• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
HALMASHAURI YA MANISPAA YA IRINGA
HALMASHAURI YA MANISPAA YA IRINGA

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA OFISI YA RAIS TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA HALMASHAURI YA MANISPAA YA IRINGA

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Mipango Miji
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Afya
      • Maji
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Environment and Cleaning
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Kazi
    • Vitengo
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji nyuki
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Ufugaji
    • Kilimo
  • Huduma zetu
    • Huduma ya elimu
    • Huduma ya Afya
    • Huduma ya Maji
    • Huduma ya kilimo
    • Huduma ya Uvuvi
    • Huduma ya Ufugaji
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu
    • Ratiba ya Vikao
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati wa Halmashauri
    • Ripoti
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Maktaba ya picha
    • Video za shughuli za ofisi au Kitaifa
    • Hotuba

WAZIRI ULEGA APONGEZA JITIHADA ZA MANISPAA MIRADI YA MAENDELEO

Posted on: September 17th, 2024

Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mhe. Abdallah Ulega ametoa pongezi kwa viongozi wa Halmashauri ya Manispaa ya Iringa kwa utekelezaji wa miradi ya maendeleo ikiwemo ujenzi wa Daraja, Bweni pamoja na Stoo ya dawa  miradi ambayo itawanufaisha wakazi wa Iringa.

Waziri Ulega ametoa pongezi hizo wakati akizungumza na wananchi wa Iringa katika Mkutano wa hadhara, uliofanyika katika Uwanja wa shule ya Msingi Muungano iliyopo Kata ya Mwangata Tarehe 17.09.2024.

"Yanapofanywa mazuri lazima tupongezane, hiyo inatoa kasi zaidi ya kufanya vizuri zaidi, nawashukuruni sana wanaIringa, nimekagua, nimefungua na kuweka mawe ya msingi katika  miradi ya maendeleo ya  ujenzi wa Daraja Kigonzile, Bweni la Mawelewele na Stoo ya Dawa Hospitali ya Frelimo. Miradi hiyo inakwenda kutatua kero na changamoto za watu. Hakika nmeridhia, mmefanya vizuri. Nawapongeza sana. Ntazifikisha salamu zenu kwa Mheshimiwa  Rais". Amesema Ulega.

Aidha, Ulega amewaasa wananchi kuchagua viongozi bora, wachapakazi, wazalendo, wabunifu na wenye uwezo wa kusimamia maendeleo ya watu katika uchaguzi ujao wa Serikali za Mitaa utakaofanyika mwishoni mwa Mwezi Novemba 2024. Vilevile wahakikishe wanaendesha uchaguzi kwa amani na utulivu ili kulinda amani ya Nchi yetu.

Wakati huo, Mkuu wa Mkoa wa Iringa Mhe, Peter Serukamba ametoa shukrani kwa  Rais Samia Suluhu kwa kuleta fedha kwa ajili ya utekelezaji wa miradi ya maendeleo ya wananchi kwani anapambana katika kuondoa maadui watatu katika Nchi ya Tanzania ambao ni "Ujinga, Maradhi na Umaskini". Ndio maana amejikita kuleta fedha hasa katika miradi ya Elimu kwa ajili ya kufuta Ujinga, miradi ya Afya kwa kuondoa maradhi pamoja na kutoa mikopo kwa kina mama,watu wenye ulemavu na vijana kwa lengo la kuondoa umaskini.

Naye, Mbunge wa Jimbo la Iringa Mjini Mhe, Jesca Msambatavangu ameushukuru uongozi wa awamu ya sita kwa kuzindua bohari ya Dawa ya wilaya(Frelimo) ikiwa ni mkakati wa kupunguza malalamiko na kutatua changamoto ya upatikanaji wa dawa na vifaa tiba kwani  kutokana na utunzaji wa dawa kwenye bohari hiyo itakuwa njia bora kwa zahanati na vituo vya afya vilivyopo kwenye Halmashauri yetu kuweza kupata dawa na vifaa tiba kwa wakati na kwa urahisi hivyo kurahisisha huduma za matibabu kwa wananchi wa Iringa.

Katibu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM ) Wilaya ya Iringa, Mjini Ndg. Hassan Makoba amesema kuwa ziara hiyo ya Mheshimiwa waziri ni pamoja na kukamilisha ilani ya CCM 2020-2025 ambapo amekuja kuthibitisha kama ilani hiyo imetekelezwa na kuhakikisha zile fedha nyingi ambazo zinaletwa na Mheshimiwa Rais kwenye Hlalmashauri na Mkoa wa Iringa kupitia usimamizi wa Madiwani na wabunge zimekwenda kutatua kero na kutekelezwa kwa vitendo ikiwemo ujenzi wa Daraja, Bweni na Stoo ya dawa.

Miradi mitatu iliyozinduliwa na kuweka jiwe la msingi na waziri huyo ni Ujenzi wa Daraja la Kigonzile lenye (urefu wa mita 10.8) ambao  umegharimu Shilingi Milioni 119, Bweni la Shule ya Sekondari  Mawelewele Shilingi Milioni 112 na Stoo ya kuhifadhi dawa Hospitali ya Frelimo uliogharimu Shilingi Milioni 160. Miradi hiyo imeshakamilika kwa ajili ya kuwahudumia wananchi wa Iringa

Matangazo

  • TANGAZO LA KUONGEZWA MUDA WA KUCHUKUA FOMU YA UJENZI WA JENGO LA BIASHARA TEMBO BAR February 15, 2024
  • MATOKEO YA KIDATO CHA SITA, 2023/2024 July 13, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI July 17, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI July 23, 2024
  • Soma zote

Habari za Hivi punde

  • PPP CENTRE YATOA MAFUNZO KWA WATAALAMU IRINGA MC

    April 04, 2025
  • ALUTE: "HAKIKISHENI MIRADI INAKAMILIKA KWA WAKATI NA KWA UBORA"

    December 21, 2024
  • UCHAGUZI HURU NA WA HAKI UNAHITAJI USHIRIKISHAJI - RC SERUKAMBA

    October 10, 2024
  • MSIGALA AWAONYA MAAFISA MAENDELEO KUJIHUSISHA NA MIKOPO HEWA

    October 05, 2024
  • Soma zote

Video

MEYA WA MANISPAA KUZIPIGANIA TIMU ZA MKOA KUPANDA DARAJA
More Videos

Viunganisho vya Haraka

  • National Examination Council of Tanzania
  • Watumishi Portal
  • MATOKEO YA KIDATO CHA SITA,2023/2024
  • Sheria ndogo za Manispaa
  • Vivutio vya Utalii na Taarifda zake
  • Taarifa kwa vyombo vya Habari

Tovuti Zinazofanana

  • Goverment Website
  • TAMISEMI
  • Iringa Region Website
  • IMtv Fahari ya Iringa

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

https://bachelorthesiswritingservice.com

Location Map

Wasiliana nasi

    Iringa Municipal Council

    Sanduku la Posta: 162

    Telephone: +255-2702647

    Mobile: 255-2702647

    Email: md@iringamc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya usiri
    • Ukanusho
    • MMM
    • Ramani ya eneo
    • Huduma zetu

hakimiliki@2017Iringa Manispaa haki zote zimehifadhiwa