• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
HALMASHAURI YA MANISPAA YA IRINGA
HALMASHAURI YA MANISPAA YA IRINGA

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA OFISI YA RAIS TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA HALMASHAURI YA MANISPAA YA IRINGA

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Mipango Miji
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Afya
      • Maji
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Environment and Cleaning
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Kazi
    • Vitengo
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji nyuki
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Ufugaji
    • Kilimo
  • Huduma zetu
    • Huduma ya elimu
    • Huduma ya Afya
    • Huduma ya Maji
    • Huduma ya kilimo
    • Huduma ya Uvuvi
    • Huduma ya Ufugaji
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu
    • Ratiba ya Vikao
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati wa Halmashauri
    • Ripoti
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Maktaba ya picha
    • Video za shughuli za ofisi au Kitaifa
    • Hotuba

MANISPAA YA IRINGA INATARAJIA KUKUSANYA BILIONI 8 KWA MWAKA WA FEDHA 2024/2025.

Posted on: September 9th, 2024

MANISPAA YA IRINGA INATARAJIA KUKUSANYA BILIONI 8 KWA MWAKA WA FEDHA 2024/2025.

Mstahiki Meya wa Halmashauri ya Manispaa ya Iringa, Mhe. Ibrahim Ngwada amesema kuwa Manispaa ya Iringa inatarajia kukusanya  fedha kiasi cha shilingi Bilioni 8 kwa mwaka wa fedha 2024/25 kutokana na mapato kuongezeka na kufikia shilingi Bilioni 6.7  kwa mwaka wa fedha uliopita.

Hayo ameyasema katika Mkutano wa Mwaka wa Baraza la Madiwani kwa kipindi cha Mwaka wa Fedha 2023/24, ambao  umefanyika katika Ukumbi wa Manispaa ya Iringa Tarehe 09 Septemba, 2024 kwa lengo la kujadili taarifa ya utendaji kazi na uwajibikaji katika Halmashauri ya Manispaa ya Iringa, na kufanya uchaguzi wa Naibu Meya na Uteuzi wa wajumbe wa

kamati za kudumu za Halmashauri

"Moja ya mafanikio makubwa katika Halmashauri ambayo tunajivunia ni kupandisha mapato yetu kutoka shilingi Bilioni 3.5 kwa miaka iliyopita mpaka kufikia shilingi Bilioni 6.3 kwa mwaka wa fedha 2023/24 ambapo makisio ilikuwa ni Bilioni 6.7. Hakika tumepanda kwa kiwango kikubwa. Kutokana na hilo tunaweza kukusanya kiasi cha Bilioni 8 kwa Mwaka wa fedha 2024/25". Amesema Ngwada.

Naye Mkuu wa Wilaya ya Iringa, Komredi Kheri James ameupongeza uongozi wa Halmashauri kwa uwajibikaji uliotukuka katika kuwahudumia wananchi kwa mwaka wa fedha uliopita,pia ametoa msisitizo kwa uongozi huo kuwa mwaka unapokamilika inatakiwa wajipange hasa katika masuala ya ukusanyaji wa mapato, usimamizi wa

miradi, usikilizaji na utatuzi wa kero za wananchi, usafi pamoja na kuboresha maamuzi na kusimamia biashara na huduma bora ndani  ya Manispaa.

"Uwepo wa Halmashauri zetu za wilaya au Manispaa ni dhamira ya kuwasogezea wananchi bunge lao la kujadili mambo yao, yanayostawisha dhamira zao Kupitia Baraza hili tumeshuhudia mipango mikubwa ya maendeleo liyopangwa inatekelezwa, pamoja na maamuzi yaliyopangwa kwa faida ya wananchi na tumeshuhudia maono makubwa yaliyopo kwa ajili ya leo na kesho, nina imani mtahakikisha maamuzi yenu yanagusa maisha ya watu". Amesema Kheri.

Naye Katibu wa CCM wilaya ya Iringa Mjini Ndg, Hassan Makoba ametoa rai kwa Madiwani kuwa mabalozi wazuri kwa wananchi katika Kata zao kwa kuwaeleza

mambo makubwa ambayo yamefanywa na Baraza la Madiwani kiujumla kwa maslahi ya Kata zao,pia ameshauri mambo yote yanayopangwa na Madiwani wayasimamie maana wao ndio wenye dhamana kubwa ya kusimamia Manispaa ya Iringa na kuwa wanapotekeleza hayo wanatekeleza ilani ya Chama Cha Mapinduzi (CCM).

Mkutano huo umehudhuriwa na Kamati ya Siasa ya Wilaya, Mkuu Wa Willaya, Katibu Tawala wilaya, Madiwani, Sekretariati ya Mkoa, wawakilishi wa Taasisi mbalimbali za Serikali kama TARURA, IRUWASA, TAKUKURU, TANESCO,  TANROAD, Wakuu wa Idara na Vitengo wa Manispaa, watendaji wa Kata, watumishi pamoja na wananchi.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUONGEZWA MUDA WA KUCHUKUA FOMU YA UJENZI WA JENGO LA BIASHARA TEMBO BAR February 15, 2024
  • MATOKEO YA KIDATO CHA SITA, 2023/2024 July 13, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI July 17, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI July 23, 2024
  • Soma zote

Habari za Hivi punde

  • PPP CENTRE YATOA MAFUNZO KWA WATAALAMU IRINGA MC

    April 04, 2025
  • ALUTE: "HAKIKISHENI MIRADI INAKAMILIKA KWA WAKATI NA KWA UBORA"

    December 21, 2024
  • UCHAGUZI HURU NA WA HAKI UNAHITAJI USHIRIKISHAJI - RC SERUKAMBA

    October 10, 2024
  • MSIGALA AWAONYA MAAFISA MAENDELEO KUJIHUSISHA NA MIKOPO HEWA

    October 05, 2024
  • Soma zote

Video

MEYA WA MANISPAA KUZIPIGANIA TIMU ZA MKOA KUPANDA DARAJA
More Videos

Viunganisho vya Haraka

  • National Examination Council of Tanzania
  • Watumishi Portal
  • MATOKEO YA KIDATO CHA SITA,2023/2024
  • Sheria ndogo za Manispaa
  • Vivutio vya Utalii na Taarifda zake
  • Taarifa kwa vyombo vya Habari

Tovuti Zinazofanana

  • Goverment Website
  • TAMISEMI
  • Iringa Region Website
  • IMtv Fahari ya Iringa

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

https://bachelorthesiswritingservice.com

Location Map

Wasiliana nasi

    Iringa Municipal Council

    Sanduku la Posta: 162

    Telephone: +255-2702647

    Mobile: 255-2702647

    Email: md@iringamc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya usiri
    • Ukanusho
    • MMM
    • Ramani ya eneo
    • Huduma zetu

hakimiliki@2017Iringa Manispaa haki zote zimehifadhiwa