• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
HALMASHAURI YA MANISPAA YA IRINGA
HALMASHAURI YA MANISPAA YA IRINGA

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA OFISI YA RAIS TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA HALMASHAURI YA MANISPAA YA IRINGA

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Mipango Miji
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Afya
      • Maji
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Environment and Cleaning
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Kazi
    • Vitengo
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji nyuki
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Ufugaji
    • Kilimo
  • Huduma zetu
    • Huduma ya elimu
    • Huduma ya Afya
    • Huduma ya Maji
    • Huduma ya kilimo
    • Huduma ya Uvuvi
    • Huduma ya Ufugaji
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu
    • Ratiba ya Vikao
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati wa Halmashauri
    • Ripoti
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Maktaba ya picha
    • Video za shughuli za ofisi au Kitaifa
    • Hotuba

KAMATI YA BUNGE YARIDHISHWA NA MRADI WA SEKONDARI KWAVAVA IRINGA

Posted on: January 12th, 2024

Imeelezwa kuwa Shule mpya ya Sekondari ya Kwavava iliyopo Kata ya Kitwiru ndani ya Halmashauri ya Manispaa ya Iringa imetatua tatizo la wanafunzi waliokuwa wakitembea umbali mrefu wa takribani Kilomita 18  kwa miguu hapo awali kwenda Shule ya Sekondari ya Ipogolo kupata elimu kabla ya kuanzishwa kwa mradi wa shule hiyo.

Hayo yamebainika Januari O9, 2024 katika Ziara ya Kamati ya Kudumu ya Bunge-TAMISEMI ikiongozwa na Mwenyekiti wa Kamati Mhe. Dennis Londo ilipotembelea na kukagua mradi huo kwa lengo la kujionea maendeleo ya ujenzi pamoja na kufahamu changamoto zilizopo ili kuzitafutia utatuzi.

Awali akisoma taarifa mbele ya Kamati hiyo Mkuu wa Shule ya Sekondari ya Kwavava Mwl. Vick Kasanga amesema shule hiyo imekuwa ni suluhu kwa tatizo la muda mrefu kwa wanafunzi wa Kata hiyo kutembea umbali mrefu kufika shuleni jambo ambalo lilikuwa linadhoofisha ufanisi wa wanafunzi.

Aidha Mwenyekiti wa Kamati amepongeza jiitihada zilizofanywa na Mkuu wa Mkoa wa Iringa Mhe. Halima Dendego pamoja na timu nzima ya Menejimenti ya Halmashauri ya Manispaa ya Iringa ikiongozwa na Mkurugenzi Ndg. Kastori Msigala kwa kukamilisha mradi huo kwa wakati huku ubora wa majengo yote ukiendana na thamani ya fedha zilizotolewa na kuacha maagizo ya kufanyika kwa maboresho madogo ya umaliziaji ujenzi ili kufanya muonekano wa majengo kuwa mzuri zaidi.

Mradi huo wa mpango wa kuboresha Elimu ya Sekondari (SEQUIP)

wenye thamani ya fedha za Tanzania shilingi 583,000,000/= ulianza kutekelezwa Agosti 2023  ambao una jumla ya majengo ya Madarasa 8, Ofisi 2 za Walimu, Jengo la Maktaba, Jengo la Tehama, Jengo la Utawala, Maabara 3, Vyoo vya Wasichana na Vyoo vya Wavulana.

Katika ziara hiyo ya siku moja Wajumbe wa Kamati ya Bunge- TAMISEMI walifurahishwa na jitihada za Halmashauri ya Manispaa ya Iringa kuhamasisha wazazi na walezi kuwaleta wanafunzi shuleni kwani wameshuhudia muitikio mkubwa wa wanafunzi kufika shuleni na kuonya baadhi ya shule kudai michango lukuki kwa wazazi jambo ambalo limelikemewa vikali.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUONGEZWA MUDA WA KUCHUKUA FOMU YA UJENZI WA JENGO LA BIASHARA TEMBO BAR February 15, 2024
  • MATOKEO YA KIDATO CHA SITA, 2023/2024 July 13, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI July 17, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI July 23, 2024
  • Soma zote

Habari za Hivi punde

  • PPP CENTRE YATOA MAFUNZO KWA WATAALAMU IRINGA MC

    April 04, 2025
  • ALUTE: "HAKIKISHENI MIRADI INAKAMILIKA KWA WAKATI NA KWA UBORA"

    December 21, 2024
  • UCHAGUZI HURU NA WA HAKI UNAHITAJI USHIRIKISHAJI - RC SERUKAMBA

    October 10, 2024
  • MSIGALA AWAONYA MAAFISA MAENDELEO KUJIHUSISHA NA MIKOPO HEWA

    October 05, 2024
  • Soma zote

Video

MEYA WA MANISPAA KUZIPIGANIA TIMU ZA MKOA KUPANDA DARAJA
More Videos

Viunganisho vya Haraka

  • National Examination Council of Tanzania
  • Watumishi Portal
  • MATOKEO YA KIDATO CHA SITA,2023/2024
  • Sheria ndogo za Manispaa
  • Vivutio vya Utalii na Taarifda zake
  • Taarifa kwa vyombo vya Habari

Tovuti Zinazofanana

  • Goverment Website
  • TAMISEMI
  • Iringa Region Website
  • IMtv Fahari ya Iringa

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

https://bachelorthesiswritingservice.com

Location Map

Wasiliana nasi

    Iringa Municipal Council

    Sanduku la Posta: 162

    Telephone: +255-2702647

    Mobile: 255-2702647

    Email: md@iringamc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya usiri
    • Ukanusho
    • MMM
    • Ramani ya eneo
    • Huduma zetu

hakimiliki@2017Iringa Manispaa haki zote zimehifadhiwa