Kamati ya lishe Halmashauri ya Manispaa ya Iringa leo imefanya ziara ya kukagua shughuli mbalimbali zinazotekelezwa na wadau ndani ya Halmashauri hiyo
Aidha kamati imetembelea na kukagua mradi wa ufugaji Samaki wa bwawa la kitwiru, kitalu nyumba Mkoga pamoja na klabu ya lishe katika shule ya Sekondari Nduli
Raymond Nyenza ambaye ni mtakwimu wa Halmashauri ya Manispaa ya Iringa ameongoza jopo hilo la wataalamu katika ukaguzi huo na amepongeza jitihada za maendeleo ya miradi hiyo
Mtakwimu huyo, pia ameshauri Kila mwanafunzi kupatiwa eneo ambalo ataweza kulihudumia kwa kupanda mbogamboga badala ya kuacha wachache wahusike katika kufanya kazi hiyo.
" Ila tuwapongeze sana kwa kazi nzuri mnayofanya pale ambapo mnatakiwa kurekebisha basi mfanye hivyo" alisema Nyenza.
Iringa Municipal Council
Sanduku la Posta: 162
Telephone: +255-2702647
Mobile: 255-2702647
Email: md@iringamc.go.tz
hakimiliki@2017Iringa Manispaa haki zote zimehifadhiwa