Mkuu wa Wilaya ya Iringa Mhe. Mohamed Hassan Moyo leo Septemba 4, ameukabidhi Mwenge wa Uhuru kwa Muu wa Wilaya Kilolo mara baada ya Mwenge huo kukimbizwa katika Manispaa ya Iringa jana tarehe 3/9/2022 ambao ulikimbizwa umbali wa kilomita 76
Akikabidhi Mwenge wa uhuru leo tarehe 4/9/2022 katika wilaya ya kilolo kwenye viwanja vya shule ya Msingi Lundamatwe Mhe. Mohamed Moyo amesema katika eneo la Mkesha Iringa Manispaa Mwembetogwa jumls ya wananchi 122 walijitokeza kupima VVU/UKIMWI na hakuna hata mmoja aliyekutwa na maambukizi pia wananchi 35 walijitokeza kupima malaria na hakuna ambaye amekutwa na ugonjwa, waliopata chanjo ya Uviko 19 ni watu 17 ville vile chupa 3 za damu zilichangiwa na wananchi katika eneo hilo la Mkesha.
Hata hivyo Mhe Moyo amewashukuru wakimbiza Mwenge Kitaifa 2022 na amewaahidi kuyatendea kazi yale yote ambayo wameshauri katika kuboresha usimamizi mzuri na ujenzi bora wa miradi ya Maendeleo
Kwa upande wake kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru kwa mwaka 2022, Ndg, Sahili Geraruma ameshukuru na kumpongeza Mkuu wa Wilaya na watalamu wote kwa usimamizi mzuri wa shughuli na miradi ya na kuwataka kuendele kufuata miongozo iliyopo kwa maslahi mapana ya wanachi wa Manispaa ya Iringa.
Aidha katika kukimbiza mbio za Mwenge huo siku ya jana uliopokelewa kutoka Wilaya ya Mufindi, katika Manispaa ya Iringa ulipitia miradi mitano 5 yenye thamani ya Tsh Bilioni 1.5 ambayo ni Ujenzi wa madarasa 2 na Ofisi 1 shule ya Sekondari Tagamenda, Ujenzi wa shule mpya ya Sekondari Isakalilo, Ujenzi wa jengo la upasuaji na wodi katika Hospitali ya Frelimo, Mradi wa barabara ya lami Mtwivila- Ikonongo pamoja na mradi wa kikundi cha vijana wanufaika na mkopo cha Ebeneza
Iringa Municipal Council
Sanduku la Posta: 162
Telephone: +255-2702647
Mobile: 255-2702647
Email: md@iringamc.go.tz
hakimiliki@2017Iringa Manispaa haki zote zimehifadhiwa