• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
HALMASHAURI YA MANISPAA YA IRINGA
HALMASHAURI YA MANISPAA YA IRINGA

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA OFISI YA RAIS TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA HALMASHAURI YA MANISPAA YA IRINGA

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Mipango Miji
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Afya
      • Maji
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Environment and Cleaning
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Kazi
    • Vitengo
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji nyuki
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Ufugaji
    • Kilimo
  • Huduma zetu
    • Huduma ya elimu
    • Huduma ya Afya
    • Huduma ya Maji
    • Huduma ya kilimo
    • Huduma ya Uvuvi
    • Huduma ya Ufugaji
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu
    • Ratiba ya Vikao
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati wa Halmashauri
    • Ripoti
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Maktaba ya picha
    • Video za shughuli za ofisi au Kitaifa
    • Hotuba

VIJUE VIPAUMBELE KONKI VYA MEYA MANISPAA YA IRINGA 2021

Posted on: January 13th, 2021

“Nipende kuwaomba wataalamu wetu na watumishi wenzangu, ushirikano wa kutosha katika kuiletea maendeleo Manispaa yetu”

Hayo ameyasema Meya wa Manispaa ya Iringa leo Mh. Ibrahim Gwada katika kikao chake na wakuu wa idara na watumishi wote wa Manispaa makao makuu ya Halmashauri kilichofanyika katika ukumbi wa mikutano wa Manispaa

Sambamba na hilo Mh. Ngwada ametumia nafasi hiyo kujitambulisha rasmi mbele ya watumishi hao kwa nafasi yake na kutolea ufafanuzi juu ya mpango mikakati ambayo anaipatia kipaumbele katika uongozi wake hasa kwa kipindi cha kwanza mwaka 2021

Akiendelea kuzungumza mbele ya watumishi hao amesema, moja ya kipaumbele chake kwa mwaka huu ni kutoanzishwa kwa miradi mipya na hivyo kutumia muda mwingi kumalizia miradi yote iliyokwisha kuanzishwa hapo nyuma na vilevile kuboresha miradi ambayo ipo katika uchakavu ambapo ikikamilika itasaidia kuongeza kipato cha Halmashauri

Aidha amesema “nafikiri pia kuwa na vitu vya kushikika, kuundwa ambavyo vitaacha alama katika uongozi wetu hivyo tutaanza na kujenga jengo la TEMBO Bar, na sio lazima kutumia pesa zetu na mbadala wake tutatumia wadau na wabia katika ujenzi huo ambapo itatusaidia kuongeza kipato cha ndani” na akatoa wazo la kuboreshwa upya kwa ukumbi wa Halmashauri wa community centre katika ubora mzuri kama chanzo cha mapato

“katika elimu nimefikiri tuboreshe shule zetu ili ziwe katika muonekano mzuri ambao utasaidia wanafunzi wetu kupata elimu bora bila shida yoyote tukianza na madarasa, vyoo, maabara, mabweni, maktaba na vyote vinavyohitajika katkia shuke bila kusahau viwanja vya michezo” Mh. Meya aliongezea kwa kusema hayo huku akiahidi kuziwezesha timu za mpira wa miguu za ndani kufanya vizuri katika ligi

Mh. Ngwada pia amemaliza kwa kuwataka watumishi hao kutosita kumtafuta kwaajili ya ushauri, au changamoto zozote zinazo wakumba kwa mlengo wa kuzitatua na amewashukuru kwa ushirikiano waliouonesha kipindi cha uchaguzi kwa niaba ya uongozi wa Chama Cha Mapinduzi kumchagua Mbunge nanMadiwani wote kutokea chama hiko

"Msisite kunirekebisha na kuniambia mkiona siko sahihi, hii yote ni katika kujengana kwaajili ya maendeleo ya Halmashauri yetu na mnisaidie kufikia yale malengo ambayo tumejiwekea” Mh. Meya alisisitiza

Kwa upande wake Mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa ya Iringa Ndg. Hamid Njovu amemshukuru Mh. Mstahiki Meya kuzungumza na wataalamu huku akiwaasa watumishi kwa kusema “niwakumbushe wataalamu wenzangu kuwa kila zama ina kitabu chake, hivyo angalia nini inahitajika katika zama hizi na kuwajibika kama inavyotakiwa”

Ndg. Njovu anamaliza kwa kusema “Namshukuru sana Mh. Ngwada amenipunguzia matatizo makubwa sana yaliyokuwa changamoto katika Halmashauri yetu tena kwa kipindi hiki kifupi na kumuahidi kutoa ushirikiano wake kwake kwa kutekeleza mipango yao yote kwa asilimia zote kwa maendeleo ya Manispaa yetu"

“Kama mtamtumia vizuri Mh. Ngwada kwa kipindi hiki cha miaka 5 basi tutaleta maendeleo makubwa” Njovu akihitimisha kikao hicho ameyasema hayo.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUONGEZWA MUDA WA KUCHUKUA FOMU YA UJENZI WA JENGO LA BIASHARA TEMBO BAR February 15, 2024
  • MATOKEO YA KIDATO CHA SITA, 2023/2024 July 13, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI July 17, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI July 23, 2024
  • Soma zote

Habari za Hivi punde

  • PPP CENTRE YATOA MAFUNZO KWA WATAALAMU IRINGA MC

    April 04, 2025
  • ALUTE: "HAKIKISHENI MIRADI INAKAMILIKA KWA WAKATI NA KWA UBORA"

    December 21, 2024
  • UCHAGUZI HURU NA WA HAKI UNAHITAJI USHIRIKISHAJI - RC SERUKAMBA

    October 10, 2024
  • MSIGALA AWAONYA MAAFISA MAENDELEO KUJIHUSISHA NA MIKOPO HEWA

    October 05, 2024
  • Soma zote

Video

MEYA WA MANISPAA KUZIPIGANIA TIMU ZA MKOA KUPANDA DARAJA
More Videos

Viunganisho vya Haraka

  • National Examination Council of Tanzania
  • Watumishi Portal
  • MATOKEO YA KIDATO CHA SITA,2023/2024
  • Sheria ndogo za Manispaa
  • Vivutio vya Utalii na Taarifda zake
  • Taarifa kwa vyombo vya Habari

Tovuti Zinazofanana

  • Goverment Website
  • TAMISEMI
  • Iringa Region Website
  • IMtv Fahari ya Iringa

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

https://bachelorthesiswritingservice.com

Location Map

Wasiliana nasi

    Iringa Municipal Council

    Sanduku la Posta: 162

    Telephone: +255-2702647

    Mobile: 255-2702647

    Email: md@iringamc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya usiri
    • Ukanusho
    • MMM
    • Ramani ya eneo
    • Huduma zetu

hakimiliki@2017Iringa Manispaa haki zote zimehifadhiwa