• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
HALMASHAURI YA MANISPAA YA IRINGA
HALMASHAURI YA MANISPAA YA IRINGA

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA OFISI YA RAIS TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA HALMASHAURI YA MANISPAA YA IRINGA

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Mipango Miji
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Afya
      • Maji
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Environment and Cleaning
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Kazi
    • Vitengo
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji nyuki
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Ufugaji
    • Kilimo
  • Huduma zetu
    • Huduma ya elimu
    • Huduma ya Afya
    • Huduma ya Maji
    • Huduma ya kilimo
    • Huduma ya Uvuvi
    • Huduma ya Ufugaji
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu
    • Ratiba ya Vikao
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati wa Halmashauri
    • Ripoti
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Maktaba ya picha
    • Video za shughuli za ofisi au Kitaifa
    • Hotuba

Umoja wa SACCOS Tz Wakutana Mkutano Wa Tatu Mkoani Iringa

Posted on: March 15th, 2022

Muungano wa vyama vya Ushirika vya akiba na mikopo Tanzania Tanzania umewakutanisha ma meneja 70 wa vyama mbalimbali vya SACCOS kutokea maeneo tofauti nchini katika mkutano wa tatu wa pamoja wa kujadili masuala yanayohusu vyama vyao pamoja na kubadilishana uzoefu wa utendaji kazi

Mkutano huo utakaotumia siku nne, umeanza leo, Machi 15. 2022 katika ukumbi wa mikutano wa Mount Rayal, mkoani Iringa kikiwa na ajenda mbalimbali pamoja na kuwataka viongozi hao kuwa waadilifu na waminifu katika kutekeleza majukumu yao

Akizungumza Ndugu, Hassani Mnyone, Mtendaji Mkuu wa Muungano wa vyama na ushirika vya akiba na mikopo Tanzania (SACCOS) amesema, ajenda zitakazojadiliwa ni pamoja na kuzungumzia mwenendo soko la huduma za kifedha linavyokwenda na kuzitazama fursa zilizopo, kuzitambua changamoto wanazowapata na kukabiliana nazo, masuala ya uongozi, pamoja na uboreshwaji wa mifumo ya Tehama itakayosaidia kurahisisha utoaji wa huduma zao

Hata hivyo Ndg, Hassani ameongezea kwa kusema baada ya kumaliza mkutano wao, watapata fursa za kutembelea maeneo mbalimbali ya Manispaa ya Iringa katika kutoa elimu ya ushiriki kwa vijana mbalimbali wa bodaboda na kutoa zawadi pamoja na kufanya utalii mdogo utakaoweka alama ya kiuchumi ya ujio wao mkoani hapa

“hata hivyo, tutatembelea kituo cha watoto ambayo ni sehemu yetu ya utekelezaji wa msingi namba 7 wa ushiriki unaosisitiza kuhusu kuijali jamii” alihitimisha kwa kusema hayo Ndugu. Hassani

Kwa upande wake Ndugu. Bosco Simba Meneja wa SACCOS ya walimu Wilaya ya Moshi vijijini Mkoani Kilimanjaro ameitaja changamoto ya Tehama kama ni moja ya kikwazo katika uendeshwaji wa vyama vingi vya SACCOS na hivyo kwasasa wamejipanga kuwekeza na kuimarisha mifumo ya Tehama ili kurahisisha utolewaji wa huduma kwa wanachama wao

Hata hivyo Ndugu. Bosco ameishukuru serikali kwa uwekaji wa mifumo mipya, sheria, sera na kanuni pendwa zenye kuongoza vyama vyao kwa kuzifanya ziwe bora zaidi na zenye kuaminiwa na jamii na amesema utoaji wao wa elimu umeleta tija kwa wananchi kuwafanya wajifunze, waelewe na wajiunge katika vyama hivyo

Vilevile ameongezea kwa kusema katika kupunguza matukio ya ubadhilifu wa pesa na katika vyama vyao, wamehakikisha wameendelea kukagua na kujiridhisha kwa viongozi (Mameneja) wanaosimamia vyama hivyo kuwa wanavigezo na ni waadilifu katika kazi hali inayopelekea kuzifanya taasisi zao kuwa zenye kuaminiwa na watu na kuwa na utendaji bora

Mwisho Ndg. Bosco amezitaja SCCULT na Tume ya maendeleo na ushirika (TDCD) ndio taasisi ambazo huzipelekea malalamiko na changamoto zao kwa utatuzi ili kuboresha huduma wanazozifanya

Nae Bi. Elvera Mdee, Meneja wa chama cha ushirika wa akiba na mikopo Samekaya cha Mkoani Kilimanjaro, akiwa mjumbe katika mkutano huo amesema vikao hivyo vinawasaidia kwa kupeana uzoefu, na tangu kuanza kukutana kwao kumesaidia kupungua hali ya kufa kwa vyama ukilinganisha na mwanzoni lakini pia imewapa fursa za kukutana na wataalamu mbalimbali ikiwemo wataalamu wa masuala ya uwekezaji wwkiwapatia elimu ya namna wanavyoweza kuwekeza na kupata faida katika vyama vyao na mwisho amewaomba wananchi kuendelea kuviamini na vyama vyao na kuziamiini huduma zoa na wanaweza kujiunga.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUONGEZWA MUDA WA KUCHUKUA FOMU YA UJENZI WA JENGO LA BIASHARA TEMBO BAR February 15, 2024
  • MATOKEO YA KIDATO CHA SITA, 2023/2024 July 13, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI July 17, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI July 23, 2024
  • Soma zote

Habari za Hivi punde

  • PPP CENTRE YATOA MAFUNZO KWA WATAALAMU IRINGA MC

    April 04, 2025
  • ALUTE: "HAKIKISHENI MIRADI INAKAMILIKA KWA WAKATI NA KWA UBORA"

    December 21, 2024
  • UCHAGUZI HURU NA WA HAKI UNAHITAJI USHIRIKISHAJI - RC SERUKAMBA

    October 10, 2024
  • MSIGALA AWAONYA MAAFISA MAENDELEO KUJIHUSISHA NA MIKOPO HEWA

    October 05, 2024
  • Soma zote

Video

MEYA WA MANISPAA KUZIPIGANIA TIMU ZA MKOA KUPANDA DARAJA
More Videos

Viunganisho vya Haraka

  • National Examination Council of Tanzania
  • Watumishi Portal
  • MATOKEO YA KIDATO CHA SITA,2023/2024
  • Sheria ndogo za Manispaa
  • Vivutio vya Utalii na Taarifda zake
  • Taarifa kwa vyombo vya Habari

Tovuti Zinazofanana

  • Goverment Website
  • TAMISEMI
  • Iringa Region Website
  • IMtv Fahari ya Iringa

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

https://bachelorthesiswritingservice.com

Location Map

Wasiliana nasi

    Iringa Municipal Council

    Sanduku la Posta: 162

    Telephone: +255-2702647

    Mobile: 255-2702647

    Email: md@iringamc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya usiri
    • Ukanusho
    • MMM
    • Ramani ya eneo
    • Huduma zetu

hakimiliki@2017Iringa Manispaa haki zote zimehifadhiwa