• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
HALMASHAURI YA MANISPAA YA IRINGA
HALMASHAURI YA MANISPAA YA IRINGA

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA OFISI YA RAIS TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA HALMASHAURI YA MANISPAA YA IRINGA

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Mipango Miji
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Afya
      • Maji
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Environment and Cleaning
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Kazi
    • Vitengo
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji nyuki
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Ufugaji
    • Kilimo
  • Huduma zetu
    • Huduma ya elimu
    • Huduma ya Afya
    • Huduma ya Maji
    • Huduma ya kilimo
    • Huduma ya Uvuvi
    • Huduma ya Ufugaji
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu
    • Ratiba ya Vikao
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati wa Halmashauri
    • Ripoti
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Maktaba ya picha
    • Video za shughuli za ofisi au Kitaifa
    • Hotuba

SENDIGA ATOA AGIZO ZITO KWA WAKURUGENZI KUSIMAMIA FEDHA ZA MIRADI YA MAENDELEO *Amshukuru Rais Samia kwa kuupatia Mkoa wa Iringa Sh.8.6 bilioni

Posted on: November 3rd, 2021

Na Mwandishi Wetu, Iringa

MKUU wa Mkoa wa Iringa, Queen Sendiga, amewaagiza wakurugenzi wa halmashauri za Mkoani humo kusimamia shilingi bilioni 8.6 zilizotolewa na Serikali kwa ajili ya miradi ya maendeleo kwa kuhakikisha zinatumika kwa malengo yaliyokusudiwa.

Ametoa agizo hilo Novemba 3, mwaka huu wakati akizungumza kwenye  kikao na watumishi wa Wilaya ya Iringa na wa Halmashauri ya Manispaa ya Iringa kilichofanyika kwenye ukumbi wa Orofea uliopo kata ya Kitanzini mjini Iringa.

Katika kikao hicho, Sendiga alimshukuru Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan kwa kutoa fedha  Sh bilioni 8.6 katika Mpango wa Maendeleo kwa ustawi wa Taifa na mapambano dhidi ya UVIKO-19  kwa Mkoa wa Iringa.

"Wakurugenzi hakikisheni fedha hizo mnazisimamia vyema ziweze kutumika kama zilivyokusudiwa na kukamilisha miradi kwa wakati uliopangwa ili kutatua changamoto katika jamii," alisema Sendiga.

Aidha, Mkuu wa Mkoa wa Iringa amewataka watumishi kumpa ushirikiano katika kutekeleza majukumu yake ili kuleta maendeleo chanya Mkoani hapa.

"Niwaombe watumishi tushirikiane na kila mmoja atimize wajibu wake nami nitawapa ushirikiano wa kutosha kwani  sisi tunategemeana katika utekelezaji wa majukumu," alisema Sendiga.

Pia amewataka watumishi kuacha migogoro na viongozi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) hususani waheshimiwa madiwani na badala yake washirikiane nao katika kutekeleza ilani ya chama hicho tawala.

Katika hatua nyingine, Sendiga amepongeza Mkoa wa Iringa kwa kufanya vizuri katika matokeo ya mtihani wa darasa la saba  mwaka 2021 kwa kushika nafasi ya pili kitaifa.

Amesema jitihada zilizofanywa na walimu na kuwawezesha wanafunzi kufanya  vizuri katika mtihani huo ziendelee ili Iringa izidi kung'ara kitaifa katika matokeo ya miaka ijayo.

Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Iringa, Mohamed Moyo amewataka wakuu wa Idara na vitengo kuzingatia changamoto zilizotolewa na wasaidizi wao  ziwe chachu ya mabadiliko  na wakasimamie mipango yote ya Serikali iweze kutekelezeka kwa wakati na kuleta tija.

Awali akijibu maswali ya baadhi ya watumishi Sandiga alisema amezichukua changamoto hizo  ikiwamo kucheleshwa kwa stahiki zao na ucheleweshwaji wa kupanda madaraja kwamba atahakikisha zinapatiwa  ufumbuzi wa haraka.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUONGEZWA MUDA WA KUCHUKUA FOMU YA UJENZI WA JENGO LA BIASHARA TEMBO BAR February 15, 2024
  • MATOKEO YA KIDATO CHA SITA, 2023/2024 July 13, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI July 17, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI July 23, 2024
  • Soma zote

Habari za Hivi punde

  • PPP CENTRE YATOA MAFUNZO KWA WATAALAMU IRINGA MC

    April 04, 2025
  • ALUTE: "HAKIKISHENI MIRADI INAKAMILIKA KWA WAKATI NA KWA UBORA"

    December 21, 2024
  • UCHAGUZI HURU NA WA HAKI UNAHITAJI USHIRIKISHAJI - RC SERUKAMBA

    October 10, 2024
  • MSIGALA AWAONYA MAAFISA MAENDELEO KUJIHUSISHA NA MIKOPO HEWA

    October 05, 2024
  • Soma zote

Video

MEYA WA MANISPAA KUZIPIGANIA TIMU ZA MKOA KUPANDA DARAJA
More Videos

Viunganisho vya Haraka

  • National Examination Council of Tanzania
  • Watumishi Portal
  • MATOKEO YA KIDATO CHA SITA,2023/2024
  • Sheria ndogo za Manispaa
  • Vivutio vya Utalii na Taarifda zake
  • Taarifa kwa vyombo vya Habari

Tovuti Zinazofanana

  • Goverment Website
  • TAMISEMI
  • Iringa Region Website
  • IMtv Fahari ya Iringa

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

https://bachelorthesiswritingservice.com

Location Map

Wasiliana nasi

    Iringa Municipal Council

    Sanduku la Posta: 162

    Telephone: +255-2702647

    Mobile: 255-2702647

    Email: md@iringamc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya usiri
    • Ukanusho
    • MMM
    • Ramani ya eneo
    • Huduma zetu

hakimiliki@2017Iringa Manispaa haki zote zimehifadhiwa