• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
HALMASHAURI YA MANISPAA YA IRINGA
HALMASHAURI YA MANISPAA YA IRINGA

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA OFISI YA RAIS TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA HALMASHAURI YA MANISPAA YA IRINGA

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Mipango Miji
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Afya
      • Maji
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Environment and Cleaning
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Kazi
    • Vitengo
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji nyuki
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Ufugaji
    • Kilimo
  • Huduma zetu
    • Huduma ya elimu
    • Huduma ya Afya
    • Huduma ya Maji
    • Huduma ya kilimo
    • Huduma ya Uvuvi
    • Huduma ya Ufugaji
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu
    • Ratiba ya Vikao
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati wa Halmashauri
    • Ripoti
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Maktaba ya picha
    • Video za shughuli za ofisi au Kitaifa
    • Hotuba

WAZAZI WALINDENI WATOTO DHIDI YA VITENDO VYA UKATILI WA KIJINSIA-MBUNGE MSAMBATAVANGU

Posted on: July 8th, 2023

MBUNGE wa Jimbo la Iringa Mjini Dkt.Jesca Msambatavangu amewataka wazazi na walezi kuwalinda watoto dhidi ya vitendo vya ukatili wa kijinsia ambavyo vimekwa vikiripotiwa kuongezeka siku hadi siku katika baadhi ya maeneo Manispaa ya Iringa.

Msambatavangu ameyasema hayo Julai 8 2023. Katika Kata ya Nduli  Mtaa wa Msisina na Mtalagala wakati akihitimisha ziara yake ya Siku 8 iliyofanyika  Mtaa kwa Mtaa ,Kata kwa Kata kwa lengo la kusikiliza kero na changamoto za wananchi pamoja na kuzitafutia ufumbuzi, huku akiwaeleza namna ambavyo Serikali ya awamu ya sita  ilivyotoa zaidi ya shs.bilioni 39 kwa ajili ya utekelezaji wa miradi ya maendeleo katika Sekta ya Elimu,Afya na miundombinu Katika Halimashauri.

Msambatavangu amesema kumekuwa na Wimbi la vitendo vya ukatili wanaofanyiwa watoto kama ubakaji na ulawiti hivyo amewaasa wazazi na Walezi kuwa makini kuhakikisha wanawalinda watoto wasifanyiwe vitendo hivyo kwani vinaathiri afya ya mwili, akili na kumfanya mtoto kukosa ujasiri.

'Nawaomba sana walindeni watoto wapeni haki zote za msingi kwani mkiwatendea mema watoto hawa mmemtendea Mungu na atawabariki,mkitaka laana basi watendeeni watoto hawa mabaya alisema Msambatavangu.'

Kwa upande wa utekelezaji wa miradi ya Maendeleo Dkt.Jesca amesema katka kipindi cha mwaka 2021 hadi  Juni 2023 Miradi mingi ya Maendeleo imetekelezwa na Halmashauri kutokana na Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan kumwaga fedha nyingi katika  ili kuwasogezea karibu wananchi huduma za vituo vya afya,zahanati,madarasa na  kuboresha miundo mbunu ya barabara .

Awali Diwani wa Kata ya Nduli Mhe.Bashiri  Mtove amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt.Samia Suluhu Hassan kwa kutoa fedha za Miradi mbali mbali ya aendeleo ambapo Kata ya Nduli imenufaika na fedha  hizo kwa ujenzi wa Shule ya Sekondari ya Nduli,zahanati ya Mtalagala na Barabara ya Mgongo-msisina na upanuzi wa uwanja wa Ndege Nduli ambao uko hatua ya ukamilishaji.

Wakitoa kero na changamoto zao wananchi wa Msisina na Mtalagala wamesema kero kubwa  ni ukosefu wa maji,umeme na ukosefu wa shule ya Sekondari hivyo kupelekea wanafunzi kutembea umbali mrefu kufika shuleni.

Akijibu kero hizo Mbunge amesema kuhusu Shule eneo limepattikana hivyo waanze utaratibu wa ujenzi kwa kushirikiana na ofisi ya Kata huku akiahidi kutafuta ufumbuzi changamoto ya maji na umeme.

Ziara ya Mbunge wa Jimbo la Iringa Mjini iliyoanza Julai 1 2023 imemalizika leo Julai 8 2023 ambapo iliwashirikisha viongozi mbali mbali wa chama na Serikali.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUONGEZWA MUDA WA KUCHUKUA FOMU YA UJENZI WA JENGO LA BIASHARA TEMBO BAR February 15, 2024
  • MATOKEO YA KIDATO CHA SITA, 2023/2024 July 13, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI July 17, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI July 23, 2024
  • Soma zote

Habari za Hivi punde

  • PPP CENTRE YATOA MAFUNZO KWA WATAALAMU IRINGA MC

    April 04, 2025
  • ALUTE: "HAKIKISHENI MIRADI INAKAMILIKA KWA WAKATI NA KWA UBORA"

    December 21, 2024
  • UCHAGUZI HURU NA WA HAKI UNAHITAJI USHIRIKISHAJI - RC SERUKAMBA

    October 10, 2024
  • MSIGALA AWAONYA MAAFISA MAENDELEO KUJIHUSISHA NA MIKOPO HEWA

    October 05, 2024
  • Soma zote

Video

MEYA WA MANISPAA KUZIPIGANIA TIMU ZA MKOA KUPANDA DARAJA
More Videos

Viunganisho vya Haraka

  • National Examination Council of Tanzania
  • Watumishi Portal
  • MATOKEO YA KIDATO CHA SITA,2023/2024
  • Sheria ndogo za Manispaa
  • Vivutio vya Utalii na Taarifda zake
  • Taarifa kwa vyombo vya Habari

Tovuti Zinazofanana

  • Goverment Website
  • TAMISEMI
  • Iringa Region Website
  • IMtv Fahari ya Iringa

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

https://bachelorthesiswritingservice.com

Location Map

Wasiliana nasi

    Iringa Municipal Council

    Sanduku la Posta: 162

    Telephone: +255-2702647

    Mobile: 255-2702647

    Email: md@iringamc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya usiri
    • Ukanusho
    • MMM
    • Ramani ya eneo
    • Huduma zetu

hakimiliki@2017Iringa Manispaa haki zote zimehifadhiwa