• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
HALMASHAURI YA MANISPAA YA IRINGA
HALMASHAURI YA MANISPAA YA IRINGA

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA OFISI YA RAIS TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA HALMASHAURI YA MANISPAA YA IRINGA

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Mipango Miji
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Afya
      • Maji
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Environment and Cleaning
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Kazi
    • Vitengo
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji nyuki
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Ufugaji
    • Kilimo
  • Huduma zetu
    • Huduma ya elimu
    • Huduma ya Afya
    • Huduma ya Maji
    • Huduma ya kilimo
    • Huduma ya Uvuvi
    • Huduma ya Ufugaji
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu
    • Ratiba ya Vikao
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati wa Halmashauri
    • Ripoti
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Maktaba ya picha
    • Video za shughuli za ofisi au Kitaifa
    • Hotuba

WANANCHI CHAGUENI VIONGOZI BORA UCHAGUZI SERIKALI ZA MTAA- MZAVA

Posted on: June 25th, 2024

“Kiongozi bora ni yule mwenye sifa na uwezo wa kuwaongoza wananchi, lakini pia ni yule ambaye sera na mipango yake inaakisi uhalisia wa changamoto za wananchi katika maeneo yao.”

Kauli hiyo imetolewa na Kiongozi wa Kitaifa wa Mbio za Mwenge wa Uhuru 2024, Ndg. Godfrey Mzava wakati akizungumza na wananchi wa Iringa katika eneo la bustani (Garden) iliyopo Kata ya Gangilonga Manispaa ya Iringa na kutoa ujumbe wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Mwaka 2024.

Mzava amesema, uchaguzi wa Serikali za Mitaa utafanyika hivi karibuni nchi nzima hivyo wananchi wachague kiongozi mwenye vitendo vizuri kwenye jamii, wanaokubalika lakini pia wenye sifa njema na wasichague viongozi wala rushwa na mafisadi.

Moja ya Askari Mkimbiza Mwenge Ndg. Makwaya Joseph ametoa salamu za mbio za Mwenge wa Uhuru 2024 kwa niaba ya Kiongozi Mkuu wa Kitaifa na kusema ni vyema wananchi washiriki katika mchakato wa uchaguzi wa Serikali za Mitaa ili kupata viongozi bora na wenye sifa.

"Wananchi mna wajibu wa kufanya mambo yafuatayo ili kuweza kutimiza uchaguzi wa Serikali za  Mitaa, Moja, kujitambua mwenyewe kama unaona una vigezo na sifa za kuwa kiongozi jambo lingine, twende tukachukue fomu kwa wingi kwenye vyama vyetu vya siasa na muhudhurie kampeni kwa wingi ili kusikiliza sera za viongozi hao, msipokee wala kutoa rushwa". Amesema Makwaya.

Aidha Makwaya ametoa rai kwa wananchi kuwa ifikapo siku ya uchaguzi wajitokeze kwa wingi kupiga kura ili kuweza kupata kiongozi bora.

Afisa Uchaguzi wa Halmashauri ya Manispaa ya Iringa, Ndg. Bernard Mwaituka amesema Manispaa ya Iringa inatarajia kushiriki uchaguzi wa Serikali za  Mitaa na mpaka sasa imekwishaandaa vituo 199 vya kuandikisha wapiga kura, pia  vituo 358 vimeandaliwa kwa ajili ya kupigia kura pamoja na kuanza maandalizi ya awali ya kufanikisha shughuli za uchaguzi.

Mwaituka ameendelea kutoa elimu ya uchaguzi kupitia vyombo vya habari na kuhamasisha wananchi kujiandaa kushiriki katika uchaguzi wa Serikali za Mitaa.

Wakimbiza Mwenge Kitaifa na wananchi waliojitokeza kwa wingi kuupokea Mwenge wa uhuru walikongwa mioyo yao kutokana na  umahiri wa  wanafunzi wa Shule ya Msingi Ipogolo wakiongozwa na mwalimu wao walivyoonyesha igizo la uhamasishaji wa wananchi kujitokeza kupiga kura na namna wananchi watakavyopiga kura katika uchaguzi ujao.

#tume ya uchaguzi_TZ

#Tume Huru ya Taifa ya uchaguzi

#ofisiyawazirimkuu

www.kazi.go.tz


Matangazo

  • TANGAZO LA KUONGEZWA MUDA WA KUCHUKUA FOMU YA UJENZI WA JENGO LA BIASHARA TEMBO BAR February 15, 2024
  • MATOKEO YA KIDATO CHA SITA, 2023/2024 July 13, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI July 17, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI July 23, 2024
  • Soma zote

Habari za Hivi punde

  • PPP CENTRE YATOA MAFUNZO KWA WATAALAMU IRINGA MC

    April 04, 2025
  • ALUTE: "HAKIKISHENI MIRADI INAKAMILIKA KWA WAKATI NA KWA UBORA"

    December 21, 2024
  • UCHAGUZI HURU NA WA HAKI UNAHITAJI USHIRIKISHAJI - RC SERUKAMBA

    October 10, 2024
  • MSIGALA AWAONYA MAAFISA MAENDELEO KUJIHUSISHA NA MIKOPO HEWA

    October 05, 2024
  • Soma zote

Video

MEYA WA MANISPAA KUZIPIGANIA TIMU ZA MKOA KUPANDA DARAJA
More Videos

Viunganisho vya Haraka

  • National Examination Council of Tanzania
  • Watumishi Portal
  • MATOKEO YA KIDATO CHA SITA,2023/2024
  • Sheria ndogo za Manispaa
  • Vivutio vya Utalii na Taarifda zake
  • Taarifa kwa vyombo vya Habari

Tovuti Zinazofanana

  • Goverment Website
  • TAMISEMI
  • Iringa Region Website
  • IMtv Fahari ya Iringa

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

https://bachelorthesiswritingservice.com

Location Map

Wasiliana nasi

    Iringa Municipal Council

    Sanduku la Posta: 162

    Telephone: +255-2702647

    Mobile: 255-2702647

    Email: md@iringamc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya usiri
    • Ukanusho
    • MMM
    • Ramani ya eneo
    • Huduma zetu

hakimiliki@2017Iringa Manispaa haki zote zimehifadhiwa