IMC NA GIPCO KUSHIKANA MKONO MRADI WA MACHINJIO - NGELEWALA
Mstahiki Meya wa Halmashauri ya Manispaa ya Iringa Mhe. Ibrahim Ngwada mapema Februari 02, 2026 katika Ofisi yake, amesaini mkatabata wa mradi wa ukamilishaji wa machinjio ya Ngelewala yenye thamani ya Tshs. Millioni 920.
Akizungumza baada ya zoezi la utiaji saini baina ya Halmashauri ya Manispaa ya Iringa na Kampuni ya GIPCO Construction Ltd, Mstahiki Meya ameipongeza Kampuni ya GIPCO Construction Ltd kwa kushinda tenda hiyo na kuwataka kwenda kutekeleza makubaliano yote yaliyowekwa na kukamilisha kazi hiyo kwa wakati.
Meneja wa Kampuni ya GIPCO Construction Ltd Ndg. Alexanda Muchunguzi amemshukuru Mhe. Rais wa Jamhuri wa Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kutoa fesha za kutekeleza mradi huu.
Hafla hiyo ya Utiaji saini imehudhuriwa na Mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa ya Iringa Ndg. Zaina Mlawa, Afisa Kilimo wa Manispaa, Mwanasheria wa Manispaa, Kaimu Afisa Manunuzi wa Manispaa Bi. Jema Monge na viongozi wa Kampuni ya GIPCO Construction Ltd wakiongozwa na Meneja Ndg. Alexanda Muchunguzi.
Iringa Municipal Council
Sanduku la Posta: 162
Telephone: +255-2702647
Mobile: 255-2702647
Email: md@iringamc.go.tz
hakimiliki@2017Iringa Manispaa haki zote zimehifadhiwa