• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
HALMASHAURI YA MANISPAA YA IRINGA
HALMASHAURI YA MANISPAA YA IRINGA

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA OFISI YA RAIS TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA HALMASHAURI YA MANISPAA YA IRINGA

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Mipango Miji
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Afya
      • Maji
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Environment and Cleaning
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Kazi
    • Vitengo
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji nyuki
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Ufugaji
    • Kilimo
  • Huduma zetu
    • Huduma ya elimu
    • Huduma ya Afya
    • Huduma ya Maji
    • Huduma ya kilimo
    • Huduma ya Uvuvi
    • Huduma ya Ufugaji
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu
    • Ratiba ya Vikao
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati wa Halmashauri
    • Ripoti
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Maktaba ya picha
    • Video za shughuli za ofisi au Kitaifa
    • Hotuba

KOMREDI KHERI AVALIA NJUGA MGOMO WA DALADALA IRINGA.

Posted on: May 15th, 2024

Mkuu wa Wilaya ya Iringa Komredi Kheri James ametaka kutekelezwa kwa maagizo aliyotoa kwa wamiliki na madereva daladala na sio kutoa ahadi ili kutatua changamoto zilizopo na kustawisha huduma ya usafiri ndani ya Halmashauri ya Manispaa ya Iringa.

Komred Kheri amesema hayo wakati akifungua kikao cha kusikiliza kero na changamoto za wamiliki na madereva Daladala kilichofanyika katika ukumbi wa Siasa ni Kilimo.

“Nataka kuona maagizo ninayotoa katika kikao hiki utekelezaji wake unaanza mara moja kwenye kikao hiki sihitaji ahadi bali nahitaji utekelezaji kuanza mara moja.” Amesema Komred Kheri

Hatua hii imefikiwa mara baada ya Madereva na Wamiliki wa Daladala kufanya mgomo wa takribani siku 3 mfulizo bila kutoa huduma za usafiri kuanzia tarehe 6-8/5/2024 na kusababisha adha kwa abiria, kwa madai mbalimbali ikiwemo kuvunjwa kwa makubaliano baina ya Daladala na Umoja wa Madereva Bajaji yaliyosainiwa mbele ya aliyekuwa Mkuu wa Mkoa Mhe. Halima Dendego na Mstahiki Meya Mhe. Ibrahim Ngwada tarehe 13 Julai 2023 katika Uwanja wa Mwembetogwa.

“Mwanasheria na Afisa Biashara mnazo sheria ndogo za Halmashauri ambazo mnapaswa kuzisimamia Mgambo mnao na OCD atakuwa nanyi katika usimamizi wa utekelezaji wa sheria hizo, hivyo jipangeni kufanya kazi hiyo kuanzia tarehe 15.05.2024 kukamata wale wote watakaokiuka taratibu muweze kuwachukulia hatua za kisheria na kila wiki mnatakiwa kunipa taarifa na changamoto mtakazokabiliana nazo wakati wa utekelezaji ili nizishughulikie.” Amesema Komredi Kheri

Mfawidhi LATRA Mkoa wa Iringa Ndg. Joseph Umoti amesema kuwa  wamebaini asilimia 90 ya madereva  bajaji hawana sifa pia baadhi ya madereva huacha masomo na kukimbilia kuendesha bajaji hivyo ameonya kuacha tabia hiyo mara moja kwani mamlaka itahakikisha sheria, kanuni na taratibu zinafuatwa.

Mwenyekiti wa Umoja wa Daladala Ndg. Rashid Mshana amesema kukosekana kwa usimamizi toka kwa mamlaka zinazohusika ndio imepelekea madereva Bajaji kuvunja sheria na kukiuka makubaliano ya njia waliyopangiwa na kupelekea wao kufanya mgomo.

Katibu wa Umoja wa Daladala Manispaa Ndg. Shaibu Maluzuku amesema uwepo wa vituo binafsi vidogo vya mabasi (Terminal) vilivyopo katikati ya Mji vimekuwa ni kiwazo kwao kwani vinasababisha wao kukosa abiria.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUONGEZWA MUDA WA KUCHUKUA FOMU YA UJENZI WA JENGO LA BIASHARA TEMBO BAR February 15, 2024
  • MATOKEO YA KIDATO CHA SITA, 2023/2024 July 13, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI July 17, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI July 23, 2024
  • Soma zote

Habari za Hivi punde

  • PPP CENTRE YATOA MAFUNZO KWA WATAALAMU IRINGA MC

    April 04, 2025
  • ALUTE: "HAKIKISHENI MIRADI INAKAMILIKA KWA WAKATI NA KWA UBORA"

    December 21, 2024
  • UCHAGUZI HURU NA WA HAKI UNAHITAJI USHIRIKISHAJI - RC SERUKAMBA

    October 10, 2024
  • MSIGALA AWAONYA MAAFISA MAENDELEO KUJIHUSISHA NA MIKOPO HEWA

    October 05, 2024
  • Soma zote

Video

MEYA WA MANISPAA KUZIPIGANIA TIMU ZA MKOA KUPANDA DARAJA
More Videos

Viunganisho vya Haraka

  • National Examination Council of Tanzania
  • Watumishi Portal
  • MATOKEO YA KIDATO CHA SITA,2023/2024
  • Sheria ndogo za Manispaa
  • Vivutio vya Utalii na Taarifda zake
  • Taarifa kwa vyombo vya Habari

Tovuti Zinazofanana

  • Goverment Website
  • TAMISEMI
  • Iringa Region Website
  • IMtv Fahari ya Iringa

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

https://bachelorthesiswritingservice.com

Location Map

Wasiliana nasi

    Iringa Municipal Council

    Sanduku la Posta: 162

    Telephone: +255-2702647

    Mobile: 255-2702647

    Email: md@iringamc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya usiri
    • Ukanusho
    • MMM
    • Ramani ya eneo
    • Huduma zetu

hakimiliki@2017Iringa Manispaa haki zote zimehifadhiwa