• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
HALMASHAURI YA MANISPAA YA IRINGA
HALMASHAURI YA MANISPAA YA IRINGA

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA OFISI YA RAIS TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA HALMASHAURI YA MANISPAA YA IRINGA

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Mipango Miji
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Afya
      • Maji
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Environment and Cleaning
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Kazi
    • Vitengo
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji nyuki
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Ufugaji
    • Kilimo
  • Huduma zetu
    • Huduma ya elimu
    • Huduma ya Afya
    • Huduma ya Maji
    • Huduma ya kilimo
    • Huduma ya Uvuvi
    • Huduma ya Ufugaji
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu
    • Ratiba ya Vikao
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati wa Halmashauri
    • Ripoti
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Maktaba ya picha
    • Video za shughuli za ofisi au Kitaifa
    • Hotuba

MILIONI 3 ZATOLEWA NA MSTAHIKI MEYA MANISPAA YA IRINGA KWA LIPULI FC | HAMASA MCHEZO WAO DHIDI YA MAWENZI MARKET FC

Posted on: February 19th, 2021

Mstahiki Meya wa Halmashauri ya Manispaa ya Iringa Mh. Ibrahim Ngwada amekabidhi shilingi Milini 3 kwa Timu ya Lipuli leo tarehe 19.02.2021, kama hamasa kuelekea katika mchezo baina yao dhidi ya Mawenzi Market FC ya Morogoro.

Aidha Mh. Ngwada amekabidhi pesa hiyo kwa mchanganuo wa laki moja kwa kila mchezaji na benchi la ufundi huku akiwatakia heri ya mchezo huo utakaochezwa kesho kwenye majira ya saa kumi jioni

Sambamba na hilo Mh. Ngwada akizungumza na wachezaji hao katika ukumbi wa mikutano wa Manispaa amesema "sisi kama viongozi tunahitaji kuona timu ya Lipuli inapanda daraja na kwenda kucheza katika Ligi kuu"

"Sisi kama Halmashauri, tupo tayari kuwa mmoja ya wadau, na mimi kama Meya nipo tayari kwa timu hii ya Lipuli kushirikiana nayo ili kuhakikisha inapata mafanikio" Mh. Ngwada alisema

Aidha amesema, yeye kama kiongozi dhamira yake ni kuhakikisha anashirikiana na chama cha mpira wa miguu na uongozi wa Lipuli katika kuifanya timu kuwa na chachu ya maendeleo hasa katika kujiingizia kipato na kupanda kwa daraja

"Jiwekezeni katika michezo ndio ajira yenu, zingatieni mafunzo ipo siku mtafika mbali zaidi ya hapo huku heshima yenu na nidhamu ndio itakayo wapa kufika viwango vya juu zaidi" Hayo yamezungumzwa na Naibu Waziri, Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia watu Wenye Ulemavu Mhe. Ummy Nderiananga akiwa kama mmoja wa aliyeshiriki katika tukio hilo

Kwa upande wake Mwenyekiti wa UVCCM Wilaya ya Iringa Ndg. Salvatory Ngelela, amempongeza Mstahiki Meya kwa kuifanyia kazi Ilani ya Chama Cha Mapinduzi katika upande wa Michezo na kutimiza ahadi yake wakati alipokuwa akiomba kura kwa wananchi kuwa angezisaidia timu za mpira wa miguu zilizopo katika Halmashauri yake

Rita Kabati, Mbunge wa Viti Maalum Jimbo la Iringa Mjini naye amewataka viongozi wa Lipuli na mpira wa miguu, wasiache kuwashirikisha changamoto zao ili kama viongozi wajue ni kwa namna gani wataweza kuwasaidia huku akiamini timu ya Lipuli inaenda kupanda daraja katika msimu huu

Mwenyekiti wa Timu ya Lipuli Ndg. Mussa Wanguvu, amemshukuru Mstahiki Meya kwa mchango wake dhidi ya timu ya Lipuli huku akimkabidhi tisheti ya uwananchama wa heshima katika timu yake

"Tunashukuru sana Mstahiki kwa ulichokifanya, na sisi tunakuahidi siku ya kesho kufanya vizuri katika matokeo dhidi ya Mawenzi Market" Mwenyekiti wa Lipuli aliongezea kwa kusema hayo

Kwa upande wake nahodha wa timu ya Lipuli Ndg. Hamis Mroki ameahidi kwa niaba ya wachezaji kuonesha nidhamu, kufanya vizuri mpaka kurudi katika Ligi kuu huku akibainisha moja ya changamoto yao kuwa ni ukosefu wa viatu wakati wa mazoezi.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUONGEZWA MUDA WA KUCHUKUA FOMU YA UJENZI WA JENGO LA BIASHARA TEMBO BAR February 15, 2024
  • MATOKEO YA KIDATO CHA SITA, 2023/2024 July 13, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI July 17, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI July 23, 2024
  • Soma zote

Habari za Hivi punde

  • PPP CENTRE YATOA MAFUNZO KWA WATAALAMU IRINGA MC

    April 04, 2025
  • ALUTE: "HAKIKISHENI MIRADI INAKAMILIKA KWA WAKATI NA KWA UBORA"

    December 21, 2024
  • UCHAGUZI HURU NA WA HAKI UNAHITAJI USHIRIKISHAJI - RC SERUKAMBA

    October 10, 2024
  • MSIGALA AWAONYA MAAFISA MAENDELEO KUJIHUSISHA NA MIKOPO HEWA

    October 05, 2024
  • Soma zote

Video

MEYA WA MANISPAA KUZIPIGANIA TIMU ZA MKOA KUPANDA DARAJA
More Videos

Viunganisho vya Haraka

  • National Examination Council of Tanzania
  • Watumishi Portal
  • MATOKEO YA KIDATO CHA SITA,2023/2024
  • Sheria ndogo za Manispaa
  • Vivutio vya Utalii na Taarifda zake
  • Taarifa kwa vyombo vya Habari

Tovuti Zinazofanana

  • Goverment Website
  • TAMISEMI
  • Iringa Region Website
  • IMtv Fahari ya Iringa

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

https://bachelorthesiswritingservice.com

Location Map

Wasiliana nasi

    Iringa Municipal Council

    Sanduku la Posta: 162

    Telephone: +255-2702647

    Mobile: 255-2702647

    Email: md@iringamc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya usiri
    • Ukanusho
    • MMM
    • Ramani ya eneo
    • Huduma zetu

hakimiliki@2017Iringa Manispaa haki zote zimehifadhiwa