• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
HALMASHAURI YA MANISPAA YA IRINGA
HALMASHAURI YA MANISPAA YA IRINGA

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA OFISI YA RAIS TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA HALMASHAURI YA MANISPAA YA IRINGA

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Mipango Miji
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Afya
      • Maji
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Environment and Cleaning
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Kazi
    • Vitengo
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji nyuki
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Ufugaji
    • Kilimo
  • Huduma zetu
    • Huduma ya elimu
    • Huduma ya Afya
    • Huduma ya Maji
    • Huduma ya kilimo
    • Huduma ya Uvuvi
    • Huduma ya Ufugaji
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu
    • Ratiba ya Vikao
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati wa Halmashauri
    • Ripoti
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Maktaba ya picha
    • Video za shughuli za ofisi au Kitaifa
    • Hotuba

WAZAZI WAMESHAURIWA KUTENGA MUDA WA KUKAA NA WATOTO WAO

Posted on: May 24th, 2024

Mkuu wa Wilaya ya Iringa, Komred Kheri James amewashauri Wazazi kutenga muda wa kukaa na watoto wao na kujenga mahusiano mazuri ya kirafiki na ya ukaribu ili kuwaweka karibu watoto na kuwafanya wawajue wazazi wao vizuri.

Ametoa ushauri huo wakati wa kuweka Jiwe la Msingi katika Shule mpya ya Sekondari ya Kwavava iliyopo Kata ya Kitwiru Halmashauri ya  Manispaa ya Iringa huku akiwaasa kina mama wanaolea watoto peke yao kuepuka kuvunja mahusiano baina ya baba na watoto kwani kufanya hivyo ni kuwanyima watoto haki yao ya msingi ya malezi.

“Malezi bora ya watoto yanatoka kwa wazazi wa pande zote mbili, wakati akinamama wanawafundisha watoto huruma na upendo lakini ujasiri na mapambano hujifunza kutoka kwa akinababa na hii huwafanya watoto kuwa watu bora zaidi katika maisha yao na kwamba watoto ni watu ambao tutakuwa nao katika nyakati zote” Amesema Komred Kheri

Aidha amewataka watoto ambao ni wanafunzi wa shule hiyo kusoma kwa bidii sana na kujipanga kufaulu katika masomo yao, kwa kuwapenda sana walimu wao na kufanya hivyo itawasaidia kulipenda somo la mwalimu husika tofauti na hivyo ni mwanzo wa kuwapelekea kufeli, pia amewashauri kujijengea ujasiri wa kufuatilia kwa kuwaomba msaada walimu wao katika masomo wasiyoyaelewa.

Mwalimu Mkuu wa Shule ya Sekondari ya Kwavava Ndg. Vick Kasanga, amesema Mradi huo umegharimu zaidi ya Tsh. Milioni 500 na Malengo ya Mradi huo wa ujenzi wa Shule ulianza kutekelezwa Agosti 2023 na kukamilika kwa asilimia 98, pamoja na kuboresha mazingira ya kujifunza na kujifunzia, kupunguza msongamano darasani na kusogeza karibu huduma ya elimu kwa jamii.

Mwl. Kasanga amebainisha kuwa Shule ya Sekondari ya Kwavava imeanza kutoa elimu kwa Mwaka wa masomo 2024 kwa kidato cha kwanza na hadi sasa wana jumla ya wanafunzi 105 na walimu watano (5)

Kwa upande wake Diwani wa Kata ya Kitwiru Mhe. Hamza Mwamhehe amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuwajali wananchi wa Kata hiyo kwani katika kipindi kifupi cha Uongozi wake ametoa fedha nyingi katika Sekta ya Elimu na Afya.

Uwekaji wa Jiwe la Msingi umeshuhudiwa na Viongozi wa Chama cha Mapinduzi ngazi ya Kata, Wenyeviti wa Serikali za Mitaa na Kamati ya Ulinzi na Usalama Wilaya, Kamati ya Ujenzi, Walimu, Wanafunzi, Watendaji wa Mitaa na Mtendaji wa Kata pamoja na wazazi.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUONGEZWA MUDA WA KUCHUKUA FOMU YA UJENZI WA JENGO LA BIASHARA TEMBO BAR February 15, 2024
  • MATOKEO YA KIDATO CHA SITA, 2023/2024 July 13, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI July 17, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI July 23, 2024
  • Soma zote

Habari za Hivi punde

  • PPP CENTRE YATOA MAFUNZO KWA WATAALAMU IRINGA MC

    April 04, 2025
  • ALUTE: "HAKIKISHENI MIRADI INAKAMILIKA KWA WAKATI NA KWA UBORA"

    December 21, 2024
  • UCHAGUZI HURU NA WA HAKI UNAHITAJI USHIRIKISHAJI - RC SERUKAMBA

    October 10, 2024
  • MSIGALA AWAONYA MAAFISA MAENDELEO KUJIHUSISHA NA MIKOPO HEWA

    October 05, 2024
  • Soma zote

Video

MEYA WA MANISPAA KUZIPIGANIA TIMU ZA MKOA KUPANDA DARAJA
More Videos

Viunganisho vya Haraka

  • National Examination Council of Tanzania
  • Watumishi Portal
  • MATOKEO YA KIDATO CHA SITA,2023/2024
  • Sheria ndogo za Manispaa
  • Vivutio vya Utalii na Taarifda zake
  • Taarifa kwa vyombo vya Habari

Tovuti Zinazofanana

  • Goverment Website
  • TAMISEMI
  • Iringa Region Website
  • IMtv Fahari ya Iringa

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

https://bachelorthesiswritingservice.com

Location Map

Wasiliana nasi

    Iringa Municipal Council

    Sanduku la Posta: 162

    Telephone: +255-2702647

    Mobile: 255-2702647

    Email: md@iringamc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya usiri
    • Ukanusho
    • MMM
    • Ramani ya eneo
    • Huduma zetu

hakimiliki@2017Iringa Manispaa haki zote zimehifadhiwa