• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
HALMASHAURI YA MANISPAA YA IRINGA
HALMASHAURI YA MANISPAA YA IRINGA

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA OFISI YA RAIS TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA HALMASHAURI YA MANISPAA YA IRINGA

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Mipango Miji
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Afya
      • Maji
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Environment and Cleaning
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Kazi
    • Vitengo
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji nyuki
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Ufugaji
    • Kilimo
  • Huduma zetu
    • Huduma ya elimu
    • Huduma ya Afya
    • Huduma ya Maji
    • Huduma ya kilimo
    • Huduma ya Uvuvi
    • Huduma ya Ufugaji
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu
    • Ratiba ya Vikao
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati wa Halmashauri
    • Ripoti
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Maktaba ya picha
    • Video za shughuli za ofisi au Kitaifa
    • Hotuba

HALMASHAURI YA MANISPAA YA IRINGA YAPONGEZWA KWA USIMAMIZI WA USAFI

Posted on: March 30th, 2024

Ikiwa  ni  muendelezo wa Kampeni ya usafi ndani ya Halmashauri ya Manispaa ya Iringa Mkuu wa Wilaya ya Iringa Komred Kheri James amewapongeza Wananchi na Viongozi wa Manispaa hiyo kwa usimamizi bora wa usafi wa mji.

Komred Kheri James ameyasema hayo leo Machi 30, 2024 katika Kampeni ya usafi wa mwisho wa mwezi iliyofanyika katika Kata ya Kihesa Manispaa ya Iringa.

Akizungumza katika Kampeni hiyo Komred Kheri ameeleza kuwa Manispaa na viunga vyake imekuwa na mazingira safi kutokana na mpango mzuri wa usafi unaoshirikisha wananchi kikamilifu kwa kushiriki na kuchangia gharama za usafi wa maeneo yao ya huduma na makazi.

“Niwapongeze Mkurugenzi na wataalamu kwa namna ambavyo mipango ya usafi ya mji wetu inatekelezwa vizuri hivyo niwaahidi nikiwa kama Mkuu wa Wilaya nitaendeleza yale yote mazuri mliyoanza na hata mkiniamsha saa 8 usiku kwa kazi hii tutaifanya ili kuhakikisha Manispaa yetu ya Iringa inakuwa safi, hasa tukianza kwa kutokufanya biashara katika maeneo ambayo hayajapangwa na serikali” Amesema DC Kheri

Kupitia Kampeni hiyo Komred Kheri amewasihi wananchi kuendelea kutekeleza Kampeni hii ya usafi katika maeneo yao ili kudhibiti mlipuko wa maradhi, kuweka vizuri mandhari ya mji ili kuepuka usumbufu unaoweza kutokana na takataka kuzagaa.

“Kampeni hii ya usafi ina dhima maalum ya kuhakikisha mji wetu unakuwa safi, kupambana na magonjwa ya mlipuko, kuweka vizuri mazingira yetu ya biashara na hudumu na mwisho usafi ni kwaajili yetu sisi wenyewe, niwaombe wananchi leo tumeshiriki hapa Kihesa lakini hili ni tangazo na hamasa kwa kila mmoja kufanya usafi katika eneo lake” Amesema DC Kheri

Pamoja na kuwahimiza wananchi kufanya usafi na kulipia gharama za usafi, Komred amewataka Maafisa Tarafa, Watendaji wa Kata na Mitaa kuongeza kasi ya usimamizi ili kuongeza uwajibikaji wa kila mdau katika kuhakikisha maeneo yanakuwa safi na salama.

Mstahiki Meya wa Halmashauri ya Manispaa ya Iringa Mhe. Ibrahim Ngwada ametumia fursa hiyo kumkaribisha Mkuu wa Wilaya ya Iringa na kuwaomba wananchi wa Iringa kuendelea kudumisha suala la usafi katika meneo yetu ya Halmashauri ya Manispaa ya Iringa

“Sisi kama Halmahsuri tumekubali na tunaingia gharama kubwa kila siku tunatumia mafuta zaidi ya Lita 350 mpaka 400 kwajili ya usafi, tunao vibarua zaidi ya 50 kwaajili  ya kufanya usafi wanaozunguka ndani ya Manispaa na kuwalipa mishahara na kununua vifaa, nikuombe Mkuu wa Wilaya uendelee kuhimiza tozo za usafi kwa wananchi Majumbani, Nyumba za wageni (Guest Houses), Mashuleni na Taasisi zetu ili mji wetu uendelee kuwa msafi zaidi kama ambavyo huwa tunashika nafasi ya 1 au 2 kwa Halmashauri za Manispaa” Amesema Mhe. Ngwada

Kampeni hiyo ya usafi kwa Manispaa ya Iringa yenye kaulimbiu ya “Usafi wa Mji Wetu ni Wajibu Wetu” imehudhuriwa pia na Viongozi, Watendaji na Watumishi wa Kada zote.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUONGEZWA MUDA WA KUCHUKUA FOMU YA UJENZI WA JENGO LA BIASHARA TEMBO BAR February 15, 2024
  • MATOKEO YA KIDATO CHA SITA, 2023/2024 July 13, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI July 17, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI July 23, 2024
  • Soma zote

Habari za Hivi punde

  • PPP CENTRE YATOA MAFUNZO KWA WATAALAMU IRINGA MC

    April 04, 2025
  • ALUTE: "HAKIKISHENI MIRADI INAKAMILIKA KWA WAKATI NA KWA UBORA"

    December 21, 2024
  • UCHAGUZI HURU NA WA HAKI UNAHITAJI USHIRIKISHAJI - RC SERUKAMBA

    October 10, 2024
  • MSIGALA AWAONYA MAAFISA MAENDELEO KUJIHUSISHA NA MIKOPO HEWA

    October 05, 2024
  • Soma zote

Video

MEYA WA MANISPAA KUZIPIGANIA TIMU ZA MKOA KUPANDA DARAJA
More Videos

Viunganisho vya Haraka

  • National Examination Council of Tanzania
  • Watumishi Portal
  • MATOKEO YA KIDATO CHA SITA,2023/2024
  • Sheria ndogo za Manispaa
  • Vivutio vya Utalii na Taarifda zake
  • Taarifa kwa vyombo vya Habari

Tovuti Zinazofanana

  • Goverment Website
  • TAMISEMI
  • Iringa Region Website
  • IMtv Fahari ya Iringa

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

https://bachelorthesiswritingservice.com

Location Map

Wasiliana nasi

    Iringa Municipal Council

    Sanduku la Posta: 162

    Telephone: +255-2702647

    Mobile: 255-2702647

    Email: md@iringamc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya usiri
    • Ukanusho
    • MMM
    • Ramani ya eneo
    • Huduma zetu

hakimiliki@2017Iringa Manispaa haki zote zimehifadhiwa