• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
HALMASHAURI YA MANISPAA YA IRINGA
HALMASHAURI YA MANISPAA YA IRINGA

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA OFISI YA RAIS TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA HALMASHAURI YA MANISPAA YA IRINGA

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Mipango Miji
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Afya
      • Maji
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Environment and Cleaning
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Kazi
    • Vitengo
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji nyuki
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Ufugaji
    • Kilimo
  • Huduma zetu
    • Huduma ya elimu
    • Huduma ya Afya
    • Huduma ya Maji
    • Huduma ya kilimo
    • Huduma ya Uvuvi
    • Huduma ya Ufugaji
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu
    • Ratiba ya Vikao
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati wa Halmashauri
    • Ripoti
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Maktaba ya picha
    • Video za shughuli za ofisi au Kitaifa
    • Hotuba

SAWANI-NAIBU MEYA APATA USHINDI WA KISHINDO.

Posted on: September 9th, 2024

Baraza la Madiwani la Halmashauri ya Manispaa ya Iringa limemchagua Mhe. Juli Sawani kuwa Naibu Meya wa Manispaa ya Iringa katika Uchaguzi uliofanyika kwenye Mkutano wa Baraza la Madiwani wa Mwaka  Jumatatu 09, Septemba 2024 katika ukumbi wa Manispaa ya Iringa .

Akiongoza mchakato wa uchaguzi huo Meya wa Manispaa ya Iringa, Mhe. Ibrahim Ngwada amesema kuwa uchaguzi huo unazingatia kanuni na taratibu za uongozi wa Baraza hilo ambapo hushirikisha wajumbe (Madiwani) kupiga kura na kumchagua Naibu Meya na Uteuzi wa wajumbe wa kamati za kudumu ambao wataongoza kwa muhula wa Mwaka Moja (2024/25) mpaka kufikia uchaguzi mkuu

ujao wa Mwaka 2025.

Awali, Uchaguzi huo ulifanywa na wajumbe 21 ambao walipiga kura za Ndiyo na Hapana ambapo madiwani wote 21 walimpigia kura za Ndiyo Mheshimiwa Sawani na kumpa ushindi usio na mpinzani.

Akiongea baada ya ushindi huo, Mhe. Sawani ametoa shukrani za dhati kwa  Mstahiki Meya wa Manispaa ya Iringa na  Madiwani kwa ujumla kwa ushirikiano waliounyesha katika muda wote ambao wamefanya kazi na Chama Cha Mapinduzi(CCM) kiujumla kwa kuendelea kumuamini na kumpigia kura hivyo kuahidi kushirikiana nao katika kuwatumikia wananchi wa Iringa kwa lengo la kuwaletea maendeleo.

 "Nawashukuru sana Waheshimiwa

Madiwani, Mkurugenzi na Wataalamu kwa ushirikiano mliounesha kwa mwaka uliopita. Nawashukuru pia kwa kuniamini na kunichagua kuwa kiongozi wenu tena, Naahidi kushirikiana nanyi ili tukamilishe na kutekeleza ahadi tulizotoa kwa wananchi,pia naahidi tutashirikiana na Mstahiki Meya wa Manispaa katika kumshauri mambo mbalimbali ya maendeleo na yanayogusa kutatua kero na matatizo ya wananchi wa Manispaa kiujumla". Amesema Sawani.

Aidha, kikao hicho kiliambatana na uundaji wa Kamati za Kudumu za Halmashauri pamoja na uchaguzi wa Wenyeviti wa Kamati hizo ambapo  Mwenyekiti wa Kamati  ya kudhibiti ukimwi kwa mujibu wa kanuni ni Naibu Meya ambaye ni Ndg. Juli Sawani, Kamati ya Mipangomiji na Mazingira ilimchagua Mhe.Hamid Mbata, Mwenyekiti

aliyechaguliwa kwenye Kamati ya Uchumi, Afya na Elimu ni Mhe. Eliud Mvela huku Kamati ya Maadili ilimchagua Mhe. Mahadhi Hepautwa, na Kamati ya Mfuko wa Jimbo imewateua Waheshimiwa Kenyata Likotiko na Hellen Machibya. Kamati ya Bodi ya ajira  aliyeteuliwa ni Mhe. Hamid Mbata

Wajumbe wengineo  walioteuliwa ni  wawakilishi wa ALAT Mkoa ambao ni Mhe. Juli Sawani na Pascalina Lweve. Mwakilishi aliyeteuliwa kwenye Bodi ya IRUWASA ni Mhe. Thadeus Tenga Wajumbe wawakilishi kwa Kamati ya kugawa Ardhi ni Mhe. Hellen Machibya na Amri Kalinga.,Kamati ya Fedha na uongozi itakuwa chini ya Mstahiki Meya wa Manispaa ya Iringa,Naibu  Meya, wenyeviti wa kamati zote pamoja na Mhe.Amri Kalinga  na  Mhe.Christina  Ngohani wajumbe wa kuteuliwa

Akifunga kikao hicho Mstahiki Meya wa Manispaa ya Iringa Mhe. Ibrahim Ngwada amewaasa Madiwani, Mkurugenzi na Wataalamu wa Manispaa kufanya kazi kwa ushirikiano ili kuongeza mapato ya Halmashauri na hatimaye kuweza kukamilisha miradi ya Manispaa kwa nia ya  kuwaletea maendeleo wananchi na Taifa kwa ujumla.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUONGEZWA MUDA WA KUCHUKUA FOMU YA UJENZI WA JENGO LA BIASHARA TEMBO BAR February 15, 2024
  • MATOKEO YA KIDATO CHA SITA, 2023/2024 July 13, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI July 17, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI July 23, 2024
  • Soma zote

Habari za Hivi punde

  • PPP CENTRE YATOA MAFUNZO KWA WATAALAMU IRINGA MC

    April 04, 2025
  • ALUTE: "HAKIKISHENI MIRADI INAKAMILIKA KWA WAKATI NA KWA UBORA"

    December 21, 2024
  • UCHAGUZI HURU NA WA HAKI UNAHITAJI USHIRIKISHAJI - RC SERUKAMBA

    October 10, 2024
  • MSIGALA AWAONYA MAAFISA MAENDELEO KUJIHUSISHA NA MIKOPO HEWA

    October 05, 2024
  • Soma zote

Video

MEYA WA MANISPAA KUZIPIGANIA TIMU ZA MKOA KUPANDA DARAJA
More Videos

Viunganisho vya Haraka

  • National Examination Council of Tanzania
  • Watumishi Portal
  • MATOKEO YA KIDATO CHA SITA,2023/2024
  • Sheria ndogo za Manispaa
  • Vivutio vya Utalii na Taarifda zake
  • Taarifa kwa vyombo vya Habari

Tovuti Zinazofanana

  • Goverment Website
  • TAMISEMI
  • Iringa Region Website
  • IMtv Fahari ya Iringa

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

https://bachelorthesiswritingservice.com

Location Map

Wasiliana nasi

    Iringa Municipal Council

    Sanduku la Posta: 162

    Telephone: +255-2702647

    Mobile: 255-2702647

    Email: md@iringamc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya usiri
    • Ukanusho
    • MMM
    • Ramani ya eneo
    • Huduma zetu

hakimiliki@2017Iringa Manispaa haki zote zimehifadhiwa