• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
HALMASHAURI YA MANISPAA YA IRINGA
HALMASHAURI YA MANISPAA YA IRINGA

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA OFISI YA RAIS TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA HALMASHAURI YA MANISPAA YA IRINGA

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Mipango Miji
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Afya
      • Maji
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Environment and Cleaning
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Kazi
    • Vitengo
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji nyuki
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Ufugaji
    • Kilimo
  • Huduma zetu
    • Huduma ya elimu
    • Huduma ya Afya
    • Huduma ya Maji
    • Huduma ya kilimo
    • Huduma ya Uvuvi
    • Huduma ya Ufugaji
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu
    • Ratiba ya Vikao
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati wa Halmashauri
    • Ripoti
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Maktaba ya picha
    • Video za shughuli za ofisi au Kitaifa
    • Hotuba

KAMATI YA FEDHA NA UONGOZI MANISPAA YA IRINGA YAKAGUA UTEKELEZAJI WA BEI ELEKEZI YA SUKARI

Posted on: February 24th, 2024

Kamati ya Fedha na Uongozi ya Halmashauri ya Manispaa ya Iringa ikiongozwa na Diwani wa Kata ya Mkimbizi Mheshimiwa Eliud Mvela imefanya ziara ya kutembelea na kukagua baadhi ya Maduka yaliyopo Kata ya Mkwawa ndani ya Manispaa kwa lengo la kujiridhisha kwa wafanyabiashara kama wanatekeleza agizo la Serikari juu ya bei elekezi ya sukari.

Hatua hiyo imefikiwa mara baada ya baadhi ya wafanyabiashara kuuza bidhaa hiyo kwa bei holela ya Tsh. 4000/= hadi Tsh. 5000/= kwa kilo moja kitendo ambacho kimewafanya wananchi wengi kushindwa kumudu gharama hiyo.

Aidha Mhe. Mvela amesema kuwa katika ziara hiyo Kamati imebaini maduka mengi kutokuuza sukari kutokana na kuadimika kwa bidhaa hiyo na kwa maduka machache waliyokuta sukari ilikuwa inauzwa kwa bei elekezi ya Serikali ambayo ni TSh. 2800 hadi Tsh. 3200/= kwa kilo moja.

Mvela ametoa rai kwa wafanyabiashara kufuata bei elekezi na  watakaokiuka agizo hilo hatua za kisheria zitachukuliwa dhidi yao.

“Nawaomba sana ndugu zangu wafanyabiashara muuze sukari kwa bei elekezi pia wale wanaoificha sukari waache tabia hiyo mara moja” Amesema Mvela

Kamati pia ilifanya ukaguzi wa leseni za biashara, Ushuru wa huduma, Ushuru wa taka ngumu na Kutoa elimu kwa wafanyabiashara kulipa kodi na tozo mbalimbali za Halmashauri kwa wakati.

Mstahiki Meya wa Halmashauri ya Manispaa Mhe. Ibrahim Ngwada amesisitiza Wataalamu na Madiwani kushirikiana kwa pamoja kuhakikisha  mapato ya Halmashauri yanaongezeka.

Mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa ya Iringa Ndg. Kastori Msigala amesema amepokea maelekezo yote yaliyotolewa na Kamati na kuhakikisha anayafanyia kazi kwa maslahi mapana ya Halmashauri na wananchi.

Ziara imehusisha Timu ya Menejimenti ya Halmashauri ya Manispaa kwa kutembelea na kukagua miradi miwili ya Maendeleo ambayo ni Mradi wa Ujenzi wa Jengo la Kitega Uchumi la Community Centre na mradi wa Ujenzi wa Jengo la Utawala Stendi mpya ya Igumbilo.

Jumla ya Kanda 5 zimetembelewa na Kamati ya Fedha na Uongozi wa Halmashauri ya Manispaa ya Iringa ambazo ni Kanda ya Mkwawa, Kanda ya Kihesa, Kanda ya Mlandege, Kanda ya Mkimbizi na Kanda ya Ruaha ambapo utaratibu huu utakuwa unafanywa na Kamati katika vikao vyake vya kila mwezi.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUONGEZWA MUDA WA KUCHUKUA FOMU YA UJENZI WA JENGO LA BIASHARA TEMBO BAR February 15, 2024
  • MATOKEO YA KIDATO CHA SITA, 2023/2024 July 13, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI July 17, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI July 23, 2024
  • Soma zote

Habari za Hivi punde

  • PPP CENTRE YATOA MAFUNZO KWA WATAALAMU IRINGA MC

    April 04, 2025
  • ALUTE: "HAKIKISHENI MIRADI INAKAMILIKA KWA WAKATI NA KWA UBORA"

    December 21, 2024
  • UCHAGUZI HURU NA WA HAKI UNAHITAJI USHIRIKISHAJI - RC SERUKAMBA

    October 10, 2024
  • MSIGALA AWAONYA MAAFISA MAENDELEO KUJIHUSISHA NA MIKOPO HEWA

    October 05, 2024
  • Soma zote

Video

MEYA WA MANISPAA KUZIPIGANIA TIMU ZA MKOA KUPANDA DARAJA
More Videos

Viunganisho vya Haraka

  • National Examination Council of Tanzania
  • Watumishi Portal
  • MATOKEO YA KIDATO CHA SITA,2023/2024
  • Sheria ndogo za Manispaa
  • Vivutio vya Utalii na Taarifda zake
  • Taarifa kwa vyombo vya Habari

Tovuti Zinazofanana

  • Goverment Website
  • TAMISEMI
  • Iringa Region Website
  • IMtv Fahari ya Iringa

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

https://bachelorthesiswritingservice.com

Location Map

Wasiliana nasi

    Iringa Municipal Council

    Sanduku la Posta: 162

    Telephone: +255-2702647

    Mobile: 255-2702647

    Email: md@iringamc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya usiri
    • Ukanusho
    • MMM
    • Ramani ya eneo
    • Huduma zetu

hakimiliki@2017Iringa Manispaa haki zote zimehifadhiwa