Diwani wa Kata ya Kihesa July Sawan amewataka wakazi wa kata ya kihesa kushiriki maendeleo ya kielimu kwa kujitokeza kwa wingi katika mikutano ya hadhara ya kata inayaitishwa na kushirikiana kwa pamoja bila kujali itikadi za vyama vya siasa ili kuchochea maendeleo kwa wanafunzi kutoka kwenye kata yao.
Mh Sawan ametoa wito huo katika mkutano wa hadhara uliofanyika katika viwanja vya ofisi ya kata ya kihesa lengo kuu likiwa ni kujadili agenda ya kukuza elimu kwa wanafunzi wa kata ya kihesa kupitia ujenzi wa vyumba vya Madarasa, agenda nyingine ni pamoja na kutoa taarifa ya shughuli zilizofanyika katika kata ya kihesa kwa kipindi cha mwaka mmoja,kutoa taarifa ya utekelezaji wa mpango wa TASAF na kujadili mpango wa ujenzi wa vyumba 2 vya madarasa.
Aidha diwan wa kihesa Mh.July Sawan alifanya harambee katika mkutano huo na kufanikiwa kupata jumla ya shilingi 450,000/= taslim, ahadi ya shilingi 100,000/= pia ahadi ya mifuko ya saruji sabini,tofali mia mbili, mchanga lori moja kutoka kwa viongozi mbalimbali wa chama cha mapinduzi pamoja na wadau wa maendeleo wa kata ya kihesa katika kuhakikisha wanafunzi 114 waliofaulu na hawajapata madarasa ya kwa ajili ya kujiunga na elimu ya sekondari wanaanza masomo mapema iwezekanavyo.
Katika hatua nyingine wananchi wa kata ya kihesa wamemshukuru mdau wa maendeleo( MNEC) Salim Asas kwa kuwachangia zaidi ya sh milioni 25 kwa ajiliya ujenzi wa frem za biashara, jengo ambalo likikamilika linatarajia kuwanufaisha zaidi ya wajasiliamali 22.
Kiziza Nzali ni mkazi wa kata ya kihesa mtaa wa Dodoma Road A anasema wanampongeza SALIM ASAS kwa kuwajengea jengo hilo kwani litaleta tija kwa wakazi wa kata hiyo kwa kuwaongezea kipato,aidha amewaomba wananchi pamoja na wadau wengine wa maendeleo kujijitokeza kumalizia jengo hilo ili liweze kuleta tija kwa wakazi wa kihesa.
Mradi huu ukikamilika utatumia jumla ya shilingi milioni 40 mpaka sasa umekamilika kwa alisimia 75 na bado asiimia 25 sawa na shilingi miloni 15 zimesalia kukamilisha ujenzi huo.
Iringa Municipal Council
Sanduku la Posta: 162
Telephone: +255-2702647
Mobile: 255-2702647
Email: md@iringamc.go.tz
hakimiliki@2017Iringa Manispaa haki zote zimehifadhiwa