AfisaElimu Sekondari wa Halmashauri ya Manispaa ya Iringa Ndg. Tupe Kayingaameongoza zoezi la ugawaji wa zawadi na vyeti kwa wanafunzi, walimu na shule zandani ya Manispaa zilizoonyesha juhudi katika ufaulu wa mitihani ya kitaifamwaka 2023.
Zoezihilo limefanyika katika Shule ya Sekondari ya Lugalo na kuhudhuriwa na MaafisaElimu Halmashauri ya Manispaa ya Iringa na Wakuu wa Shule za Sekondari Manispaaya Iringa pamoja na wanafunzi kwa lengo la kuzungumza na Walimu na kutathminiMaendeleo ya Taaluma kwa ujumla, pamoja na kutoa zawadi na vyeti kwa waliofanyavizuri.
Kayingaamesema zawadi hizo zimetolewa katika makundi matatu ambayo ni: Moja; Shuleambazo zimeongoza kwa ufaulu katika matokeo yao ukilinganisha na mwaka jana,Pili; Mwalimu mmoja mmoja aliyefanya vizuri katika somo lake kwa kutambuajuhudi binafsi na Tatu; Mwanafunzi aliyefaulu mtihani wa kidato cha nne au pilikwa ufaulu wa Daraja la I ya pointi 7.
"Tunatoazawadi kwa makundi mbalimbali kwa lengo la kutoa motisha Shule zilizofanyavizuri, pia kuongeza hamasa kwa walimu na wanafunzi waweze kufanya vizuri zaidikatika masomo yao na hatimaye kuboresha kiwango cha elimu katika Halmashauriyetu". Amesema Kayinga.
AfisaElimu Taaluma Sekondari Ndg. Yahya Mpongwe amesema mara tu yanapotangazwamatokeo ya mitihani ya kidato cha sita, nne na pili idara ya Elimu na Maafisawake kutoka Halmashauri ya Manispaa ya Iringa hukutana mwezi wa pili baada yamatokeo ya kidato cha nne kwa lengo la kufanya tathmini ya matokeo yote kwaujumla.
"Tunapokutanakwa ajili ya tathmini hatuangalii tuna Daraja la 1 au 2 ngapi, badala yaketunaangalia uchambuzi wa somo mojamoja mwaka jana tulikuwa wapi na mwaka huu tupowapi ili tuweze kujipanga zaidi kwa matokeo yanayofuata". Amesema Mpongwe.
Kwakuongezea, Mpongwe amesema kuwa Shule za Sekondari za Manispaa ya Iringazimeanza kuinuka kutokana na ushirikiano uliopo baina ya Maafisa Elimuwanavyofanya jitihada za kutembelea shule na kuzingatia vigezo vya utendaji wakazi (key performance), pamoja na ushirikiano wa walimu.
Katikazoezi hili Wanafunzi 4 kutoka Shule za Sekondari Lugalo, St. Joseph-Ipogolo, naShule ya Wasichana Iringa waliopata ufaulu wa Daraja la I pointi 7 ambapowamezawadiwa TSh. 100,000 kila mmoja, Shule zilizopandisha ufaulu zimezawadiwavyeti pamoja na Tsh. 50,000 sambamba na hilo wametoa zawadi kwa Walimuwaliofanya vizuri kwenye masomo yao na kusema zoezi hili litakuwa endelevu.
Iringa Municipal Council
Sanduku la Posta: 162
Telephone: +255-2702647
Mobile: 255-2702647
Email: md@iringamc.go.tz
hakimiliki@2017Iringa Manispaa haki zote zimehifadhiwa