• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
HALMASHAURI YA MANISPAA YA IRINGA
HALMASHAURI YA MANISPAA YA IRINGA

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA OFISI YA RAIS TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA HALMASHAURI YA MANISPAA YA IRINGA

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Mipango Miji
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Afya
      • Maji
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Environment and Cleaning
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Kazi
    • Vitengo
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji nyuki
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Ufugaji
    • Kilimo
  • Huduma zetu
    • Huduma ya elimu
    • Huduma ya Afya
    • Huduma ya Maji
    • Huduma ya kilimo
    • Huduma ya Uvuvi
    • Huduma ya Ufugaji
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu
    • Ratiba ya Vikao
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati wa Halmashauri
    • Ripoti
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Maktaba ya picha
    • Video za shughuli za ofisi au Kitaifa
    • Hotuba

DC IRINGA ATAKA WANANCHI KUCHUKUA TAHADHARI WIMBI LA NNE LA CORONA

Posted on: December 7th, 2021

Na Mwandishi Wetu, Iringa

MKUU wa Wilaya ya Iringa, Mohamed Moyo, amewataka wananchi kuendelea kuchukua tahadhari zinazotolewa na wataalam wa afya kufuatia kuibuka kwa wimbi la nne la ugonjwa wa Corona.

Alisema hayo leo (Disemba 7, 2021) wakati akizungumza na wananchi kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika kata za Mshindo na Miyombo-Kitanzini ambao pia uliohudhuriwa na Mstahiki Meya wa Manispaa ya Iringa, Mhe.Ibrahim Ngwada na mhe Epautwa Maadhi ukiwa na lengo la kusikiliza kero za wananchi na kuzipatia ufumbuzi.

Moyo alisema wakati wakiendelea kuchukua tahadhari la wimbi hilo ambalo lilianza kujitokea mwishoni mwa Oktoba mwaka huu, wananchi waendelee pia kujitokeza kupata chanjo ambazo zinatolewa bure kwenye vituo vya afya wilayani humo.

Aidha, Mkuu wa Wilaya amewapongeza waheshimiwa madiwani kwa jinsi wanavyoendelea kusimamia miradi ya ujenzi wa shule za sekondari na vituo vya afya  inayojengwa chini ya fedha za UVIKO-19 zilizotolewa na Serikali kuu.

 Kuhusu sensa ya watu na makazi inayotarajia kufanyika mwakani 2022, Mkuu wa Wilaya amewataka wananchi kuwapa ushirikiano makarani wa Serikali ili kupata takwimu na ifikapo muda huo watu wote wanapaswa kuwa katika makazi yao husika.

Kwa upande wake Mstahiki Meya Manispaa ya Iringa, Mhe. Ngwada, alimweleza Mkuu wa Wilaya kuwa  Manispaa hiyo inatekeleza miradi ya UVIKO-19 kwa kujenga madarsa 33 na kituo cha afya cha kisasa cha Mkimbizi katika kata ya Mkimbizi ujenzi wa barabara kwa kiwango cha lami katika kata ya Mtwivila.

Mhe.Ngwada alisema Halmashauri ya Manispaa ya Iringa,  pia ina mpango wa   kuboresha ujenzi wa jengo la Community Centre.

Aliongeza kuwa halmashauri pia itahakikisha miradi yote inayojengwa kwa fedha za ndani kama vile ujenzi wa soko la Mlandege na stendi ya Igumbilo  inakamilika kwa wakati.

"Mhe Mkuu Wilaya lengo letu tunataka kuhakikisha kuwa halmashauri yetu ya Manispaa ya Iringa inakuwa ya mfano," alisema Mhe.Ngwada.

Nao wananchi waliwasilisha kero zao kwa viongozi hao ambapo Agustino Sambaji alisema kumekuwa kero ya maji kwa wasomaji wa mita kuongeza idadi ya namba za mita na kuleta changamoto kwani gharama zinazokuja ni kubwa mno ukilinganisha na matumizi ya maji wanayotumia wananchi.

Sambaji pia alizungumzia suala la kupanda kwa bei pembejeo kama mbolea hali ambayo imesababisha kilimo msimu huu kuwa kigumu.

Kwa upande wake Shabani Borakupata mjumbe wa Kitanzini amesema miundo mbinu bado ni tatizo kwani barabara zimekuwa ni mbovu na kuwa kero kwa wananchi na kuiomba Serikali kuangalia uwezekano wa kuzijenga kwa kiwango cha lami.

Akijibu kero zilizotolewa na wananchi hao, Mkuu wa Wilaya alisema kero zote Serikali imezichukuwa na kuwaahidi kuwa itazifanyia kazi.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUONGEZWA MUDA WA KUCHUKUA FOMU YA UJENZI WA JENGO LA BIASHARA TEMBO BAR February 15, 2024
  • MATOKEO YA KIDATO CHA SITA, 2023/2024 July 13, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI July 17, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI July 23, 2024
  • Soma zote

Habari za Hivi punde

  • PPP CENTRE YATOA MAFUNZO KWA WATAALAMU IRINGA MC

    April 04, 2025
  • ALUTE: "HAKIKISHENI MIRADI INAKAMILIKA KWA WAKATI NA KWA UBORA"

    December 21, 2024
  • UCHAGUZI HURU NA WA HAKI UNAHITAJI USHIRIKISHAJI - RC SERUKAMBA

    October 10, 2024
  • MSIGALA AWAONYA MAAFISA MAENDELEO KUJIHUSISHA NA MIKOPO HEWA

    October 05, 2024
  • Soma zote

Video

MEYA WA MANISPAA KUZIPIGANIA TIMU ZA MKOA KUPANDA DARAJA
More Videos

Viunganisho vya Haraka

  • National Examination Council of Tanzania
  • Watumishi Portal
  • MATOKEO YA KIDATO CHA SITA,2023/2024
  • Sheria ndogo za Manispaa
  • Vivutio vya Utalii na Taarifda zake
  • Taarifa kwa vyombo vya Habari

Tovuti Zinazofanana

  • Goverment Website
  • TAMISEMI
  • Iringa Region Website
  • IMtv Fahari ya Iringa

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

https://bachelorthesiswritingservice.com

Location Map

Wasiliana nasi

    Iringa Municipal Council

    Sanduku la Posta: 162

    Telephone: +255-2702647

    Mobile: 255-2702647

    Email: md@iringamc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya usiri
    • Ukanusho
    • MMM
    • Ramani ya eneo
    • Huduma zetu

hakimiliki@2017Iringa Manispaa haki zote zimehifadhiwa