• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
HALMASHAURI YA MANISPAA YA IRINGA
HALMASHAURI YA MANISPAA YA IRINGA

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA OFISI YA RAIS TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA HALMASHAURI YA MANISPAA YA IRINGA

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Mipango Miji
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Afya
      • Maji
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Environment and Cleaning
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Kazi
    • Vitengo
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji nyuki
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Ufugaji
    • Kilimo
  • Huduma zetu
    • Huduma ya elimu
    • Huduma ya Afya
    • Huduma ya Maji
    • Huduma ya kilimo
    • Huduma ya Uvuvi
    • Huduma ya Ufugaji
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu
    • Ratiba ya Vikao
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati wa Halmashauri
    • Ripoti
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Maktaba ya picha
    • Video za shughuli za ofisi au Kitaifa
    • Hotuba

WANAWAKE MKOANI IRINGA WAJIPANGA KULETA MABADILIKO CHANYA KUELEKEA KILELE MAADHIMISHO YA MWANAMKE DUNIANI

Posted on: March 4th, 2021

"Wanawake tuzikamate nyumba, lakini pia tusiache kujishughulisha ili kuepukana na kunyanyasika kwani naamini sisi wanawake tukijiimarisha kiuchumi basi tutaheshimika"

Hayo yamezungumzwa leo na Mhe. Rita Kabati, Mbunge wa Viti Maalum Jimbo la Iringa Mjini akiwa Mgeni rasmi katika Kongamano la Wanawake kuelekea maadhimisho ya siku ya mwanamke duniani ifikapo  tarehe 8 Machi  mwaka huu

Aidha Mhe. Rita Kabati amewataka wanawake hao kuendelea kusaidiana katika changamoto wanazokutana nazo na sio kushirikiana wakati wa raha tu huku akiwataka  kujitokeza katika nafasi mbalimbali za uongozi zinapojitokeza

Nae Mwenyekiti wa UWT Mkoa wa Iringa Ndugu. Nicolina Lulandala amewaomba wanawake hao kujiwekea utamaduni washiriki katika masuala mbalimbali wanayoshirikishwa ili kuonesha wanauwezo pia amewataka kuendelea kushikamana wao kwa wao kwani kupitia umoja wao utaweza kuleta mabadiliko chanya katika familia zao,jamii na Taifa kwa ujumla

Sambamba hayo, pia kongamano hilo limeambatana na uwasilishwaji wa mada mbalimbali zilizofundishwa kwa wanawake waliohudhuria kama hamasa katika kuelekea siku hiyo kwa ujumbe usemao wanawake katika uongozi chachu kufikia dunia yenye usawa

Mada zilizowasilishwa ni pamoja na Ujasiriamali, Wanawake na Uongozi, Mirathi, Ndoa, Ukatili wa kijinsia, CHF Iliyoboreshwa, Elimu ya fedha, Lishe pamoja na Masuala ya Binti

Dkt. Given Msomba kutokea Chuo Kikuu cha Iringa ambae ni muwasilishaji wa mada ya Wanawake na Uongozi amewataka wanawake hao kujijengea maamuzi binafsi yenye hamasa ya kuleta mabadiliko na sio kubaki nyuma na kutegemea maamuzi yote kutoka kwa mwanaume hali ambayo itaonyesha kuwa  ishara ya sifa ya mwanamke kiongozi bora

Tiniel Mbaga, Afisa Utawi wa Jamii Manispaa ya Iringa amewataka wanawake kupinga ukatili dhidi yao na watoto wao pia kuyatolea taarifa katika vyombo vya kisheria ili kupata msaada kwa haraka mara baada ya matukio hayo kutokea

Kwa upande wake Bi. Flora Bruno ambaye ni Mratibu wa bima ya afya ya CHF Iliyoboreshwa Manispaa ya Iringa, amesema ili kuyafikia maendeleo kiujumla, afya ni jambo la kuzingatia hivyo ametoa elimu juu ya bima hiyo na amewataka wanawake hao kuziboresha afya zao na familia zao kwa kujiunga katika mfuko huo.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUONGEZWA MUDA WA KUCHUKUA FOMU YA UJENZI WA JENGO LA BIASHARA TEMBO BAR February 15, 2024
  • MATOKEO YA KIDATO CHA SITA, 2023/2024 July 13, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI July 17, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI July 23, 2024
  • Soma zote

Habari za Hivi punde

  • PPP CENTRE YATOA MAFUNZO KWA WATAALAMU IRINGA MC

    April 04, 2025
  • ALUTE: "HAKIKISHENI MIRADI INAKAMILIKA KWA WAKATI NA KWA UBORA"

    December 21, 2024
  • UCHAGUZI HURU NA WA HAKI UNAHITAJI USHIRIKISHAJI - RC SERUKAMBA

    October 10, 2024
  • MSIGALA AWAONYA MAAFISA MAENDELEO KUJIHUSISHA NA MIKOPO HEWA

    October 05, 2024
  • Soma zote

Video

MEYA WA MANISPAA KUZIPIGANIA TIMU ZA MKOA KUPANDA DARAJA
More Videos

Viunganisho vya Haraka

  • National Examination Council of Tanzania
  • Watumishi Portal
  • MATOKEO YA KIDATO CHA SITA,2023/2024
  • Sheria ndogo za Manispaa
  • Vivutio vya Utalii na Taarifda zake
  • Taarifa kwa vyombo vya Habari

Tovuti Zinazofanana

  • Goverment Website
  • TAMISEMI
  • Iringa Region Website
  • IMtv Fahari ya Iringa

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

https://bachelorthesiswritingservice.com

Location Map

Wasiliana nasi

    Iringa Municipal Council

    Sanduku la Posta: 162

    Telephone: +255-2702647

    Mobile: 255-2702647

    Email: md@iringamc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya usiri
    • Ukanusho
    • MMM
    • Ramani ya eneo
    • Huduma zetu

hakimiliki@2017Iringa Manispaa haki zote zimehifadhiwa