• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
HALMASHAURI YA MANISPAA YA IRINGA
HALMASHAURI YA MANISPAA YA IRINGA

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA OFISI YA RAIS TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA HALMASHAURI YA MANISPAA YA IRINGA

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Mipango Miji
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Afya
      • Maji
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Environment and Cleaning
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Kazi
    • Vitengo
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji nyuki
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Ufugaji
    • Kilimo
  • Huduma zetu
    • Huduma ya elimu
    • Huduma ya Afya
    • Huduma ya Maji
    • Huduma ya kilimo
    • Huduma ya Uvuvi
    • Huduma ya Ufugaji
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu
    • Ratiba ya Vikao
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati wa Halmashauri
    • Ripoti
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Maktaba ya picha
    • Video za shughuli za ofisi au Kitaifa
    • Hotuba

ZAIDI YA MITI 200 YAPANDWA KITUO CHA AFYA MKOGA

Posted on: March 6th, 2024

ZAIDI YA MITI 200 YAPANDWA KITUO CHA AFYA MKOGA

Katika kuelekea kilele cha Maadhimisho ya Siku ya Mwanamke Duniani,  wanawake wa Halmashauri ya Manispaa ya Iringa wametumia fursa hiyo kupanda miti zaidi ya 200 siku ya Jumatano  tarehe 06 Machi, 2024 katika kituo cha afya Mkoga kilichopo kata ya Isakalilo Mjini Iringa.

Akizungumza katika zoezi hilo la upandaji Miti, Mratibu wa sherehe ya siku ya Mwanamke Duniani wa Manispaa ya Iringa, Ndg. Sunday Mtamakaya amesema kabla ya kilele cha  Maadhimisho ya sherehe ya Mwanamke Manispaa ya Iringa huwa inaandaa shughuli mbalimbali. ambapo kwa mwaka huu walipanga kutembelea Mbuga za wanyama za Mikumi tarehe 02 Machi na tayari zoezi hilo  limeshafanyika, 05 Machi limefanyika kongamano la wanawake na tarehe 06 Machi ni zoezi la upandaji wa miti kwenye Mituo cha Afya Mkoga kwa lengo la kutunza Mazingira.

"Leo wanawake wote wa Manispaa tumeungana pamoja ili kuboresha Mazingira kama kauli ya Mama Samia Sulluhu inavyosema kuwa kila iitwapo leo tukumbuke kupanda Miti. Lakini pia tunapopanda miti ya matunda ili wagonjwa waweze kula na kuboresha afya". Amesema Mtamakaya


Aidha, Afisa Misitu wa Halmashauri ya Manispaa ya Iringa Ndg, Enock Changime amesema yeye kama Mtaalamu wa Misitu ameshiriki kwenye zoezi hilo ili kuweza kuwaongoza na kuwasaidia kina mama na hatimaye zoezi hilo liende vizuri.


Pia, Akitoa elimu ya upandaji miti kwa wakina Mama amesema kuwa miti ina faida nyingi ambapo  itanufaisha wagonjwa na kuboresha Mazingira kiujumla.


"Faida ya upandaji wa miti ambayo tumepanda eneo hili, kwanza Kuna faida za moja kwa moja ambazo wagonjwa watakaokuja eneo hili watanufaika kwa maana ya matunda, pili wataweza kupata kivuli na tatu wataweza kupata hewa safi", Amesema Changime.


Pia, amesema kuwa wagonjwa watakaofika eneo hilo watapewa miche ya miti kwa ajili ya kupanda kwenye maeneo yao. Mbali na hilo, amewashauri wananchi wajitokeze kwa wingi kwenye mazoezi mengine kama hayo.


Kwa upande wake, Afisa Afya kata ya Isakalilo Ndg, Matilda Kasanga ameushukuru uongozi wa Manispaa ya Iringa hasa Serikali ya Mama Samia kwa kuweza kujenga kituo cha afya cha Mkoga  kwani kitasaidia kuboresha huduma za afya kwa wananchi wa eneo hilo hususani kina mama, wajawazito na watoto ambao ni walengwa wakuu.


Kasanga amemshukuru Mkurugenzi wa Manispaa ya Iringa kwa kuweza kuwapatia Miti katika Kituo hicho cha afya ili kuboresha Mazingira na ametoa wito kwa wananchi wa eneo hilo watunze kituo hicho.


Naye mkazi wa kata hiyo, Ndg, Twina Nyaulembo ameishukuru Serikali kwa kupeleka kituo cha Afya kwenye Kata hiyo. Pia amewapongeza  wanawake kwa upandaji wa Miti na ataendelea kuelimisha na kuhamasisha jamii ili kila mmoja aone umuhimu wa kupanda miti.


Maadhimisho ya Siku ya Mwanamke  Duniani hufanyika Tar 08 Machi kila mwaka, ambapo wanawake wa Manispaa ya Iringa wataungana na Mkoa kuadhimisha sherehe hizo kimkoa katika uwanja wa Samora


 Kauli mbiu ya mwaka huu inasema, "Wekeza kwa Mwanamke Kuharakisha Maendeleo ya Taifa na Ustawi wa Jamii".

Matangazo

  • TANGAZO LA KUONGEZWA MUDA WA KUCHUKUA FOMU YA UJENZI WA JENGO LA BIASHARA TEMBO BAR February 15, 2024
  • MATOKEO YA KIDATO CHA SITA, 2023/2024 July 13, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI July 17, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI July 23, 2024
  • Soma zote

Habari za Hivi punde

  • PPP CENTRE YATOA MAFUNZO KWA WATAALAMU IRINGA MC

    April 04, 2025
  • ALUTE: "HAKIKISHENI MIRADI INAKAMILIKA KWA WAKATI NA KWA UBORA"

    December 21, 2024
  • UCHAGUZI HURU NA WA HAKI UNAHITAJI USHIRIKISHAJI - RC SERUKAMBA

    October 10, 2024
  • MSIGALA AWAONYA MAAFISA MAENDELEO KUJIHUSISHA NA MIKOPO HEWA

    October 05, 2024
  • Soma zote

Video

MEYA WA MANISPAA KUZIPIGANIA TIMU ZA MKOA KUPANDA DARAJA
More Videos

Viunganisho vya Haraka

  • National Examination Council of Tanzania
  • Watumishi Portal
  • MATOKEO YA KIDATO CHA SITA,2023/2024
  • Sheria ndogo za Manispaa
  • Vivutio vya Utalii na Taarifda zake
  • Taarifa kwa vyombo vya Habari

Tovuti Zinazofanana

  • Goverment Website
  • TAMISEMI
  • Iringa Region Website
  • IMtv Fahari ya Iringa

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

https://bachelorthesiswritingservice.com

Location Map

Wasiliana nasi

    Iringa Municipal Council

    Sanduku la Posta: 162

    Telephone: +255-2702647

    Mobile: 255-2702647

    Email: md@iringamc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya usiri
    • Ukanusho
    • MMM
    • Ramani ya eneo
    • Huduma zetu

hakimiliki@2017Iringa Manispaa haki zote zimehifadhiwa