• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
HALMASHAURI YA MANISPAA YA IRINGA
HALMASHAURI YA MANISPAA YA IRINGA

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA OFISI YA RAIS TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA HALMASHAURI YA MANISPAA YA IRINGA

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Mipango Miji
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Afya
      • Maji
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Environment and Cleaning
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Kazi
    • Vitengo
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji nyuki
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Ufugaji
    • Kilimo
  • Huduma zetu
    • Huduma ya elimu
    • Huduma ya Afya
    • Huduma ya Maji
    • Huduma ya kilimo
    • Huduma ya Uvuvi
    • Huduma ya Ufugaji
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu
    • Ratiba ya Vikao
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati wa Halmashauri
    • Ripoti
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Maktaba ya picha
    • Video za shughuli za ofisi au Kitaifa
    • Hotuba

WATAALAM WATAKIWA KUTEKELEZA MASUALA YA LISHE ILI KUMALIZA UTAPIAMLO MANISPAA

Posted on: May 21st, 2021

Wito umetolewa kwa wataalam kutekeleza masuala ya Lishe katika jamii ili kupunguza na kutokomeza kabisa tatizo la utapiamlo katika Manispaa ya Iringa.

Wito huo umetolewa  leo tarehe 20.5.2021 na Mstahiki Meya wa Manispaa ya Iringa Mhe. Ibrahim Ngwada ambaye alikuwa Mwenyekiti wa Kikao hicho kilichofanyika katika ukumbi wa Chuo cha Afya kwenye  Tathmini ya Mikataba ya Lishe ambayo hufanyika kila robo lengo likiwa kuangalia utekelezaji wa viashiria vya Mkataba vilivyotekelezwa katika Kata zote

Mhe.Ngwada alieleza kwamba lazima agenda ya lishe ijadiliwe kwa weledi kwenye vikao vya maendeleo ya kata, alisisitiza watoto wote chini ya miaka mitano wapimwe hali zao za lishe kwenye siku za maadhimisho ya afya na lishe ili kuwaibua mapema wenye utapiamlo wapate matibabu kwa wakati.  Aliagiza uongozi wa kata uweze kuwasimamia wahudumu wa afya ngazi ya jamii watembelee kaya na kutoa elimu ya lishe pia kuhakikisha taarifa zote za lishe zibandikwe kwenye mbao za matangazo

Mwisho aliweza kueleza kwamba shule zote za msingi na sekondari zilizopo Manispaa ya iringa ziwe na bustani za mboga na matunda pamoja na kuhakikisha kwamba wanafunzi wote wanakula chakula wakiwa shule.

Anzael Msigwa Afisa lishe wa Manispaa amesema  mafanikio makubwa yaliyopatikana ni pamoja na usimamizi mzuri wa viashiria vya mkataba kutoka kwa wataalam waliopo kwenye kata pamoja na wahudumu wa afya ngazi ya jamii kutekeleza kwa wakati shughuli za lishe

Pia amezitaja changamoto kuwa ni  kuchelewa kuibuliwa kwa watoto wenye utapiamlo katika Mitaa na Kata hivyo kufanya kufika kwenye vituo vya Afya wakiwa na hali mbaya.

Eliud Mvela ni mhe.Diwani Kata ya Mkimbizi ameshauri watendaji na wahudumu wa afya msingi kushirikiana kwa pamoja kuibua watoto wenye utapiamlo ili waweze kupata tiba kwa wakati.


Kikao hicho kimewahusisha wadau mbalimbali wa Lishe wakiwemo  Waheshimiwa Madiwani, Wakuu wa Idara na vitengo,watendaji wa Kata Maafisa maendeleo ya jamii, wadau wa lishe ni pamoja na Papa yohana 23,Lishe Endelevu. Mbogamboga na Matunda,Save the Children,Tahea, Alamano na Call Africa.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUONGEZWA MUDA WA KUCHUKUA FOMU YA UJENZI WA JENGO LA BIASHARA TEMBO BAR February 15, 2024
  • MATOKEO YA KIDATO CHA SITA, 2023/2024 July 13, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI July 17, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI July 23, 2024
  • Soma zote

Habari za Hivi punde

  • PPP CENTRE YATOA MAFUNZO KWA WATAALAMU IRINGA MC

    April 04, 2025
  • ALUTE: "HAKIKISHENI MIRADI INAKAMILIKA KWA WAKATI NA KWA UBORA"

    December 21, 2024
  • UCHAGUZI HURU NA WA HAKI UNAHITAJI USHIRIKISHAJI - RC SERUKAMBA

    October 10, 2024
  • MSIGALA AWAONYA MAAFISA MAENDELEO KUJIHUSISHA NA MIKOPO HEWA

    October 05, 2024
  • Soma zote

Video

MEYA WA MANISPAA KUZIPIGANIA TIMU ZA MKOA KUPANDA DARAJA
More Videos

Viunganisho vya Haraka

  • National Examination Council of Tanzania
  • Watumishi Portal
  • MATOKEO YA KIDATO CHA SITA,2023/2024
  • Sheria ndogo za Manispaa
  • Vivutio vya Utalii na Taarifda zake
  • Taarifa kwa vyombo vya Habari

Tovuti Zinazofanana

  • Goverment Website
  • TAMISEMI
  • Iringa Region Website
  • IMtv Fahari ya Iringa

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

https://bachelorthesiswritingservice.com

Location Map

Wasiliana nasi

    Iringa Municipal Council

    Sanduku la Posta: 162

    Telephone: +255-2702647

    Mobile: 255-2702647

    Email: md@iringamc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya usiri
    • Ukanusho
    • MMM
    • Ramani ya eneo
    • Huduma zetu

hakimiliki@2017Iringa Manispaa haki zote zimehifadhiwa