• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
HALMASHAURI YA MANISPAA YA IRINGA
HALMASHAURI YA MANISPAA YA IRINGA

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA OFISI YA RAIS TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA HALMASHAURI YA MANISPAA YA IRINGA

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Mipango Miji
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Afya
      • Maji
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Environment and Cleaning
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Kazi
    • Vitengo
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji nyuki
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Ufugaji
    • Kilimo
  • Huduma zetu
    • Huduma ya elimu
    • Huduma ya Afya
    • Huduma ya Maji
    • Huduma ya kilimo
    • Huduma ya Uvuvi
    • Huduma ya Ufugaji
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu
    • Ratiba ya Vikao
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati wa Halmashauri
    • Ripoti
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Maktaba ya picha
    • Video za shughuli za ofisi au Kitaifa
    • Hotuba

MANISPAA YA IRINGA ILIVYOFANIKIWA KWA MWAKA WA FEDHA 2021/2022

Posted on: August 17th, 2022

Mstahiki Meya wa Halmashauri ya Manispaa ya Iringa mhe.Ibrahim Ngwada ameyataja mafanikio na ubora wa miradi mbalimbali  iliyotekelezwa ndani ya Manispaa ya Iringa kwa mwaka wa fedha 2021/2022 huku akizipongeza kamati za kudumu za Halmashauri kwa usimamizi mzuri wa miradi hiyo ya maendeleo.

Hayo ameyasema leo Agasti 17/2022  katika Mkutano wa Baraza la Madiwani wa kuwasiliana na kujadili  taarifa za robo ya nne ya mwaka 2021/2022, lililofanyikab katika ukumbi wa Mikutano wa Manispaa ya Iringa

Akizungumza wakati wa kufungua kikao hicho ameyataja mafanikio hayo kuwa ni pamoja na ukamilishaji ujenzi wa Machinjio kubwa ya Ngelewala yenye uwezo wa kuchinja ng'ombe 100 na mbuzi 200 kwa siku, ukamilishaji wa wodi ya kina baba na kina mama, jengo la upasuaji pamoja na chumba cha kuhifadhia maiti katika Hospital ya Wilaya ya Iringa (Frelimo)

Miradi mingine ni ujenzi wa Shule na Madarasa, zahanati, vituo vya afya, Masoko, Stendi ya mabasi pamoja na usimamizi mzuri wa usafi wa mazingira.

Kwa upande wake Mbunge wa Jimbo la Iringa Mjini Mhe. Jesca Msambatavangu ambaye ni mjumbe katika Baraza hilo  amesema anatamani kwa mwaka mpya wa fedha 2022/2023 vipaumbele viwe katika ujenzi wa shule za msingi katika kukarabati na ujenzi wa madarasa hasa shule zilizopo pembezoni mwa Halmashauri.

"Kutokana na hali ya uchakavu na changamoto shule zetu nyingi za msingi, tunaomba Halmashauri ifanye kipaumbele kwa awamu hii ili kuona watoto wetu wanapata Elimu kwa urahisi ili kutimiza ndoto zao" Mhe Jesca alisema

Hata hvyo Mhe. Mohamed Moyo, Mkuu wa Wilaya ya Iringa amempongeza Mkurugenzi kwa jitihada walizofanya kukusanya mapato hadi kuvuka lengo

Pia Mhe. Moyo amekemea jambo la ukatili wa kijinsia kuendelea kushamiri katika baadhi ya maeneo ya Manispaa ya Iringa na kuwataka Madiwani kuendelea kulikemea suala hilo katika maeneo yao na kuchukua sheria stahiki kwa wale wote watakaoshiriki ama kubainika wamefanya ukatili wa kijinsia.

Naye Kaimu Mkurugenzi wa Manispaa ya Iringa Ndg. Gerald Mwamuhamila amewataka wananchi wote ambao maeneo yao yalichukuliwa na Halamashauri huku wakidai fidia kuwa wawe wavumilivu kwani ameshamuagiza Mkuu wa Idara ya Mipango Miji kushughulikia suala lao la kulipwa fidia zao

Akihitimisha kwa kufunga Baraza hilo Mstahiki Meya Mhe. Ibrahim Ngwada amempongeza mwenyekiti wa kamati ya maadili Mhe. Mahazi Epautwa, Diwani wa Kata ya Kitanzini kwa kufanikiwa kusimamia vizuri kamati yake ya Maadili kwa kipindi cha Robo zote kwa mwaka huu.

Mwisho amewataka Madiwani kuendelea kuzungumzia mazuri yanayoendelea kufanyika ndani ya Halmashauri chini ya Uongozi wa Rais wa Awamu ya sita ya Mhe. Samia Suluhu Hassan.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUONGEZWA MUDA WA KUCHUKUA FOMU YA UJENZI WA JENGO LA BIASHARA TEMBO BAR February 15, 2024
  • MATOKEO YA KIDATO CHA SITA, 2023/2024 July 13, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI July 17, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI July 23, 2024
  • Soma zote

Habari za Hivi punde

  • PPP CENTRE YATOA MAFUNZO KWA WATAALAMU IRINGA MC

    April 04, 2025
  • ALUTE: "HAKIKISHENI MIRADI INAKAMILIKA KWA WAKATI NA KWA UBORA"

    December 21, 2024
  • UCHAGUZI HURU NA WA HAKI UNAHITAJI USHIRIKISHAJI - RC SERUKAMBA

    October 10, 2024
  • MSIGALA AWAONYA MAAFISA MAENDELEO KUJIHUSISHA NA MIKOPO HEWA

    October 05, 2024
  • Soma zote

Video

MEYA WA MANISPAA KUZIPIGANIA TIMU ZA MKOA KUPANDA DARAJA
More Videos

Viunganisho vya Haraka

  • National Examination Council of Tanzania
  • Watumishi Portal
  • MATOKEO YA KIDATO CHA SITA,2023/2024
  • Sheria ndogo za Manispaa
  • Vivutio vya Utalii na Taarifda zake
  • Taarifa kwa vyombo vya Habari

Tovuti Zinazofanana

  • Goverment Website
  • TAMISEMI
  • Iringa Region Website
  • IMtv Fahari ya Iringa

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

https://bachelorthesiswritingservice.com

Location Map

Wasiliana nasi

    Iringa Municipal Council

    Sanduku la Posta: 162

    Telephone: +255-2702647

    Mobile: 255-2702647

    Email: md@iringamc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya usiri
    • Ukanusho
    • MMM
    • Ramani ya eneo
    • Huduma zetu

hakimiliki@2017Iringa Manispaa haki zote zimehifadhiwa