Timu ya Wataalam kutoka ofisi ya Mkuu wa Mkoa Ikiongozwa na Kaimu Katibu Tawala Bi. Saida Mgeni imefanya ziara ya ufuatiliaji wa utekelezaji wa Miradi ya maendeleo inayotekelezwa na Halmashauri ya Manispaa ya Iringa kwa lengo la kuona mafanikio na changamoto katika Miradi hiyo
Vikundi viliyotembelewa ni pamoja na Envibright kikundi cha vijana kilichopo Gangilonga kinachjishughulisha na uoteshaji wa miti ya asili .Kikundi cha watu wenye ulemavu cha Amani group kilichopo Donbosco kinachojishughulisha na ufugaji wa Sungura na kikundi cha Tupendane vicoba kilichopo Frelimo kinachojishughulisha na ununuaji wa hisa pamoja na ufugaji wa kuku wa mayai
Bi.Mgeni amewataka wanavikundi vinavyotekeleza miradi hiyo kuwa na umoja na ushirikiano ili kuhakikisha wanakuwa na mikakati ya kukuza uchumi wao
Myovela amesema kikundi cha Tupendane vicoba kinafanya vizuri hivyo Mkurugenzi aone namna ya kutatua changamoto zao na kuwawezesha kupata eneo kubwa kwa ajili ya mradi wa ufugaji wa kuku wa mayai ambao walianza kutekeleza tangu mwaka 2020 wakiwa na idadi ya vifaranga 200 na mpaka sasa wanafuga kuku zaidi ya 400
Aidha amevitaka vikundi vinavyonufaika na mikopo ya Manispaa katika makundi ya wanawake, Vijana na watu wenye ulemavu kufanya marejesho kwa wakati ili kupata kiwango kikubwa zaidi pindi wanapomaliza mikopo hiyo na kuomba awamu nyingine pia kutoa nafasi kwa wengine kunufaika na mikopo hiyo
'Rejesheni fedha kwa wakati ili na wengine waweze kunufaika na mikopo, fedha mlizopewa hazina riba mnaposuasua kurejesha mnawafanya wengine kukosa fursa hiyo muhimu alisisitiza Bi.Mgeni"
Benedict Dembe ni Mwenyekiti wa Serikali ya mtaa wa Muungano B. Ametoa wito kwa maafisa Maendeleo ya jamii kutoa elimu ya ujasiriamali kwa vikundi kwani itasaidia kuwapa uelewa wa matumizi sahihi ya fedha wanazopewa ili waweze kutimiza malengo kusudiwa
Awali akisoma taarifa ya kikundi mbele ya Mgeni rasmi Bi.Redemta Mwinyi amemshukuru Mkurugenzi kwa kupitia ofisi ya Maendeleo ya jamii kwa kupata mkopo wa jumla ya shilingi milioni milioni 4 kwa awamu mbili ambazo zimewasaidia kukuza uchumi wa kikundi kupitia mradi huo wa ufugaji wa kuku. Na ameomba waweze kupewa fedha nyingine ili waweze kupanua eneo la ufugaji
Ziara hii ya siku tatu imeanza tarehe 29/6 hadi 1/7/2021 ambayo itatembelea miradi mbalimbali katika kata zote zilizopo Manispaa ya Iringa.
Iringa Municipal Council
Sanduku la Posta: 162
Telephone: +255-2702647
Mobile: 255-2702647
Email: md@iringamc.go.tz
hakimiliki@2017Iringa Manispaa haki zote zimehifadhiwa