• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
HALMASHAURI YA MANISPAA YA IRINGA
HALMASHAURI YA MANISPAA YA IRINGA

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA OFISI YA RAIS TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA HALMASHAURI YA MANISPAA YA IRINGA

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Mipango Miji
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Afya
      • Maji
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Environment and Cleaning
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Kazi
    • Vitengo
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji nyuki
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Ufugaji
    • Kilimo
  • Huduma zetu
    • Huduma ya elimu
    • Huduma ya Afya
    • Huduma ya Maji
    • Huduma ya kilimo
    • Huduma ya Uvuvi
    • Huduma ya Ufugaji
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu
    • Ratiba ya Vikao
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati wa Halmashauri
    • Ripoti
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Maktaba ya picha
    • Video za shughuli za ofisi au Kitaifa
    • Hotuba

IRINGA: MWAROBAINI WA MALALAMIKO YA ARDHI KWENYE KATA WAPATIKANA

Posted on: June 8th, 2024

Mstahiki Meya wa Halmashauri ya Manispaa ya Iringa, Mhe. Ibrahim A. Ngwada amezindua rasmi kliniki ya ardhi kwa lengo la kusikiliza na kutatua migogoro mbalimbali ya ardhi kwa wananchi wa Kata ya Nduli iliyopo Manispaa ya Iringa.

Uzinduzi huo, umefanyika katika Ofisi ya Kata hiyo kwa lengo la kusikiliza migogoro  mbalimbali ya wananchi huku akiambatana na Viongozi mbalimbali wa Chama na Serikali wakiwemo Katibu Tawala wa Wilaya ya Iringa, Ndg. Michael Semindu, Katibu wa CCM Wilaya Ndg. Hassan Makoba, Diwani wa Kata ya Nduli Mhe. Bashiri Mtove, Diwani Viti Maalum Mhe. Paskalina Lweve, Wataalamu wa ardhi Mkoa na Manispaa, Wakuu wa Idara na Vitengo, Watendaji wa Kata na Mitaa,  Afisa Tarafa, Wenyeviti wa Serikali za Mitaa na wananchi wa Nduli.

Ngwada amesema kuwa Mkutano huo ni matokeo ya ziara ya Mkuu wa Wilaya ya Iringa, Mhe. Kheri James iliofanyika Mei 31, 2024 kwa ajili ya ukaguzi wa miradi na kusikiliza wananchi ambapo baada ya kufika Kata ya Nduli migogoro mingi ya ardhi iliibuka.

Aidha Ngwada amesema kutokana na hali hiyo ilipelekea Mkuu wa Wilaya kutenga siku rasmi ya kusikiliza na kutatua migogoro inayohusu ardhi katika Kata hiyo.

"Pamoja na kwamba kliniki hii itaendelea katika eneo hili la Nduli, wananchi wafahamu kwamba Ofisi zetu za ardhi zipo wazi, Ofisi ya kamishna, Ofisi ya ardhi Manispaa na Ofisi ya Mkuu wa Wilaya, wakati wowote mnapokuwa na changamoto kuhusu masuala ya ardhi msisubiri kliniki au tusisubiri viongozi kuja huku sisi wenyewe twende ofisi hizo ili kutoa malalamiko au changamoto zilizopo, lakini pia ofisi za viongozi wote zipo wazi". Amesema Ngwada.

Mkuu wa Sekta ya Ardhi Manispaa ya Iringa, Ndg. Abenance Kamamonga amesema kuwa zoezi la kutatua migogoro ya wananchi kwa Kata ya Nduli linafanyika kwa siku 2 ambapo Siku ya kwanza itahusisha mitaa ya Mjimwema, Kilimahewa, Mapanda, Kipululu na Kisowele. Siku ya pili itahusisha Mitaa ya Mtalagala, Msisina na Njiapanda.

Akijibu swali la wananchi juu ya urasimishaji wa maeneo kwenye Kata hiyo, Kamomonga amesema kuwa wananchi ya Mitaa ya Kilimahewa, Mapanda na Mjimwema wameshaandika barua kwenye ofisi ya ardhi na tayari wameshalipia gharama za upimaji, hivyo zoezi hilo linatarajia kufanyika mapema wiki ijayo na kwamba huo ndio utakuwa mwarobaini wa malalamiko mengi ya Ardhi kwenye Kata hiyo.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUONGEZWA MUDA WA KUCHUKUA FOMU YA UJENZI WA JENGO LA BIASHARA TEMBO BAR February 15, 2024
  • MATOKEO YA KIDATO CHA SITA, 2023/2024 July 13, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI July 17, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI July 23, 2024
  • Soma zote

Habari za Hivi punde

  • PPP CENTRE YATOA MAFUNZO KWA WATAALAMU IRINGA MC

    April 04, 2025
  • ALUTE: "HAKIKISHENI MIRADI INAKAMILIKA KWA WAKATI NA KWA UBORA"

    December 21, 2024
  • UCHAGUZI HURU NA WA HAKI UNAHITAJI USHIRIKISHAJI - RC SERUKAMBA

    October 10, 2024
  • MSIGALA AWAONYA MAAFISA MAENDELEO KUJIHUSISHA NA MIKOPO HEWA

    October 05, 2024
  • Soma zote

Video

MEYA WA MANISPAA KUZIPIGANIA TIMU ZA MKOA KUPANDA DARAJA
More Videos

Viunganisho vya Haraka

  • National Examination Council of Tanzania
  • Watumishi Portal
  • MATOKEO YA KIDATO CHA SITA,2023/2024
  • Sheria ndogo za Manispaa
  • Vivutio vya Utalii na Taarifda zake
  • Taarifa kwa vyombo vya Habari

Tovuti Zinazofanana

  • Goverment Website
  • TAMISEMI
  • Iringa Region Website
  • IMtv Fahari ya Iringa

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

https://bachelorthesiswritingservice.com

Location Map

Wasiliana nasi

    Iringa Municipal Council

    Sanduku la Posta: 162

    Telephone: +255-2702647

    Mobile: 255-2702647

    Email: md@iringamc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya usiri
    • Ukanusho
    • MMM
    • Ramani ya eneo
    • Huduma zetu

hakimiliki@2017Iringa Manispaa haki zote zimehifadhiwa