• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
HALMASHAURI YA MANISPAA YA IRINGA
HALMASHAURI YA MANISPAA YA IRINGA

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA OFISI YA RAIS TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA HALMASHAURI YA MANISPAA YA IRINGA

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Mipango Miji
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Afya
      • Maji
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Environment and Cleaning
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Kazi
    • Vitengo
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji nyuki
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Ufugaji
    • Kilimo
  • Huduma zetu
    • Huduma ya elimu
    • Huduma ya Afya
    • Huduma ya Maji
    • Huduma ya kilimo
    • Huduma ya Uvuvi
    • Huduma ya Ufugaji
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu
    • Ratiba ya Vikao
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati wa Halmashauri
    • Ripoti
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Maktaba ya picha
    • Video za shughuli za ofisi au Kitaifa
    • Hotuba

WANANCHI WAHIMIZWA KUWASILISHA CHANGAMOTO ZILIZOPO MAENEO YA HUDUMA

Posted on: June 3rd, 2024

Mkuu wa Wilaya ya Iringa Mhe. Kheri James amewataka wananchi kuwa na utaratibu wa kuwasilisha changamoto wanazozikuta kwenye maeneo mbalimbali ya huduma ili serikali iweze kuchukua hatua za kuboresha changamoto hizo.

Mhe. Kheri amesema hayo katika Mkutano na Wananchi wa Kata ya Ilala, uliofanyika siku ya tarehe 03/06/2024 katika Ofisi ya Kata ambapo amesema kuwa serikali hii ni serikali ya wananchi, inachaguliwa kwa kura za wananchi na inaongozwa kwa kodi za wananchi. Hivyo serikali inafanya utaratibu wa kuwasikiliza wananchi. Na ndio sababu katika maeneo ya huduma kama vile hospitali, ofisi za umma, polisi, taasisi za elimu na kwingineko kuwa serikali imeweka namba za mawasiliano pindi mwananchi anapokutana na kero zozote zile wawasiliane na uongozi kwa hatua zaidi.

"Ukienda hospitali, utakuta tumekuandikia pale namba za Mganga Mkuu wa Wilaya, Mganga Mfawidhi, na wengine wote tukiwa na dhamira ya unapofika hospitali, ukaona mwenendo wa huduma si mzuri. Unatakiwa kuwasiliana na sisi kupitia namba hizo, ili tujue hapo ulipofika changamoto ni nini, unasumbuliwa na nani ili tuchukue hatua za kuboresha changamoto hizo". Amesema Kheri.

Katika ziara hiyo ya kata ya Ilala Mkuu wa Wilaya amekagua miradi miwili ambayo ni ujenzi wa choo chenye matundu manne kilichojengwa eneo la Soko la Ilala ambalo limegharimu kiasi cha Shilingi Milioni 9, pamoja na Ujenzi wa Madarasa katika Shule ya Sekondari Mlamke.

Mstahiki Meya wa Halmashauri ya Manispaa ya Iringa Mhe. Ibrahim Ngwada amesema kuwa serikali inafanya jitihada mbalimbali kuboresha huduma kwa wananchi kama vile Ujenzi wa barabara za mitaa kwa kiwango cha lami, Ujenzi na Uboreshaji wa Shule za Msingi na Sekondari pamoja na Ujenzi wa Zahanati na

Vituo vya Afya.

Pia amesema katika kipindi hiki Halmashauri imepokea zaidi ya Shilingi Bilioni 2 kwa ajili ya uboreshaji wa hospitali ya Wilaya - Frelimo. Mpaka sasa hospitali ina   Wodi za Wanaume na Wanawake, Jengo la kujifungulia, Huduma ya Mama na Mtoto pamoja na Jengo la kuhifadhia maiti.

Akiwasilisha taarifa katika Mkutano huo, Diwani wa Kata ya Ilala Mhe. Conrad Mlowe amesema serikali imekamilisha ujenzi wa barabara kwa kiwango cha lami kwa wananchi wa Ilala, Ujenzi wa madarasa, pia imetafuta eneo la soko ambapo sasa hivi kufikia hatua ya ujenzi wa choo, kwa niaba ya wananchi ameiomba serikali kujenga uzio kwa Shule ya Sekondari Mlamke kwaajili ya usalama wa wanafunzi kwani mazingira si rafiki.

Mpaka sasa Mhe. Kheri ameshafanya ziara katika Kata ya Nduli, Mwangata, Mkimbizi, Mtwivila na Ilala huku lengo kuu la ziara hiyo ni Ukaguzi wa miradi ya Maendeleo ya Kata, Kuhamasisha Shughuli za Maendeleo na Kuwasikiliza Wananchi.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUONGEZWA MUDA WA KUCHUKUA FOMU YA UJENZI WA JENGO LA BIASHARA TEMBO BAR February 15, 2024
  • MATOKEO YA KIDATO CHA SITA, 2023/2024 July 13, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI July 17, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI July 23, 2024
  • Soma zote

Habari za Hivi punde

  • PPP CENTRE YATOA MAFUNZO KWA WATAALAMU IRINGA MC

    April 04, 2025
  • ALUTE: "HAKIKISHENI MIRADI INAKAMILIKA KWA WAKATI NA KWA UBORA"

    December 21, 2024
  • UCHAGUZI HURU NA WA HAKI UNAHITAJI USHIRIKISHAJI - RC SERUKAMBA

    October 10, 2024
  • MSIGALA AWAONYA MAAFISA MAENDELEO KUJIHUSISHA NA MIKOPO HEWA

    October 05, 2024
  • Soma zote

Video

MEYA WA MANISPAA KUZIPIGANIA TIMU ZA MKOA KUPANDA DARAJA
More Videos

Viunganisho vya Haraka

  • National Examination Council of Tanzania
  • Watumishi Portal
  • MATOKEO YA KIDATO CHA SITA,2023/2024
  • Sheria ndogo za Manispaa
  • Vivutio vya Utalii na Taarifda zake
  • Taarifa kwa vyombo vya Habari

Tovuti Zinazofanana

  • Goverment Website
  • TAMISEMI
  • Iringa Region Website
  • IMtv Fahari ya Iringa

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

https://bachelorthesiswritingservice.com

Location Map

Wasiliana nasi

    Iringa Municipal Council

    Sanduku la Posta: 162

    Telephone: +255-2702647

    Mobile: 255-2702647

    Email: md@iringamc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya usiri
    • Ukanusho
    • MMM
    • Ramani ya eneo
    • Huduma zetu

hakimiliki@2017Iringa Manispaa haki zote zimehifadhiwa