• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
HALMASHAURI YA MANISPAA YA IRINGA
HALMASHAURI YA MANISPAA YA IRINGA

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA OFISI YA RAIS TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA HALMASHAURI YA MANISPAA YA IRINGA

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Mipango Miji
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Afya
      • Maji
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Environment and Cleaning
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Kazi
    • Vitengo
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji nyuki
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Ufugaji
    • Kilimo
  • Huduma zetu
    • Huduma ya elimu
    • Huduma ya Afya
    • Huduma ya Maji
    • Huduma ya kilimo
    • Huduma ya Uvuvi
    • Huduma ya Ufugaji
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu
    • Ratiba ya Vikao
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati wa Halmashauri
    • Ripoti
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Maktaba ya picha
    • Video za shughuli za ofisi au Kitaifa
    • Hotuba

Wajasiriamali waomba msaada wa Bajaji *wasema itawasaidia kusafirishia bidhaa wanazozalisha

Posted on: October 22nd, 2021

Kamati ya kudhibiti Ukimwi katika Halmashauri ya Manispaa ya Iringa ikiongozwa na Mwenyekiti Kenyatta Likotiko ambaye pia ni Naibu Meya imefanya ziara ya kutembelea kikundi cha ITIKA kilichopo kata ya Mwangata, na zahanati ya Itamba.

Ziara hiyo imefanyika leo tarehe 22/10/2021 kwa lengo la kuona maendeleo na kusikiliza changamoto na kuzitafutia ufumbuzi

Awali akisoma taarifa juu ya uendeshaji wa kikundi hicho kinachojishughulisha na uokaji wa mikate,katibu wa kikundi Bi.Haika Luisa amesema kikundi kina jumla ya wanachama kumi na sita,wanawake kumi na nne na wanaume wawili, ambao waliweza kupatiwa mafunzo juu ya utengenezaji wa mikate.

Alisema pia, kikundi kilipata msaada wa mashine ya kisasa ya kuoka mikate kutoka shirika la lisilo la Kiserikali Allamano yenye thamani ya shilingi milioni Arobaini ( 40,000,000)

Pia  walipata  mkopo kutoka Halmashauri ya Manispaa ya Iringa kiasi cha shilingi milioni tano, na shilingi milioni Moja ikiwa ni ruzuku kwa vikundi vyenye mahitaji maalum kutoka ofisi ya Mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa, kwa lengo la  kufanikisha shughuli za  kikundi.

Haika alisema kikundi kinaweza kutumia  kuanzia kilo 75 za unga wa ngano kwa siku na kuzalisha mikate hadi kufikia mia tatu hamsini kwa siku, ambayo ikiuzwa  hupatikana wastani wa shilingi 247,000. Mikate hii huuzwa kwa wakazi wa maeneo ya jirani na maeneo ya mjini ikiwemo kwenye Taasisi mbalimbali za jirani.

Kikundi kimefanikiwa  kununua trei 111 kwaajili ya kuokea mikate zenye ukubwa tofauti tofauti zenye thamani ya 780,000.

Alisema changamoto walizonazo ni  ukosefu wa usafiri kwaajili ya kusambaza mikate katika maeneo ya mbali kama vile Kata ya Ruaha, Igumbilo na Kitwiru, Upungufu wa trei 89 kwa ajili ya kuoka mikate,  pia upungufu wa mitungi ya gesi.

Kamati iliweza kutembelea pia  zahanati ya Itamba kwa lengo la kufuatilia utoaji wa huduma katika kliniki ya VVU ya tiba na mafunzo  kwa mujibu wa taarifa  iliyosomwa mbele ya kamati hiyo juu ya uendeshaji washughuli za kituo hicho ilionyesha kuwa  kituo kimefanikiwa kutoa huduma ya utoaji dawa za kufubaza virusi vya ukimwi pamoja na Kifua kikuu. ushauri na mafunzo mbalimbali.

Hata hivyo, Zahanati ya Itamba imebainisha  ukosefu wa mshine ya kupimia CD4 pamoja na chumba  cha uangalizi na matibabu kwa watu wanaochukua dawa za kufubaza virusi vya ukimwi kwani kilichopo ni kidogo na hakina  usiri.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUONGEZWA MUDA WA KUCHUKUA FOMU YA UJENZI WA JENGO LA BIASHARA TEMBO BAR February 15, 2024
  • MATOKEO YA KIDATO CHA SITA, 2023/2024 July 13, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI July 17, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI July 23, 2024
  • Soma zote

Habari za Hivi punde

  • PPP CENTRE YATOA MAFUNZO KWA WATAALAMU IRINGA MC

    April 04, 2025
  • ALUTE: "HAKIKISHENI MIRADI INAKAMILIKA KWA WAKATI NA KWA UBORA"

    December 21, 2024
  • UCHAGUZI HURU NA WA HAKI UNAHITAJI USHIRIKISHAJI - RC SERUKAMBA

    October 10, 2024
  • MSIGALA AWAONYA MAAFISA MAENDELEO KUJIHUSISHA NA MIKOPO HEWA

    October 05, 2024
  • Soma zote

Video

MEYA WA MANISPAA KUZIPIGANIA TIMU ZA MKOA KUPANDA DARAJA
More Videos

Viunganisho vya Haraka

  • National Examination Council of Tanzania
  • Watumishi Portal
  • MATOKEO YA KIDATO CHA SITA,2023/2024
  • Sheria ndogo za Manispaa
  • Vivutio vya Utalii na Taarifda zake
  • Taarifa kwa vyombo vya Habari

Tovuti Zinazofanana

  • Goverment Website
  • TAMISEMI
  • Iringa Region Website
  • IMtv Fahari ya Iringa

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

https://bachelorthesiswritingservice.com

Location Map

Wasiliana nasi

    Iringa Municipal Council

    Sanduku la Posta: 162

    Telephone: +255-2702647

    Mobile: 255-2702647

    Email: md@iringamc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya usiri
    • Ukanusho
    • MMM
    • Ramani ya eneo
    • Huduma zetu

hakimiliki@2017Iringa Manispaa haki zote zimehifadhiwa