• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
HALMASHAURI YA MANISPAA YA IRINGA
HALMASHAURI YA MANISPAA YA IRINGA

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA OFISI YA RAIS TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA HALMASHAURI YA MANISPAA YA IRINGA

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Mipango Miji
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Afya
      • Maji
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Environment and Cleaning
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Kazi
    • Vitengo
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji nyuki
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Ufugaji
    • Kilimo
  • Huduma zetu
    • Huduma ya elimu
    • Huduma ya Afya
    • Huduma ya Maji
    • Huduma ya kilimo
    • Huduma ya Uvuvi
    • Huduma ya Ufugaji
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu
    • Ratiba ya Vikao
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati wa Halmashauri
    • Ripoti
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Maktaba ya picha
    • Video za shughuli za ofisi au Kitaifa
    • Hotuba

ULEVI KUPINDUKIA,IMANI POTOFU CHANZO CHA UKATILI WA KIJINSIA-RC DENDEGO

Posted on: November 26th, 2022

182  WAMERIPOTI KUFANYIWA UKATILI

Imeelezwa kuwa ulevi kupindukia,Imani potofu,Kulegea kwa malezi ya watoto vinachangia kwa kiasi kikubwa vitendo vya ukatili wa kijinsia na watoto Mkoani Iringa.

Hayo yamebainika leo tarehe 26/11/2022  katika kongamano la uzinduzi wa kampeni ya siku 16 za kupinga ukatili wa kijinsia kimkoa lililofanyika katika ukumbi wa siasa na kilimo uliopo Manispaa ya Iringa

Akifungua kongamano hilo  

Mkuu wa Mkoa wa Iringa Mhe.Halima Dendego amesema Iringa bila ukatili wa kijinsia inawezekana ikiwa kila mmoja wetu atatimiza wajibu wake ipasavyo.

Mhe.Dendego amelitaka Jeshi la polisi katika siku 16 za kupinga ukatili wa kijinsia kuweka kipaumbele cha kukabiliana na matukio hayo katika upelelezi ili kuwezesha mahakama kutoa hukumu haraka

Aidha Mhe.Dendego ameyataka mabaraza ya watoto Mkoa wa Iringa yapatayo 1433, club za watoto 341,kamati za malezi  207,wakuuu wa Wilaya,Wakurugenzi na Maafisa watendaji kuzuia matukio hayo kwani yanaharibu nguvu kazi ya Taifa na kupoteza ndoto  za watoto hao.

'Naagiza kila Halmashauri kwenda kutoa Elimu kwenye Mitaa,Kata na Vijijini Mashuleni na vyuoni wakuu wa Wilaya Wakurugenzi,na watendaji wa Kata hakikisheni mnatoa elimu  ya masuala ya ukatili ili wananchi wawe na uelewa mpana kuhusu masuala hayo alisema Dendego'

Awali akisoma risala  ya uzinduzi wa kampeni ya siku 16 za kupinga ukatili  wa kijinsia na watoto Mkoa wa Ironga Bi.Tiniel Mbaga Afisa Ustawi wa Jamii Manisaa ya Iringa amesema juhudi za kupambana na  vitendo vya ukatili wa kijinsia zimekuwa zikifanywa na Halmashauri kwa kushirikiana na  wadau mbalimbali kama vile; Taasisi za umma,Mashirika yasiyo ya kiserikali,Taasisi za dini,vyombo vya habari,vyama vya Siasa na viongozi mbalimbali,vyuo vikuu,vyuo vya kati na makampuni ya watu binafsi.

Mbaga amesema juhudi hizo zimekuwa zikilenga kupunguza matukio ya ukatili kwa kuzuia vitendo vya ukatili visitokee na kuitikia pale vinapotokea.

Pamoja na jitijada hizo  bado wanakabiliwa na changamoto mbali mbali wanaposhughulikia masuala ya ukatili kama vile;baadhi ya wananchi kutokuwa na ushirikiano wa kutosha katika kushughulikia mashauri ya ukatili hasa watendaji wa makosa wanapokuwa ni ndugu wa karibu,kesi za ukatili kuchukua muda mrefu mahakamani jambo ambalo linatoa mwanya wa maridhiano baina ya pande mbili na kupelekea kesi kuharibika.

Akisoma ripoti ya matukio ya ukatili ya Mkoa mbele ya mgeni rasmi,Mkaguzi Msaidizi ndg.Paul Bundala amesema matukio 182 ya ubakaji yameripotiwa kwa kipindi cha januari hadi Oktoba mwaka 2022 sawa na  asilimia 47 miongoni mwa matukio 384.

Aidha amesema kwa upande wa takwimu za Kitaifa jumla ya matukio 29,373 ya ukatili yaliripotiwa Mwaka 2021 yakihusisha ubakaji,ulawiti, ngono na wanafunzi huku Mikoa ya Arusha,Dare es salaam,Tanga na Rukwa ikiongoza kwa matukio hayo ya ukatili.

Siku 16 za kupinga ukatili  huadhimishwa Novemba 25 hadi Disemba 10 kila mwaka.kauli mbiu ya mwaka huu inasema 'KILA UHAI UNA THAMANI.TOKOMEZA MAUAJI NA UKATILI DHIDI YA WANAWAKE NA WATOTO'

Matangazo

  • TANGAZO LA KUONGEZWA MUDA WA KUCHUKUA FOMU YA UJENZI WA JENGO LA BIASHARA TEMBO BAR February 15, 2024
  • MATOKEO YA KIDATO CHA SITA, 2023/2024 July 13, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI July 17, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI July 23, 2024
  • Soma zote

Habari za Hivi punde

  • PPP CENTRE YATOA MAFUNZO KWA WATAALAMU IRINGA MC

    April 04, 2025
  • ALUTE: "HAKIKISHENI MIRADI INAKAMILIKA KWA WAKATI NA KWA UBORA"

    December 21, 2024
  • UCHAGUZI HURU NA WA HAKI UNAHITAJI USHIRIKISHAJI - RC SERUKAMBA

    October 10, 2024
  • MSIGALA AWAONYA MAAFISA MAENDELEO KUJIHUSISHA NA MIKOPO HEWA

    October 05, 2024
  • Soma zote

Video

MEYA WA MANISPAA KUZIPIGANIA TIMU ZA MKOA KUPANDA DARAJA
More Videos

Viunganisho vya Haraka

  • National Examination Council of Tanzania
  • Watumishi Portal
  • MATOKEO YA KIDATO CHA SITA,2023/2024
  • Sheria ndogo za Manispaa
  • Vivutio vya Utalii na Taarifda zake
  • Taarifa kwa vyombo vya Habari

Tovuti Zinazofanana

  • Goverment Website
  • TAMISEMI
  • Iringa Region Website
  • IMtv Fahari ya Iringa

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

https://bachelorthesiswritingservice.com

Location Map

Wasiliana nasi

    Iringa Municipal Council

    Sanduku la Posta: 162

    Telephone: +255-2702647

    Mobile: 255-2702647

    Email: md@iringamc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya usiri
    • Ukanusho
    • MMM
    • Ramani ya eneo
    • Huduma zetu

hakimiliki@2017Iringa Manispaa haki zote zimehifadhiwa