• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
HALMASHAURI YA MANISPAA YA IRINGA
HALMASHAURI YA MANISPAA YA IRINGA

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA OFISI YA RAIS TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA HALMASHAURI YA MANISPAA YA IRINGA

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Mipango Miji
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Afya
      • Maji
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Environment and Cleaning
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Kazi
    • Vitengo
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji nyuki
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Ufugaji
    • Kilimo
  • Huduma zetu
    • Huduma ya elimu
    • Huduma ya Afya
    • Huduma ya Maji
    • Huduma ya kilimo
    • Huduma ya Uvuvi
    • Huduma ya Ufugaji
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu
    • Ratiba ya Vikao
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati wa Halmashauri
    • Ripoti
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Maktaba ya picha
    • Video za shughuli za ofisi au Kitaifa
    • Hotuba

USHURU WA BIASHARA KIKWAZO UKUSANYAJI MAPATO RUAHA

Posted on: February 25th, 2024

Kamati ya Fedha na Uongozi Halmashauri ya Manispaa ya Iringa chini ya Diwani wa Kata ya Mkwawa, Mhe. Amri Kalinga imekagua maeneo mbalimbali ya biashara katika Kata ya Ruaha.

Mhe. Kalinga akishirikiana na wataalamu kutoka Manispaa ya Iringa pamoja na viongozi wa eneo husika wamekagua biashara hizo Mtaa wa Ipogolo, Kata ya Ruaha. Huku lengo kuu la ziara ni kukagua Leseni za biashara, Ushuru wa huduma, Kutathmini utekelezaji wa bei elekezi ya sukari kama ilivyopangwa na serikali na Ukusanyaji wa ushuru wa taka.

Katika ziara hiyo wajumbe hao walipata fursa ya kutembelea baadhi ya wafanyabiashara waliopo eneo hilo na kukagua zaidi ya biashara 30 ikiwemo Maduka ya mahitaji ya nyumbani, Duka la nyama, Maduka ya pombe (grocery), Nyumba za kulala wageni, Saluni za kike na kiume, Ofisi za huduma za pesa, Gereji na pamoja na Migahawa.

Timu hiyo imebaini kuwa zaidi ya asilimia 80% ya wafanyabiashara eneo hilo hawana leseni ambapo kuna ambao hawajakata kabisa na wengine leseni zao zimekwisha muda wake. Pia zaidi ya asilimia 90% ya wafanyabiashara eneo hilo hawalipii ushuru wa huduma (service levy).

"Kwa wale ambao hamna leseni, pia hamlipii ushuru wa huduma (service levy) pamoja na ushuru wa taka hakikisheni mnakwenda Halmashauri kupata utaratibu wa malipo ili kuepusha usumbufu. Na baada ya malipo hakikisheni mnaweka hati za malipo kwenye biashara zenu ili ukaguzi unapofanyika iwepo tayari". Amesema Kalinga.

Aidha, Katika ukaguzi wa bei ya sukari timu hiyo haikufanikiwa kupata bei halisi inayotumika kwa wafanyabiashara hao. Kwani maduka waliyofanya  ukaguzi hakukuwa na sukari. Na hiyo imepelekea kutathmini kuwa huenda wafanyabiashara hao wamekuwa wakiuza bidhaa hiyo kwa bei ya juu ambayo haijaelekezwa na serikali.

Mwenyekiti wa Kamati hiyo, ambaye pia ni Mstahiki Meya wa Halmashauri ya Manispaa ya Iringa Mhe. Ibrahim Ngwada baada ya kupata ripoti ya timu zote za ukaguzi wa biashara kutoka Kata mbalimbali za Manispaa ya Iringa ametoa rai kwa wajumbe wa Kamati hiyo washirikiane pamoja na Viongozi wa mitaa kufanya ukaguzi wa biashara mara kwa mara ili kuongeza mapato ya Halmashauri.

"Tuwe na karatasi ambayo itatambua jina la mfanyabiashara, eneo analofanyia biashara, pamoja na namba ya simu mwisho wa siku tutawasilisha kwenye Kamati kwa ajili ya ufuatiliaji wa mapato". Amesema Ngwada.

Mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa ya Iringa Ndg. Kastori Msigala ameshukuru kwa kikao hicho na kuahidi kuwa yale yalioahidiwa yatatekelezwa.

Ziara hiyo imehusisha pia ukaguzi wa maendeleo ya miradi ya Ujenzi wa Ukumbi wa Welfare eneo la Kitanzini unaokisiwa kuwa na thamani ya Shilingi Milioni 44 pamoja na ukamilishaji wa Ujenzi na Miundombinu Stendi ya Igumbilo ambapo ilihusisha timu nzima ya Kamati ya Fedha na Utawala.


Matangazo

  • TANGAZO LA KUONGEZWA MUDA WA KUCHUKUA FOMU YA UJENZI WA JENGO LA BIASHARA TEMBO BAR February 15, 2024
  • MATOKEO YA KIDATO CHA SITA, 2023/2024 July 13, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI July 17, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI July 23, 2024
  • Soma zote

Habari za Hivi punde

  • PPP CENTRE YATOA MAFUNZO KWA WATAALAMU IRINGA MC

    April 04, 2025
  • ALUTE: "HAKIKISHENI MIRADI INAKAMILIKA KWA WAKATI NA KWA UBORA"

    December 21, 2024
  • UCHAGUZI HURU NA WA HAKI UNAHITAJI USHIRIKISHAJI - RC SERUKAMBA

    October 10, 2024
  • MSIGALA AWAONYA MAAFISA MAENDELEO KUJIHUSISHA NA MIKOPO HEWA

    October 05, 2024
  • Soma zote

Video

MEYA WA MANISPAA KUZIPIGANIA TIMU ZA MKOA KUPANDA DARAJA
More Videos

Viunganisho vya Haraka

  • National Examination Council of Tanzania
  • Watumishi Portal
  • MATOKEO YA KIDATO CHA SITA,2023/2024
  • Sheria ndogo za Manispaa
  • Vivutio vya Utalii na Taarifda zake
  • Taarifa kwa vyombo vya Habari

Tovuti Zinazofanana

  • Goverment Website
  • TAMISEMI
  • Iringa Region Website
  • IMtv Fahari ya Iringa

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

https://bachelorthesiswritingservice.com

Location Map

Wasiliana nasi

    Iringa Municipal Council

    Sanduku la Posta: 162

    Telephone: +255-2702647

    Mobile: 255-2702647

    Email: md@iringamc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya usiri
    • Ukanusho
    • MMM
    • Ramani ya eneo
    • Huduma zetu

hakimiliki@2017Iringa Manispaa haki zote zimehifadhiwa