Halmashauri ya Manispaa ya Iringa kwenda mjini Morogoro kujifunza namna nzuri ya kuwapanga wafanyabiashara ndogo ndogo ( Machinga) katika maeneo yao .

Ziara hiyo iliyofanyika  hivi karibuni  ni sehemu ya maandalizi ya Utekelezaji wa agizo la Rais Samia Suluhu Hassan juu ya Halmashauri zote kuwapanga machinga kwenye maeneo sahihi .

Ziara hiyo imeongozwa na mkuu wa Wilaya ya Iringa Mhe.Mohamed Moyo,akiwa ameambatana na   Mstahiki Meya na Naibu Meya wa Halmashauri ya  Manispaa ya Iringa, Mkurugenzi,Madiwani, Mwenyekiti wa CCM Wilaya  na wataalamu kutoka Idara mbalimbali.

Akizungumzia lengo la  ziara hiyo Moyo alisema  ni kupata mafunzo ya namna wenzao walivyofanikiwa  kuwaondoa machinga kwenye barabara,mitaro na kuwapatia sehemu rasmi ya kufanyia biashara zao.

Moyo alisema kwenye ziara hiyo wamepata somo kubwa,wakirudi Iringa watakaa na kutafakari, na kuyatendea kazi waliyojifunza kwa kuwashirikisha na kuwapatia  maeneo ya kufanya biashara machinga wa wilaya yao na  kuhakikisha maagizo ya Mhe Rais wanayatekekeza kwa usalama na utulivu bila ya fujo yoyote.

"Kweli ni niupongeze uongozi mzima wa Morogoro,wameweka mawazo yao pamoja mpaka kufanikiwa kwa machinga kuwa kwenye maeneo mazuri,na jinsi gani wataalamu wanavyo shirikiana na machinga,zaidi Mambo yamekuwa shwari hapa Wilaya ya Morogoro,"alisema Moyo.

Mstahiki Meya wa Halmashauri ya Manispaa ya Iringa mhe: Ibrahim Ngwada, alisema wamepata fursa ya kutembelea vyanzo vingine vya mapato vya Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro ikiwemo ukumbi wa community center ambao kwa sasa umeboreshwa sana.

"Sisi pia tunalo eneo la Maendeleo la community center,ambalo nia yetu ni  kuliboresha,kweli wametufundisha na kuweza kuona namna community center ipo na inavyowasaidia kuingiza mapato ya Halmashauri,"alisema Mhe. Ngwada.

Alisema  wamejifunza jambo kubwa baada ya kutembelea stendi ndogo ya Morogoro kwani wamehamishia baadhi ya vitengo katika eneo hilo,hivyo wamepata mawazo na wataenda kutafanyia kazi katika Halmashauri yao.

"Kikubwa niseme tumekuja Morogoro  na ziara yetu imekuwa na mafanikio na tumejifunza  zaidi,"amesema.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Iringa Manispaa  Said Rubeya alisema wamejifunza  jinsi gani ya kushughulikia  wafanyabiashara wadogo ambao wengi ni vijana wao bila ya kuwaumiza.

Kaimu mkurugenzi wa Manispaa ya Iringa Omary Mkangama alisema watakwenda kutekeleza agizo la mhe Rais  Samia   kwanza kwa kupeleka mawazo katika vikao vya kisheria  na kufuata taratibu zote ikiwemo kuwashirikisha wafanyahiashara ndogo ndogo azma ya  kutekeleza agizo la  Rais

Naye Michael Walusi kaimu mkurugenzi wa Manispaa ya Morogoro,alisema ziara ya viongozi hao kutoka Wilaya ya Iringa ni muendelezo wa Manispaa ya Morogoro kupokea wageni ambao wanakuja kwa ajili ya kujifunza  namna walivyofanikiwa kuwaondoa  wajasiriamali wadogo wadogo na Machinga ambao waliokuwa wametapakaa maeneo mbalimbali na kufanya biashara zao bila utaratibu.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUONGEZWA MUDA WA KUCHUKUA FOMU YA UJENZI WA JENGO LA BIASHARA TEMBO BAR February 15, 2024
  • MATOKEO YA KIDATO CHA SITA, 2023/2024 July 13, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI July 17, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI July 23, 2024
  • Soma zote

Habari za Hivi punde

  • PPP CENTRE YATOA MAFUNZO KWA WATAALAMU IRINGA MC

    April 04, 2025
  • ALUTE: "HAKIKISHENI MIRADI INAKAMILIKA KWA WAKATI NA KWA UBORA"

    December 21, 2024
  • UCHAGUZI HURU NA WA HAKI UNAHITAJI USHIRIKISHAJI - RC SERUKAMBA

    October 10, 2024
  • MSIGALA AWAONYA MAAFISA MAENDELEO KUJIHUSISHA NA MIKOPO HEWA

    October 05, 2024
  • Soma zote

Video

MEYA WA MANISPAA KUZIPIGANIA TIMU ZA MKOA KUPANDA DARAJA
More Videos

Viunganisho vya Haraka

  • National Examination Council of Tanzania
  • Watumishi Portal
  • MATOKEO YA KIDATO CHA SITA,2023/2024
  • Sheria ndogo za Manispaa
  • Vivutio vya Utalii na Taarifda zake
  • Taarifa kwa vyombo vya Habari

Tovuti Zinazofanana

  • Goverment Website
  • TAMISEMI
  • Iringa Region Website
  • IMtv Fahari ya Iringa

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

https://bachelorthesiswritingservice.com

Location Map

Wasiliana nasi

    Iringa Municipal Council

    Sanduku la Posta: 162

    Telephone: +255-2702647

    Mobile: 255-2702647

    Email: md@iringamc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya usiri
    • Ukanusho
    • MMM
    • Ramani ya eneo
    • Huduma zetu

hakimiliki@2017Iringa Manispaa haki zote zimehifadhiwa