• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
HALMASHAURI YA MANISPAA YA IRINGA
HALMASHAURI YA MANISPAA YA IRINGA

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA OFISI YA RAIS TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA HALMASHAURI YA MANISPAA YA IRINGA

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Mipango Miji
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Afya
      • Maji
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Environment and Cleaning
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Kazi
    • Vitengo
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji nyuki
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Ufugaji
    • Kilimo
  • Huduma zetu
    • Huduma ya elimu
    • Huduma ya Afya
    • Huduma ya Maji
    • Huduma ya kilimo
    • Huduma ya Uvuvi
    • Huduma ya Ufugaji
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu
    • Ratiba ya Vikao
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati wa Halmashauri
    • Ripoti
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Maktaba ya picha
    • Video za shughuli za ofisi au Kitaifa
    • Hotuba

MADIWANI WATAKIWA KUSIMAMIA MIRADI

Posted on: November 30th, 2021

Uongozi wa Mkoa wa Iringa umetakiwa kuhakikisha unatekeleza miradi mbalimbali inayotokana na fedha za Uviko 19 zilizotolewa na Serikali kupitia mkopo uliotolewa na shirika la fedha Duniani (IMF)

Wito huo umetolewa na Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Chama Cha Mapinduzi Taifa(MNEC) Mkoa wa Iringa Salim Abri katika  mkutano  wa  Madiwani wote  wa Mkoa wa Iringa uliofanyika ukumbi wa Royal Palm ,ukiwa na lengo la kuwakutanisha madiwani hao na viongozi wa juu wa Serikali.

"Utekelezaji wa miradi hii ni muhimu kuzingatia viwango katika kupunguza changamoto zilizotokana na Uviko 19, janga lililo tikisa dunia ikiwemo Tanzania." Alisema Abri.

Katika hatua nyingine Abri amewakumbusha Madiwani hao kuwa fedha hizo ni za mkopo na sio msaada.

"Fedha hizi ni mkopo na Serikali itatakiwa kurejesha fedha hizi japo kuwa siyo kwa riba."

Sanjari na hayo Akizungumzia mkutano huo kuwa lengo lake kuu ni kuzungumzia agenda ya utekelezaji wa Ilani CCM.

Huku akiwa pongeza Madiwani hao  kwa kuandaa mkutano huo ambao utafanya mabadilishano ya maendeleo kati ya Halmashauri na halmashauri ,kata na kata ili kuendelea kuleta maendeleo nakutekeleza ilani ya chama hicho.

Kwa upande wake Mstahiki Meya wa Manispaa ya Iringa Mhe.  Ibrahim Ngwada,ameishukuru Serikali ya awamu ya sita chini ya Mhe. Samia Suluhu Hassan kwa kupeleka fedha  nyingi katika Halmashauri ya Manispaa ambazo  zimefanya kazi nyingi katika kutekeleza miradi mbalimbali ikiwepo umaliziaji wa machinjio  ya kisasa yaliopo Ngelewala ambayo likuwa  tatizo kubwa katika Halmashauri .

Pia umaliziaji wa wodi ya hospitali ya Frelimo,umaliziaji wa madarasa 33 katika Halmashauri ya Manispaa ya Iringa pamoja na umaliziaji wa maboma ya madarasa katika maeneo ya Halmashauri .

"Katika mapato yetu ya Halmashauri  tumeweza kuhakikisha tunatekeleza miradi mbali mbali mkienda katika jengo letu la stendi ya Igumbilo tunamalizia, pia tunayo madarasa tunamalizia na maeneo mengine mengi na tunatekeleza kupitia makusanyo yetu, kupitia mapato yetu ya ndani pia tumetoa asilimia 10% kwa akina wanawake,vijana na watu wenye ulemavu ,kwakweli tumehakikisha pesa hizo zinakwenda kwa wahusika,"alisema Gwada

Mkutano huo pia umehudhuriwa na Katibu Tawala (RAS) Mkoa wa Iringa Bi. Happiness Seneda ambaye pia amepata nafasi yakutoa takwimu juu ya lishe,vita dhidi ya ukimwi ,mpango mkakati kuhusiana na mazingira ,miradi  ya maendeleo na bajeti pamoja na suala la unyanyasaji wa kijinsia kwa akina mama ,watoto na akina baba.

Hivi karibuni Serikali ya Tanzania imepokea Shilingi trioni 1.3 za kukabiliana na athari za janga la UVIKO-19 kutoka IMF na kugawa kwenye kila Mkoa.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUONGEZWA MUDA WA KUCHUKUA FOMU YA UJENZI WA JENGO LA BIASHARA TEMBO BAR February 15, 2024
  • MATOKEO YA KIDATO CHA SITA, 2023/2024 July 13, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI July 17, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI July 23, 2024
  • Soma zote

Habari za Hivi punde

  • PPP CENTRE YATOA MAFUNZO KWA WATAALAMU IRINGA MC

    April 04, 2025
  • ALUTE: "HAKIKISHENI MIRADI INAKAMILIKA KWA WAKATI NA KWA UBORA"

    December 21, 2024
  • UCHAGUZI HURU NA WA HAKI UNAHITAJI USHIRIKISHAJI - RC SERUKAMBA

    October 10, 2024
  • MSIGALA AWAONYA MAAFISA MAENDELEO KUJIHUSISHA NA MIKOPO HEWA

    October 05, 2024
  • Soma zote

Video

MEYA WA MANISPAA KUZIPIGANIA TIMU ZA MKOA KUPANDA DARAJA
More Videos

Viunganisho vya Haraka

  • National Examination Council of Tanzania
  • Watumishi Portal
  • MATOKEO YA KIDATO CHA SITA,2023/2024
  • Sheria ndogo za Manispaa
  • Vivutio vya Utalii na Taarifda zake
  • Taarifa kwa vyombo vya Habari

Tovuti Zinazofanana

  • Goverment Website
  • TAMISEMI
  • Iringa Region Website
  • IMtv Fahari ya Iringa

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

https://bachelorthesiswritingservice.com

Location Map

Wasiliana nasi

    Iringa Municipal Council

    Sanduku la Posta: 162

    Telephone: +255-2702647

    Mobile: 255-2702647

    Email: md@iringamc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya usiri
    • Ukanusho
    • MMM
    • Ramani ya eneo
    • Huduma zetu

hakimiliki@2017Iringa Manispaa haki zote zimehifadhiwa