• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
HALMASHAURI YA MANISPAA YA IRINGA
HALMASHAURI YA MANISPAA YA IRINGA

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA OFISI YA RAIS TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA HALMASHAURI YA MANISPAA YA IRINGA

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Mipango Miji
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Afya
      • Maji
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Environment and Cleaning
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Kazi
    • Vitengo
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji nyuki
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Ufugaji
    • Kilimo
  • Huduma zetu
    • Huduma ya elimu
    • Huduma ya Afya
    • Huduma ya Maji
    • Huduma ya kilimo
    • Huduma ya Uvuvi
    • Huduma ya Ufugaji
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu
    • Ratiba ya Vikao
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati wa Halmashauri
    • Ripoti
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Maktaba ya picha
    • Video za shughuli za ofisi au Kitaifa
    • Hotuba

MEYA IRINGA ATAKA JAMII KUKEMEA UKATILI WA WATOTO,WANAWAKE

Posted on: December 11th, 2021

Na Mwandishi Wetu, Iringa

MSTAHIKI Meya wa Halmashauri ya Manispaa ya Iringa, Mhe.Ibrahimu Ngwada, ameitaka jamii kupinga na kukemea kwa nguvu zote vitendo vya ukatili wa watoto na wanawake ambavyo vinaonekana kukithiri.

Alisema kesi za ukatili dhidi ya watoto na wanawake ni nyingi hivyo  tunapaswa kupinga ukatili huu kwa nguvu zote  na kukemea matendo hayo yasiyokuwa na maadili.

Alisema hayo wakati maadhimisho ya siku 16 za kupinga ukatili wa kijinsia dhidi ya watoto ambapo Halmashauri ya  Manispaa ya Iringa iliazimisha siku hiyo kwa kufanya maandamano yaliyoongozwa Mhe.Ngwada.

Kilele cha maadhimisho hayo hufanyika Disemba 10  kila mwaka Duniani kote na kwa mwaka 2021 Manispaa imeadhimisha kwa kufanya maandamano yaliyoanzia eneo la FFU Kata ya Kihesa na kumalizia kwenye uwanja wa Shule ya msingi Mlandege.

Akizungumza baada ya maandamano hayo, Mhe. Ngwada alisema inakatisha tamaa kuona vitendo vya ukatili wa watoto na wanawake vinafanywa na watu wenye akili timamu  na wanaojua jema na baya.

"Natoa rai kwa jamii kushirikiana kwa pamoja ili kukomesha vitendo hivi mara moja," alisema Mhe.Ngwada.

Kwa upande wake Afisa Ustawi wa Jamii Manispaa ya Iringa, Bi.Tiniel Mbaga amesema lengo la maadhimisho hayo ni kuhamasisha jamii kushiriki mapambano dhidi ya vitendo vya ukatili kwani msingi wa vitendo hivyo ni familia, wazazi na walezi ambavyo hufanyika majumbani na wanaofanya ni ndugu wa karibu, wazazi na walezi.

"Hatuawezi kuwa na ulinzi na usalama wa kutosha kwa wanawake na watoto endapo wataendeleza vitendo hivi vya kikatili kwa sababu ukatili huu unafanyika kwa kificho hivyo ulinzi kwa wanawake na watoto unakuwa mdogo kwa sababu hawajitokezi kuleta malalamiko hayo," alisema Mbaga.

Mbaga amesema kuwa ukatili unasababishwa na mambo kama ulevi, mila na desturi, mfumo dume  na kutokuwepo kwa hali za kuheshimu watoto majumbani.

Naye Bi.Editha Kayumba ambaye ni Mkaguzi Msaidizi Dawati la Jinsia na Watoto amesema watoto wanafanyiwa ukatili kwa kuajiriwa wakiwa na umri mdogo, kukatishwa shule pia hata kulawitiwa kitendo ambacho kinatengeneza chuki na kisasi kikubwa mioyoni mwao hata  kufikia hatua ya kulipa kisasi kwa vitendo walivyofanyiwa nyuma.

Mtumishi wa Mungu wa  Kanisa la Kilutheri Tanzania mama Mchungaji Upendo Koko amesema, mimba za utotoni zinakatisha ndoto za watoto , ugomvi katika familia pia ni chanzo, cha ukatili suala la kujithamini binafsi na kujipenda mwenyewe na kusema kila ukatili una kisasi chake.

Maadhimisho hayo yamefanyika  tarehe 11/12/2021  yalihudhuriwa na viongozi mbalimbali wakiwamo wa Chama  Cha Mapinduzi  (CCM) na Serikali ,Watumishi na wananchi wa Manispaa ya Iringa ambapo wataalamu walipata nafasi ya kutoa elimu katika maeneo ya soko kuu, soko la mashine tatu,stendi ya Mlandege,Stendi ya zamani  na  uwanja wa mlandege Shule ya msingi.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUONGEZWA MUDA WA KUCHUKUA FOMU YA UJENZI WA JENGO LA BIASHARA TEMBO BAR February 15, 2024
  • MATOKEO YA KIDATO CHA SITA, 2023/2024 July 13, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI July 17, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI July 23, 2024
  • Soma zote

Habari za Hivi punde

  • PPP CENTRE YATOA MAFUNZO KWA WATAALAMU IRINGA MC

    April 04, 2025
  • ALUTE: "HAKIKISHENI MIRADI INAKAMILIKA KWA WAKATI NA KWA UBORA"

    December 21, 2024
  • UCHAGUZI HURU NA WA HAKI UNAHITAJI USHIRIKISHAJI - RC SERUKAMBA

    October 10, 2024
  • MSIGALA AWAONYA MAAFISA MAENDELEO KUJIHUSISHA NA MIKOPO HEWA

    October 05, 2024
  • Soma zote

Video

MEYA WA MANISPAA KUZIPIGANIA TIMU ZA MKOA KUPANDA DARAJA
More Videos

Viunganisho vya Haraka

  • National Examination Council of Tanzania
  • Watumishi Portal
  • MATOKEO YA KIDATO CHA SITA,2023/2024
  • Sheria ndogo za Manispaa
  • Vivutio vya Utalii na Taarifda zake
  • Taarifa kwa vyombo vya Habari

Tovuti Zinazofanana

  • Goverment Website
  • TAMISEMI
  • Iringa Region Website
  • IMtv Fahari ya Iringa

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

https://bachelorthesiswritingservice.com

Location Map

Wasiliana nasi

    Iringa Municipal Council

    Sanduku la Posta: 162

    Telephone: +255-2702647

    Mobile: 255-2702647

    Email: md@iringamc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya usiri
    • Ukanusho
    • MMM
    • Ramani ya eneo
    • Huduma zetu

hakimiliki@2017Iringa Manispaa haki zote zimehifadhiwa