Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Iringa Bi. Wamoja Ayubu Ameutaka uongozi wa Manispaa ya Iringa kuongeza juhudi katika kuimarisha Elimu ya Msingi katika kikao kazi cha Kitaifa cha kupokea Matokeo ya Darasa la saba kwa mwaka 2017 kilicho fanyika Ukumbi wa Siasa ni Kilimo siku ya ijumaa tarehe 8/12/2017.
Aidha Bi, Ayubu amewapongeza Wakuu wa shule zote za Msingi kwa kufanya vizuri katika kipindi chote cha maandalizi ya mtihani wa Darsa la saba kwa watahiniwa ambayo imepelekea kupata matokeo mazuri kwa kupata nafasi ya nne (4) Kimkoa kati ya Mikoa ishirini na sita (26) ya Tanzania.
Mbali na hayo amewataka Wenyeviti na Maafisa Elimu msingi kuhakikisha Shule ambazo hazijakamilika zikamilike kwa haraka, na baadhi ya Shule ziongezewe vyumba vya Madarasa ili Watoto ambao wamechaguliwa kuingia Kidato cha kwanza wasikose nafasi.
Kikao kazi hicho hufanyika kila mwaka Kitaifa mbapo matokeo ya Darasa la Saba hutangazwa na kukabidhiwa Halmashuri mbalimbali kwa ajili yamaandalizi ya watahiniwa kuanza kidato cha Kwanza.
Iringa Municipal Council
Sanduku la Posta: 162
Telephone: +255-2702647
Mobile: 255-2702647
Email: md@iringamc.go.tz
hakimiliki@2017Iringa Manispaa haki zote zimehifadhiwa