• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
HALMASHAURI YA MANISPAA YA IRINGA
HALMASHAURI YA MANISPAA YA IRINGA

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA OFISI YA RAIS TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA HALMASHAURI YA MANISPAA YA IRINGA

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Mipango Miji
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Afya
      • Maji
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Environment and Cleaning
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Kazi
    • Vitengo
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji nyuki
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Ufugaji
    • Kilimo
  • Huduma zetu
    • Huduma ya elimu
    • Huduma ya Afya
    • Huduma ya Maji
    • Huduma ya kilimo
    • Huduma ya Uvuvi
    • Huduma ya Ufugaji
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu
    • Ratiba ya Vikao
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati wa Halmashauri
    • Ripoti
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Maktaba ya picha
    • Video za shughuli za ofisi au Kitaifa
    • Hotuba

MANISPAA YA IRINGA MSHINDI WA 3 USAFI WA MAZINGIRA

Posted on: May 10th, 2024

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt.Philip Mpango  amekabidhi cheti pamoja na zawadi ya fedha Tsh. Milioni moja kwa Mstahiki Meya wa Halmashauri ya Manispaa ya Iringa Mhe. Ibrahim Ngwada mara baada ya Halmashauri hiyo kuibuka mshindi wa 3 kati ya Manispaa 184 katika mashindano ya Afya na Mazingira kundi la Halmashauri za Manispaa Tanzania Bara mwaka 2024.

Zawadi hiyo ilikabidhiwa na  Waziri wa Afya  Mhe. Ummy  Mwalimu kwa niaba ya mgeni rasmi katika hafla fupi ya Uzinduzi wa Kampeni ya “Mtu ni Afya” awamu ya pili  yenye kauli mbiu inayosema “Mtu ni Afya,Afya Yangu Wajibu Wangu” , uliofanyika  eneo la Stendi ya zamani Maili moja Wilaya ya Kibaha Mkoani Pwani Mei 09 2024.

Uzinduzi huo umehudhuriwa na viongozi mbalimbali wa Serikali akiwemo Naibu waziri wa TAMISEMI Mhe. Festo Dugange, Mkuu wa Mkoa wa Pwani Mheshimiwa Alhaj. Abubakar Kunenge, Mkuu wa Mkoa wa Iringa Mhe. Peter Serukamba na Katibu Tawala Wilaya ya Iringa ndg. Michael Semindu, Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Iringa Komrade Daud Yassin, Katibu wa CCM Mkoa wa Iringa, Mstahiki Meya wa Manispaa ya Iringa Mhe. Ibrahim Ngwada, Naibu Meya wa Manispaa Iringa Mhe. Julius Sawani, Mwenyekii wa Kamati ya Uchumi, Afya na Elimu Mhe.Eliud Mvella, Kaimu Mkurugenzi Manispaa Dkt. Godfrey Mbangali, Kamati ya Ulinzi na Usalama Mkoa na Wilaya-Pwani, Wataalamu wa Afya kutoka Manispaa ya Iringa, Wanachi, na Wasanii mbalimbali.

Akizungumza katika hafla hiyo Dkt Mpango amesema ili kufanikisha kampeni hii atatumia wadau mbalimbali huku akiwataja wasanii pamoja na wanahabari kuwa na nafasi kubwa ya kuhamasisha na kuujulisha umma  na kufikisha ujumbe kama ambavyo tayari wamekwisha kuanza kufanya kupitia awamu ya kwanza na huku akizitaka Halmashauri kuwatumia vizuri wahudumu wa afya ngazi ya jamii katika kutoa elimu zaidi katika masuala ya afya na usafi.

“Watumieni vizuri wahudumu wa afya ngazi ya msingi kwani kwa  kufanya kampeni na itakuwa na mafanikio makubwa, viongozi wa Serikali za Mitaa wekezeni katika kudhibiti taka ngumu, maji taka ongezeni kasi ya ujenzi wa Mitaro, utoaji taka kwa wakati na zijengeeni uwezo timu za Menejimenti kwa kufanya hivyo mtaepusha magonjwa ya mlipuko katika maeneo yenu. Amesema Dkt.Mpango


Mstahiki Meya Mhe. Ibrahim Ngwada amesema siri ya mafanikio hayo ni uwekaji wa mapipa ya taka (dustbin) katika maeneo yote ya Halmashauri ikiwa ni pamoja na maeneo ya pembezoni mwa barabara, kuwa na utamaduni wa kufanya usafi mara kwa mara na kulinda afya ya jamii kwa watalaamu kutoa elimu ya kujikinga na mgonjwa ya mlipuko pia ameahidi kufafanyia kazi maelezo yaliyotolewa na Mgeni rasmi Dkt. Mpango.

Mashindano haya hufanyika kila mwaka na kwa takribani miaka 5 mfululizo  Manispaa imekuwa ikishika nafasi ya kwanza na ya pili kwa mwaka 2023 imeshika nafasi ya 3 huku ushindi wa ujumla wa usafi wa  mazingira na ujenzi wa vyoo bora mwaka 2024, huku nafasi ya mshindi ya kwanza ikishikiliwa na Manispaa ya Shinyanga na nafasi ya pili ni Manispaa ya Moshi.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUONGEZWA MUDA WA KUCHUKUA FOMU YA UJENZI WA JENGO LA BIASHARA TEMBO BAR February 15, 2024
  • MATOKEO YA KIDATO CHA SITA, 2023/2024 July 13, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI July 17, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI July 23, 2024
  • Soma zote

Habari za Hivi punde

  • PPP CENTRE YATOA MAFUNZO KWA WATAALAMU IRINGA MC

    April 04, 2025
  • ALUTE: "HAKIKISHENI MIRADI INAKAMILIKA KWA WAKATI NA KWA UBORA"

    December 21, 2024
  • UCHAGUZI HURU NA WA HAKI UNAHITAJI USHIRIKISHAJI - RC SERUKAMBA

    October 10, 2024
  • MSIGALA AWAONYA MAAFISA MAENDELEO KUJIHUSISHA NA MIKOPO HEWA

    October 05, 2024
  • Soma zote

Video

MEYA WA MANISPAA KUZIPIGANIA TIMU ZA MKOA KUPANDA DARAJA
More Videos

Viunganisho vya Haraka

  • National Examination Council of Tanzania
  • Watumishi Portal
  • MATOKEO YA KIDATO CHA SITA,2023/2024
  • Sheria ndogo za Manispaa
  • Vivutio vya Utalii na Taarifda zake
  • Taarifa kwa vyombo vya Habari

Tovuti Zinazofanana

  • Goverment Website
  • TAMISEMI
  • Iringa Region Website
  • IMtv Fahari ya Iringa

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

https://bachelorthesiswritingservice.com

Location Map

Wasiliana nasi

    Iringa Municipal Council

    Sanduku la Posta: 162

    Telephone: +255-2702647

    Mobile: 255-2702647

    Email: md@iringamc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya usiri
    • Ukanusho
    • MMM
    • Ramani ya eneo
    • Huduma zetu

hakimiliki@2017Iringa Manispaa haki zote zimehifadhiwa